Je, teknolojia ya roboti wanaoongea ilikuwepo wakati wa Musa na Haruni kama Kurani?

Je, teknolojia ya roboti wanaoongea ilikuwepo wakati wa Musa na Haruni kama Kurani?

Quran. imeweka wazi unabii Upo kwenye torati sahihi na injili sahihi sio hizi zenu ambazo wakina yohana waliamua kwamakusudi wachague vya kuandika na vile wanavyoona wao aviwafai waviache hata kama alifanya yesu

1. Ni Torati ipi na Injili ipi, ambayo ndiyo haijaharibiwa?
2. Mumezihifadhi wapi matini za Torati hiyo na Injili hizo na mbona hamzitoi hadharani ili wakristu waumbuke?Zimwageniu humu tujionee,basi

3. Torati na Injli ziliharibiwa lini? Ziliharibiwa wakati Muhammad amezaliwa au angali bado kuzaliwa?
 
mkuu acha hasira
sometimes mtu anaonekana mjinga kuamini tu unachoambiwa
hivi mtu anaanzaje kukwambia kaongea na mungu pangoni akiwapeke yake na wewe unaamini!!!!!

Umegonga kwenyewe mkuu! Eti, mashahidi wa Muhammad katika kisa hicho cha pangoni ni mende,mijusi,panya, sisimizi, kenge, popo na nyenyere pekee! Na katika kitu cha kushangaza baada ya kutoka huko Pangoni, akaenda kwa mchungaji wa Kinestorian,aliyeitwa Waraqahal,mjomba wake na Khadija kwenda kupata uthibitisho iwapo kweli aliyeonana naye alikuwa ni Malaika.Kwani kasisi yule ndiye alikuwa Mungu hata Muhammad aamue kusadiki?
 
1. Sasa umeruka kimanga kuwa wewe sio Muislamu? Ikiwa wewe sio Muislamu, umejuaje kuwa Biblia sio rejea ya Kurani au kwamba viwili hivyo havina uhusiano kabisa?

2. Thread zangu, kwa namna ya pekee, ina lengo la kuifahamu historia, mintarafu iwapo Babu zetu (kizazi cha akina Musa na Haruni) nao walikuwa ki-tekenolojia wamefikia uwezo wa kuweza kutengeneza roboti la Ndama anayeweza kuongea kama tunavyoelezwa katika Kurani.
Kuhusu swala la robot kuran haijasema yule ndama alikuwa robot. Viumbe hai au visivyo hai vikiwezeshwa na Allah vinaweza kuongea. Rejea mawe yaliyokuwa yakimwambia Nabii Daudi 'Nichukue mimi nikamuue Goliath'.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuhusu swala la robot kuran haijasema yule ndama alikuwa robot. Viumbe hai au visivyo hai vikiwezeshwa na Allah vinaweza kuongea. Rejea mawe yaliyokuwa yakimwambia Nabii Daudi 'Nichukue mimi nikamuue Goliath'.

Sent using Jamii Forums mobile app

1. Hakuna anayehoji uwezo wa Mungu bali hoja ni kwamba Msamaria anayedaiwa kulitengeneza roboti hilo, alikuwapo wakati wa enzi za Musa na Haruni?

2. Je,mtume Muhammad alikuwapo wakati wa Musa na Haruni hata atajwe kwamba alishikwa unyayo na msamaria katika mchakato wa kuunda hiyo roboti ya ndama?
 
Kati ya wanajamiii small minds wewe ni mmoja wao..ukiambiwa uprove hlo utaprove au utaongea kw ushabiki

Sent using Jamii Forums mobile app

1. Baadhi ya matukio katika Kurani ndiyo proof yenyewe kwamba Muhammad alikuwa ana-desa mambo kutoka sehemu mbalimbali na kuyafanya kama yeye ndiye original source wakati sivyo.Mojawapo ni hili la sanamu ya ndama kuelezwa kwamba ilitengenezwa na msamaria wakati ukweli wa kihistoria ni kwamba sanamu ya ndama ya walioiabudu waisraeli itengenezwa na Haruni.


2. Tukio ni sanamu ya ndama na waliotengenezewa ni waisraeli.Tofauti katika kisa hicho: Mosi, ni nani alitengeneza sanamu(roboti hilo).Pili, sifa za sanamu yenyewe.Kurani inasema sanamu ilikuwa inatoa sauti,kwa maana ya kuongea.Tatu, kwamba kulikuwapo mtume aliyeshikwa unyayo na msamaria wakati wa kutengeneza sanamu hiyo. Haya mambo hayo matatu ndiyo yanabatilisha ukweli wa simulizi wa Muhammad katika Kurani, mintarafu uundwaji wa sanamu kwa ajili ya waisraeli.
 
