Uchaguzi 2020 Je, Tanzania tuna upinzani makini, upinzani wa kweli wa kuing'oa CCM madarakani au bado sana? Nilichoshuhudia leo uzinduzi CHADEMA, kiukweli...

Mti wenye matunda ndio unapigwa mawe! Hutawasikia wanahangaika na Lipumba wala Mzee wa wali kuku....labda kidogo kachero.

Tunaojua kusoma lugha ya alama, hatupati shida sana.
 
Chadema ni chama cha wanaharakati. Si chama cha siasa. Wanaopaswa kupambana nao ni wanaharakati wenzao hususani wakina Musiba.
 
Pascal Mayalla,
Huo upinzani makini wa hiyo so called ability, capacity and capabilities unaweza kupatikana kweli kwa matendo haya wanayotendewa wapinzani Nchi hii? Kuminywa kuhudumu siasa zaidi ya nusu muongo, figisu za kila aina kwa wagombea wao na NEC ikipendelea waziwazi?

( usijifanye hujui walichokifanya maDED Nchi nzima ktk mchakato wa kuchukua na kurudisha fomu za ugombea na yale yanayoendelea sasa kuhusu kata kata wagombea wa upinzani bila sababu za msingi), Na zaidi hiyo TBC yenyewe kuhusu usawa wa kutangaza habari ni msamiati mgumu. Usilete kisingizio cha maudhui, mbona kwenye zile ziara tunasikia kupanuliwa na hiyo censorship haifanyiki?

Au ukiwa kada unapofuka jicho moja linabaki la kuona ya upande wako tu? Basi tufanye sawa wapinzani hawana kauli njema zenye maudhui rafiki kwa mamlaka husika, kwanini basi mnamlaumu mbowe kwa kuwafukuza TBC badala ya kumpongeza kuwa amewasaidia TBC ili wabaki na maudhui zao salama?
 
Huyu nae ni mwandishi wa habari...Yani nimekuwa nikikufatilia sn kwa muda kwa sbb nilikuwa bado kuna vitu na-kuasses...leo nimejiridhisha njaa haina baunsa na TANZANIA inaweza kuwa nchi ya Kwanza duniani yenye watu wanafiki...MAYALLA wewe ni mwandishi wa habari kweli!

Au njaa na unafiki...Hivi yote yanayowatokea wapinzani mpaka Sasa hujaona mahala pa wewe km mwandishi kuandika Jambo...ila umekereka jinsi TBC walivyokumbushwa unafiki wao...najua kuna Sheria ya maudhui ambayo pia ni hovyo (ndo mana clouds wamefungiwa lkn gazeti la uhuru halijafungiwa kwa kuripoti kitu kilekile na siku hiyohiyo.)..UNAFIKI...nimefatilia namna tbc walivyokumbushwa wakirusha matangazo ...hata mm nilikuwa natamani kuingia ndani ya tv niwachape...

Hivi kurusha kitu LIVE maana yake nn?...mbowe anaongea wao wanaendelea na uchambuzi...kisa maudhui....NGOJA TUONE KESHO,, MATANGAZO YATARUSHWA LIVE KUANZIA KUFAGIA UWANJA, KUPAKI MAGARI, KUKATA VIUNO MPAKA GIZA NA HAKUTAKUA NA INTERAPTION.. kwa mantiki hii Leo nahitimisha utafiti wangu kuwa Paskalia ni UTOPOLO
 
Huyu amebakia roho mbaya tu kuchongea chongea wenzake kama alivyomchongea Eric Kabendera,atakua na damu ya kihutu Wasukuma hawako hivyo.
 
Paskali sio kila mtu ni mjinga .muwadanganye hao hao! Actually mimi nilishablock tbc siku nyingi nyumbani na leo ilibidi nifanye trial and error ya password kwani nilishaisahau kabisa ili tu nione hicho kioja cha tbc kutangaza mkutano wa chadema.

Nilichokutana nacho ilikua aibu kabisa...TBC walienda pale kimkakati maalum kuvuruga na kupotosha uma Mbowe alikua sawa kabisa kuwatimua hao wanafiki na wachumia tumbo..anyway swali lako kuhusu upinzani wa kweli limenishangaza..wewe ndio wa kuuliza hilo swali kweli with all going on? smh halafu wewe ni mwandishi wa habari. nchi ina shida sana hii na tutaangamia
 
TBC walichokuwa wanafanya pale ni hujuma, sasa kama ukimkuta kibaka anazurula kwenye eneo lako utamkaribisha ndani au utamfukuza tena kwa kumpigia kelele za mwizi. TBC walifanya hujuma mchana kweupeeeeee.
 
Jamaa hakuna kitu wewe nashukuru hata wajumbe walikukata. Msomi na mtaalam wa maswala ya habari ila siku hizi huna chochote,
.
Kuna bandiko lako unaisifia TBC jamaa nimekudharau sana leo
 
Nyie wajinga mmekimbilia kupiga picha mapema kabla watu hawajafika kwa wingi kwenye mkutano ndio mnakuja kujidanganya nazo hapa, wacheni utoto wenu, Chadema inawakimbiza ndio maana mnawaengua wagombea wake kwa sababu za kishamba.
hiyo ni wakati mbowe anaongea ngoja nitakuletea xlip kabisa oune
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…