Je, Sokoine alikufa kwa ajali ya gari, Au aliuawa kwa kupigwa risasi 18 kifuani?

Sikio likitaka kuzidi kichwa, Nyerere alifanya sawa, hata kama aliuza meli kijana wake aliona ni sawa kumvua nguo? Alioashwa kumwambia na wakamaliza kimya kimya badala ya kuketa mtafaruku.Ili kulinda heshima ya nchi alipashwa kuwa ELIMINATED, hiyo ndiyo kamini.Pesa kama hiyo unakuwa ilienda kuwasaidia wapiganaji wa ukombozi kidini mwa Africa kwa siri baada ya kugundua jamaa ni mlopokaji.Hapo wazee hawakula chichote, nia ni kusaidia watu tu.
 
Ila mleta mada naona unapotosha tu. Yaliyopita si ndwele tugange yajayo. Jiandae kikamilifu siku yako ikiwadia. Ndio Dunia
 
Daaah
Mkuu, umesaga kunguni vya kutosha.

Haya yote mngeyaleta enzi zile hata kipindi cha awamu ya kwanza ya Mkapa tungewaelewa.

Lakini kwa sasa ni kama kuna kisasi fulani mnakifanya kupitia huu utunzi mahiri
Du wewe...angeleta lini hili bandiko??? Unafikiri bandiko kama hili nyakati zile JF ingekuwa historia na Mwanandishi mwenyewe nae hivyohivyo......wakati ule ilikuwa hatareeee....wajameni.
 
Nyerere aliyeweza kupiga simu benki kuu na kuagiza apewe fedha anazotaka kwa sababu za "usalama wa taifa" alihitaji kuuza meli ili aibe hela za umma?

Ushawahi kufika kwa Nyerere ukaona alivyoishi?
Hawa ni ile timu ya chafua Nyerere Ili magufuli aonekane bora..Nyerere hana mfano kwenye hii nchi
 
Mleta habari ni mwenye chuki kubwa na Nyerere au mbabaishaji, iweje leo ndio alete huo upupu alikuwa wapi miaka yote? na anamuadress Magufuli leo hii!!! ovyo sana mleta uzi huyu
 
Mleta habari ni mwenye chuki kubwa na Nyerere au mbabaishaji, iweje leo ndio alete huo upupu alikuwa wapi miaka yote? na anamuadress Magufuli leo hii!!! ovyo sana mleta uzi huyu

Kashindwa kujibu hoja yangu
 
Hili andiko linalomtaja Magufuli anaimba nyimbo wakati alishafariki liliandikwa lini?
Magufuli mwenyewe nae aliuwawa sema yeye kisayansi zaidi na ikachagizwa covid ndio source ya kifo chake Ila nae kafa koutata na waliomuua wanadhihirika hadharani kabisa kwanini waliamua afe, tofauti ya kifo chake na sokoine ni kwamba JPM ameuwawa kisayansi zaidi Ila walizingua kutotutudanganya kwamba amelazwa tumuombee na Sasa wanapangua aliyoyafanya maana aliwachelewesha sio Kama Sokoine waliemtandika risasi hadharani huko Morogoro Dakawa.
Dunia hii ukienda kinyume na matajiri na ukajifanya unatetea wanyonge lazima uundiwe zengwe tu, sio Tanzania pekee watetezi wa wananchi huuwawa Bali hata Marekani Marais kadhaa waliojifaragua kuwa upande wa wananchi waliishia vifo vya utata.

Halafu huyo Nyerere alikuwa akiiba hizo pesa anatambikia au? Mbona maisha yake na familia yake hayahitaji microscope kuyaona kwamba ni maisha ya kawaida kabisaaaaa wanae nao kawaida kabisa tofauti na Marais wengine walioufanya urais wao ni ufalme na familia zao zikaandaliwa urithi wa Mali na madaraka ya kudumu?
Labda useme una chuki tu na Mzanaki wa watu Ila kuhusu kufisadi pesa umemsingizia parefu.
Mafisadi huwaoni kabisaaa mpaka umtaje Mwalimu?
Bila shaka baada ya kuona Sokoine ameshauwawa na hakutaka taharuki akatumia busara tu kwamba ajali kuepusha tension.
 
"Ikumbukwe kwamba wakati anaondoka kwenda Dodoma Marehemu Sokoine alisema maneo ya mwisho yafuatayo:Nikimaliza kuwatumbua majipu mawaziri wangu, basi napanda juu nikamtumbue majipu Mwalimu Nyerere kwa vile anaonekana siyo msafi"
Hii itakuwa chai hii
 
Nyerere aliyeweza kupiga simu benki kuu na kuagiza apewe fedha anazotaka kwa sababu za "usalama wa taifa" alihitaji kuuza meli ili aibe hela za umma?

Ushawahi kufika kwa Nyerere ukaona alivyoishi?
Ajabu Sana huyu jamaa
 
Taarifa kama hizi huwa sio za kuweka hadharani,hazina faida zaidi zinaweza kuivunja nchi,
Watu kama wewe inabidi mnyamazishwe kabisa,
 
usi mchafue huyu mzee kwa hadithi zako za kusadikika mwacheni apumzike kwa amani r.I.p Mwl Nyerere, r.I.p Sokoine, ukitafutwa na wazee utolee maelezo ulicho andika humu usije leta zile story za mniombee, nchi ina wenyewe hii, kula ugali wako kwa amani.
 
Nikimaliza kuwatumbua majipu mawaziri wangu, basi napanda juu nikamtumbue majipu Mwalimu Nyerere kwa vile anaonekana siyo msafi
Hahaaaa! 🤣🤣 Huyu Nyerere atakuwa alikuwa Raisi wa ajabu na Sokoine mweneyew alikuwa zoba kweli - kwa maneno haya yasemwe hadharani.
Mimi nilikuwa na umri wa miaka 27 na niko Chuoni wakati huo na tena Dar na nilikuwa msomaji sana wa magazeti na kusikiliza radio maneneo haya ya Sokoine sikuwahi kuyasikia.
Mto mada umetubebesha magunia na labda nia yako ilikuwa ni kujaribu kuzima legacy ya Mwalimu Nyerere kwa ajili ya kumbeba Mwendazake ambaye wewe ni muumini wake.
 

Ukiona utopolo wa aina hiyo tambua hao ni wafuasi wa mwendazake kazini.

Wako mikao ya kuhimiza umilele wa legacy zake kana kwamba za kina Hitler au SABAYA zitakuja kubadilika 😁😁.
 
Basi nikajua usingizi unanifanya nisikumuelewe mleta mmada, huu ni upotoshaji mkubwa sana
 


Luuu, 😱😱
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…