1. Baadhi ya matukio katika Kurani ndiyo proof yenyewe kwamba Muhammad alikuwa ana-desa mambo kutoka sehemu mbalimbali na kuyafanya kama yeye ndiye original source wakati sivyo.Mojawapo ni hili la sanamu ya ndama kuelezwa kwamba ilitengenezwa na msamaria wakati ukweli wa kihistoria ni kwamba sanamu ya ndama ya walioiabudu waisraeli itengenezwa na Haruni.


2. Tukio ni sanamu ya ndama na waliotengenezewa ni waisraeli.Tofauti katika kisa hicho: Mosi, ni nani alitengeneza sanamu(roboti hilo).Pili, sifa za sanamu yenyewe.Kurani inasema sanamu ilikuwa inatoa sauti,kwa maana ya kuongea.Tatu, kwamba kulikuwapo mtume aliyeshikwa unyayo na msamaria wakati wa kutengeneza sanamu hiyo. Haya mambo hayo matatu ndiyo yanabatilisha ukweli wa simulizi wa Muhammad katika Kurani, mintarafu uundwaji wa sanamu kwa ajili ya waisraeli.
Wach nkusany data thn ntakufat ili uone namn ulivyo na akili ndogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
usije huku kama unataka kuujua uislamu,nenda MADRASA ,pia fahamu ya kwamba mungu hashindwi na jambo lolote
 
1. Ni Torati ipi na Injili ipi, ambayo ndiyo haijaharibiwa?
2. Mumezihifadhi wapi matini za Torati hiyo na Injili hizo na mbona hamzitoi hadharani ili wakristu waumbuke?Zimwageniu humu tujionee,basi

3. Torati na Injli ziliharibiwa lini? Ziliharibiwa wakati Muhammad amezaliwa au angali bado kuzaliwa?
Chochote ambacho kinakwenda nje ya misingi ya QURAN hicho ni fake na haliwezi kuwa fundisho la kufuata kwenye UISLAMU mfano
19:88-89
"; Na(makafiri) husema: Mwenyezi Mungu) mwingi wa rehema amejifanyia mtoto .bila shaka mumeleta jambo lichukizalo kabisa (kwa kusema hivyo)...

Hivyo chochote kile kinachokwenda nje ya QURAN sio ,taurat sahihi ,wala injili sahihi ata kama mtatoka mishipa kuvitetea na mengine mengi kama lile la bikira Maria mama wangu inashangaza kweli
 
1. Baadhi ya matukio katika Kurani ndiyo proof yenyewe kwamba Muhammad alikuwa ana-desa mambo kutoka sehemu mbalimbali na kuyafanya kama yeye ndiye original source wakati sivyo.Mojawapo ni hili la sanamu ya ndama kuelezwa kwamba ilitengenezwa na msamaria wakati ukweli wa kihistoria ni kwamba sanamu ya ndama ya walioiabudu waisraeli itengenezwa na Haruni.


2. Tukio ni sanamu ya ndama na waliotengenezewa ni waisraeli.Tofauti katika kisa hicho: Mosi, ni nani alitengeneza sanamu(roboti hilo).Pili, sifa za sanamu yenyewe.Kurani inasema sanamu ilikuwa inatoa sauti,kwa maana ya kuongea.Tatu, kwamba kulikuwapo mtume aliyeshikwa unyayo na msamaria wakati wa kutengeneza sanamu hiyo. Haya mambo hayo matatu ndiyo yanabatilisha ukweli wa simulizi wa Muhammad katika Kurani, mintarafu uundwaji wa sanamu kwa ajili ya waisraeli.
Hii akili au matope nani kakwambia kila SAUTI ni maongezi ? leta hilo andiko uthibitishe kweli sanamu liliongea na liliongea lugha gani?
 
1. Nakushukuru kwa kukumbuka kwamba Yesu alifundisha upendo.Je,unakumbuka kwamba kabla ya kuonyesha upendo huo kwa kuuishi,Yesu alianza kwa kufafanua maana ya upendo huo? Unakumbuka alianza kwa kufundisha kuwa Amri kumi(Decalogue) ni mahusiano chanya kati ya mwanadamu na Mungu wake kwa upande mmoja na mahusiano chanya kati ya mwanadamu na mwanadamu kwa upande mwingine?

