Mkuu,Sijakuelewa kabisa.Mbona umeingia katika Fallacy of Irrelevance? Ndio kusema umeacha hoja ya msingi na wewe umejenga hoja nyingine mpya.Sawa,Biblia siyo reference ya Kurani, lakini mbona munasema Biblia ilitabiri kuja kwa Mtume Muhammad katika Kitabu cha Kumbukumbu la Torati 18:18-19:
"“18 Nitawateulia miongoni mwa ndugu zao wenyewe nabii kama wewe; nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.19 Yeyote ambaye hatasikia maneno atakayosema nabii huyo kwa jina langu, mimi mwenyewe nitamwadhibu.”
Na tena mwasema Yesu Kristu aliposema katika Agano Jipya kuwa "nitawaleteeni msaidizi baada yangu..." eti alikuwa akimtabiria Muhammad?
Je,kama Biblia haina mafungamano na Kurani, ni kwa nini mnaitumia katika kumthibitishia Muhammad utme wake?