2. Kwa staili ya uandishi wako, inaelekea wewe ni Mkristu na tena pengine u Mkatoliki.Je,umewahi kujiuliza,kwa uweza wa Kristu aliokuwa nao kama Mungu, ni kwa nini alipofika duniani hakuamua kuhubiri kwa njia ya maisha yake pekee, bali alieleza yote aliyotumwa na Baba yake kwa njia ya maneno na mawazo?

3. Je,kwa kiwango cha uelewa mkubwa ambao nimeuona katika uandi wako, umeshindwa kabisa kuelewa maudhui ya uzi huu na nyuzi zingine ambazo nimeshazipandisha humu?

Ukisoma 1 Wakorintho 13:1-13, utajifunza mengi . Uwepo wa Dini na imani zingine duniani Mungu ameruhusu ili UTUKUFU wake uonekane . Huna haja ya kupambana kwa nguvu kubwa kukosoa maandiko wanayoamini wengine wakati hakuna mkamilifu duniani hapa. Onyesha kwa matendo utukufu wa Mungu ulio ndani yako na watu wataona .Giza halimalizwi kwa giza zaidi bali kwa Mwanga.
 
Chochote ambacho kinakwenda nje ya misingi ya QURAN hicho ni fake na haliwezi kuwa fundisho la kufuata kwenye UISLAMU mfano
19:88-89
"; Na(makafiri) husema: Mwenyezi Mungu) mwingi wa rehema amejifanyia mtoto .bila shaka mumeleta jambo lichukizalo kabisa (kwa kusema hivyo)...

Hivyo chochote kile kinachokwenda nje ya QURAN sio ,taurat sahihi ,wala injili sahihi ata kama mtatoka mishipa kuvitetea na mengine mengi kama lile la bikira Maria mama wangu inashangaza kweli

1. Ninakuomba jambo moja tu (na mimi mwenyewe nitakuombea) kwamba uwe na uhai tele.Kuna wanazuoni wa kiislamu mahiri sana ambao sasa wanakiri kwamba Muhammad alipotoshwa na matini za kiyahudi na za baadhi ya wakristu wa mwanzo(mfano wa akina Waraqahal) kudai kwamba Biblia(Torati na Injili) zimeharibiwa.Nitaleta uzi siku pamoja na rejea kamambe na nadhani utashangaa sana.

2. Kuna mambo yatakuja siku zijazo katika uislamu ambayo yatakushangaza sana.Na dalili zimeshaanza tayari.Nakusihi ujivue koti la kung'ang'ania uelewa ambao Muhammad alipotoshwa tu na sasa uupatie jicho jingine ukweli wa mambo.
 
Mungu anasema yeye ni nafsi tatu,wewe unasema Mungu siyo nafsi tatu.Ina maana wewe na Muhammad ndiyo munamfahamu Mungu sana kuliko Mungu anavyojifahamu?

Tunasoma hivi:

“13 Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe.14 Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?15 Yesu akajibu akamwambia, Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akamkubali.16 Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake; 17 na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.” (Mat.3:13-17).


“16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;17 ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.” (Yoh 14:16-17).

“18Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.” (Mat. 28:18-20).

Kwa nukuu hizo,Muhammad na ninyi wote, msiosadiki juu ya nafsi tatu za Mungu,ina maana nyinyi ndio mlimuumba Mungu na hivi munamfahamu vilivyo kuliko yeye anavyojifahamu?
Hizi si ngano tu kaandima Matayo? Ni maneno yake Mungu mwenyewe haya?
Hii ni story tu kaandika Matayo.

Sent using my NOKIA torch
 
Wanabodi:

Baadhi ya Wanazuoni wa Kiislamu hawataki kukubali kwamba Kurani ina maelezo au masimulizi ya visa ambavyo ama havikuwahi kutokea katika historia ya maisha ya mwanadamu au kwamba visa hivyo haviko kama vinavyoelezwa na Kurani yenyewe.

Leo,ninacho kisa kingine kinachomuhusu Musa na Kaka yake, Haruni, wakiwa na wanaisrael.Kisa hicho, tunakikuta katika Biblia,Agano la Kale,Kutoka Kitabu cha Kutoka 32:1-10:

“1Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Haruni, wakamwambia, Haya! Katufanyizie miungu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata.2 Haruni akawaambia, Zivunjeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee.3 Watu wote wakazivunja pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, wakamletea Haruni.4 Akaipokea mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha; nao wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.5 Naye Haruni alipoona jambo hili, akajenga madhabahu mbele yake; Haruni akatangaza akasema, Kesho itakuwa sikukuu kwa Bwana.6 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakatoa dhabihu, wakaleta sadaka za amani, watu wakaketi kula na kunywa, wakaondoka wacheze.7 Bwana akamwambia Musa, Haya! Shuka; kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao,8 wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru, wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu, wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.9 Tena Bwana akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu10 basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.”

Kurani na yenyewe katika Sura Ta Ha 20: 85-96,inasimulizi lile lile, ila ambalo inaonekana limefanyiwa editing kidogo.Tofauti na inavyoelezwa katika Biblia,katika Kurani Muhammad, anasema aliyewatengenezea Waisrael sanamu ya Ndama huyo ni Msamaria mmoja,ambaye hamtaji jina.Kitu kingine ambacho Muhammad anakisema kuhusiana na kisa hicho, ni kwamba sanamu hiyo ya Ndama ilikuwa na uwezo wa kuongea!Jambo la tatu, ni kwamba eti Mungu ndiye aliyewatega waisrael kuona kama ni wavumilivu,hasa baada ya Musa kuwa amewaacha Waisraeli na kaka yake Haruni,kwa muda mrefu bila kurudi.

SASA, Wasamaria ni akina nani?

Wasamaria wanatajwa kuwepo baada ya utawala wa Israeli kwa upande wa Kaskazini katika Palestina kuangukia mikononi mwa dola ya Assyria mnamo mwaka 722KK na hiyo ni kama karne saba baada ya Musa kuondoka duniani.

Wasamaria ilikuwa ni jamii ya watu waliokuwa wakiishi katika Dola ya Kaskazini mwa Israeli(Northern Kingdom of Israel).Samaria ni jina la mji uliokuwa makao makuu ya Dola hiyo (Ufalme huo) na hivi watu walioshi katika dola hiyo ya Samaria waliitwa Wasamaria.Mji wa Samaria, ulikuwa katikati ya mji wa Galilaya (kwa upande wa kaskazini) na mji wa Yudea(kwa upande wa Kusini).Wasamaria kwa rangi walikuwa mchanganyiko wa Wayahudi na uzao wa wapagani(racially mixed society with Jewish and pagan ancestry).

Kiimani pamoja na kwamba,wasamaria walikuwa wakimuabudu YAHWEH(Mungu, kama Wayahudi walivyokuwa wakimuita), sawa na wayahudi walivyofanya,dini yao haikuwa dini kuu ya Kiyahudi(mainstream Judaism).Wasamaria walikuwa wakivikubali vitabu vitano tu kati ya orodha ya vitabu viliyokuwa vikikubaliwa, na Hekalu lao lilikuwapo katika Mlima Gerazimu(Gerazim) badala ya lile Hekalu la Kiyahudi lililokuwa katika Mlima Sioni,kule Yerusalemu kama tusomavyo katika Injili ya Yohana 4:9,20-21:

“9Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia. 21Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.”

Wasamaria wa nyakati za Yesu walikuwa wakiamini kwa dhati juu ya Mungu mmoja kuliko hata Wayahudi wenyewe na namna fulani walikuwa wameshika sana sheria za Musa kuliko hata Wayahudi,kwa namna ya pekee,suala la Sheria za Sabato.Tofauti ya Wayahudi na Wasamaria ilikuwa ni kwamba wayahudi hawakuruhusiwa kutamka jina takatifu la Mungu “YAHWEH” katika viapo, isipokuwa aliyeruhusiwa kufanya hivyo alikuwa Kuhani Mkuu tu,tena akiwa huko patakatifu pa patakatifu,tena mara moja kwa mwaka na hiyo ilikuwa katika siku ile ya toba ya taifa (ndiyo,Yom Kippur). Wasamaria wao kutamka jina takatifu “YHWH” (soma “YAHWEH” ) kwa sauti au kimya kimya halikuwa tatizo hata kidogo.`

Kwa hiyo, Wayahudi wote wa kawaida hawakuwa na ruhusa na hata leo bado hawaruhusiwi kusoma, si kwa sauti tu wala kimya kimya,herufi za jina takatifu la Mungu, YHWH, kwa sababu ya utakatifu wa jina la Mungu wao. Kwa nini? Kwa sababu kuzisoma bure bure kungelingana na utovu wa heshima kwa Mungu mkuu na kuivunja amri ya Mungu ya kutolitaja bure jina lake, DECALOGUE. Ndiposa, ilikuwa marufuku na bado ni marufuku kabisa Myahudi wa kawaida kuzisoma na kuzitamka herufi hizo.

Kwa hiyo,kutokana na wasamaria kuonekana hawashiki sawa sawa dini ya Kiyahudi na kwamba walikuwa na vinasaba vya damu ya kipagani,basi walikuwa wakidhauriwa na kutengwa na wayahudi wa Kawaida.Na ndiyo maana utashangaa kwa nini wayahudi walipokuwa wakisafiri kutoka Yudea kwenda Galilaya au Galilaya kwenda Yudea,walilazimika kuvuka mto Jodani kisha kuambaaambaa ng’ambo ya Jodani na kisha kuvuka tena mto Jodani walipokaribia kufika Galilaya au Judea ili kukwepa kupitia ardhi ya Samaria kwa kukwepa wasije wakanajisika. Kwa hali hiyo,wayahudi hawakuchangamana na wasamaria na walijengeana chuki au uhasama dhidi ya Wayahudi wa kawaida. Ni kutokana wasamaria na ni kwa mazingira haya,ndiyo kisa hata Yesu alinyimwa sehemu ya kulala katika Kijiji kimoja walipokuwa wakiishi Wasamaria, kwa sababu tu ya Uyahudi wake na wala si kwa sababu hakuwa na uwezo wa kulipia sehemu hiyo.Soma Luka 9:51-56:

“51 Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa.Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine.”


Maswali ya Kujiuliza:

  • Je,Muhammad anaposema kuwa Msamaria alimshika Unyayo,anataka kuieleza na kuiaminisha jamii ya Kiislamu kwamba wakati sanamu ya ndama huyo inatengenezwa yeye alikwisha kuzaliwa, hata iwezekane kwa huyo msamaria kumshika unyayo kabla ya kumuunda ndama huyo?

  • Kwa namna inavyosimuliwa katika aya hiyo nukuliwa ya Kurani,mbona inatoa tafsiri kuwa yeye Muhammad alikuwa sehemu ya mchakato wa kuwezesha kuundwa kwa sanamu hiyo baada ya kuwa ameguswa unyayo wake? Na kama ndivyo,je,Muhammad haoni kama na yeye alikuwa ni sehemu ya kumkufuru Mungu sawa na yule msamaria?

  • Je,ikiwa Muhammad ni mtume wa mwenyezimungu (na msamaria aliwaundia waisrael sanamu iliyochukua nafasi ya Mungu, jambo ambalo ni kufuru),iliwezekanaje kwa Muhammad kukubali kushikwa unyayo na msamaria ambaye alikuwa na nia ovu ya kuwapotosha waisrael kwa kuwaundia kikaragosi cha Mungu?

  • Je, simulizi la Kisa hiki nalo limetumia lugha ya picha kama ilivyo katika kisa cha ndege na mchwa kutumika kama wanamgambo, kama tulivyoelezwa na wanazuoni wa Kiislamu katika mjadala uliopita, wa Ndege kutumika kama maaskari katika vita?

  • Je,kwa kuchukulia kweli kwamba msamaria ndiye aliyeunda roboti ya ndama iliyokuwa inaongea,msamaria huyo alikuwa na nguvu za kutenda miujiza? Na kama msamaria hakuwa na uwezo huo wa kimiujiza,je, alitumia tekinolojia gani wakati huo kuweza kuunda sanamu iliyokuwa inaoongea?

  • Historia inaonyesha Muhammad alizaliwa mwaka 570BK na kufariki dunia mwaka mnamo tarehe 8 Juni 632BK. Na Musa na Haruni(pamoja na huyo msamaria aliyetengeneza roboti la Ndama), waliishi miaka mingi sana kabla ya Yesu. Je,iliwezekanaje kwa huyo msamaria kuweza kumshika mtume unyayo katika mchakato wa kuliunda lile roboti wakati Mtume(Muhammad) hakuwa amezaliwa bado?

  • Je,kwa kadri ya historia ya uhasama kati ya Waisraeli na Wasamaria,na iwapo tukizingatia maelezo ya Muhammad, iliwezekanaje kwa Waisraeli kuweza kuchangamana na huyo msamaria, hata waweze kukubali kutengenezewa sanamu(roboti) na adui yao?

  • Kwa kuwa Kurani ni maneno ya Mungu yaliyoshushwa moja kwa moja kwa Muhammad(bila editing yoyote) toka kwa Mungu,je, kwa kisa hiki ambacho imeonekana ni uongo wa kihistoria,ni nani muongo?Ni Mungu anayedaiwa kumpelekea Muhammad Kurani au ni Muhammad tu ndiye alijisingizia kuwa Kurani ni maneno ya moja kwa moja,ambayo hayahaririwa,toka kwa Mungu?
Kwa maswali haya pamoja na mengineyo munayoweza kuongezea,nawakaribisheni,sasa kwa mjadala.
Ndugu yangu umejitahidi kujenga hoja lkni zote hazna mashiko kwnza ukizsoma aaya za sura hiyo 20:80-96 apo amezungumzia mtu anaeitwa samiri ten c pekeyke bali wamezungumziwa watu watatu samiri farao pmj na haman kwhyo unaposema samiri moja kw moj ni mtu anaetokea ktk kabila la msamaria unakosea ten huu n uwongo wa kiwango cha dgree mana hakuna aya yyt ktk kuran au hadithi iliyosema samiri n mtu wa kabla la msamaria ndani ya vitabu vya kislamu..ila nlchogundua huujui uislamu ila uliyasoma maandiko juu juu ili tu ujenge hoja zako mbovu.historia y watu wa kale wanasema mtu ambye aliwadanganya waezraili kwmba samiri n mtu wa kabila mmasari n padri anaejulikana km padri dale,sasa uislamu na padri wapi na wapi?mm nkushauri ili nkusaidie kujibu maswali yko uchwara njoo na ushahidi wa aya iliyomo ndani ya qurani inayoeleza samiri mtu tajwa ktk hzo aya ni msamaria man umeuliza maswali kwa waislamu kwhiyo tuongee ushahid utakaouona ndani y qurani..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu acha hasira
sometimes mtu anaonekana mjinga kuamini tu unachoambiwa
hivi mtu anaanzaje kukwambia kaongea na mungu pangoni akiwapeke yake na wewe unaamini!!!!!
Muhammad hakuongea na Mungu pangoni. Period. Una swali lingine?

Sent using my NOKIA torch
 
Ukisoma 1 Wakorintho 13:1-13, utajifunza mengi . Uwepo wa Dini na imani zingine duniani Mungu ameruhusu ili UTUKUFU wake uonekane . Huna haja ya kupambana kwa nguvu kubwa kukosoa maandiko wanayoamini wengine wakati hakuna mkamilifu duniani hapa. Onyesha kwa matendo utukufu wa Mungu ulio ndani yako na watu wataona .Giza halimalizwi kwa giza zaidi bali kwa Mwanga.

1.Nguvu kubwa ni ipi? Umeniona kwamba natembea na maspika mitaani kueleza haya ninayoyaeleza?

2. Mungu kuruhusu variations za dini ni suala ambalo halina uthibitisho wowote.Mungu anatuumba na utashi wa kuchagua jema au baya.Kwa hiyo, suala la kusema kwamba Mungu ndiye ameruhusu hata dini zinazompinga yeye katika nafsi zake ni kutaka kuonyesha kwamba Mungu ndiye anayeruhusu watu kufanya dhambi.

3. Hebu karibu tujadiliane zaidi.Mimi sio wa kwanza kuandika, kuchambua Imani ya Uislamu.Kama wewe ni mkatoliki,utafahamu kwamba tayari mtaguso wa II wa Vatican unaruhusu wakatoliki kuusoma Uislamu ili kuufahamu na waislamu wanaalikwa kuusoma Ukristu.Ni kwa kufanya hivyo ndipo majadiliano ya Kiekumene yatakapokuwa na maana zaidi.Nadhani pia huelewi mazungumzo hayo yana maana gani mbele ya safari. Rejea Mkutano wa Wakatoliki na Waislamu uliofanyika Libya mwaka 1976.
 
Muhammad hakuongea na Mungu pangoni. Period. Una swali lingine?

Sent using my NOKIA torch
even if you say it sarcastically
the fact is whoever believes in that laughable story/stories is a damn fool (and this includes bible stories)
 
Back
Top Bottom