Je, tofali 2800 zinatosha kujengea nyumba ya vyumba 3 na kila kitu ndani?

Je, tofali 2800 zinatosha kujengea nyumba ya vyumba 3 na kila kitu ndani?

Nilikuwa kwenye mkwamo kama mwuliza swali, nyumba yangu nimetumia tofari 1000 msingi pekee lakini jilivyojifunza ni kuwa kama eneo tambarare utatumia tofari kidogo tofauti na na eneo ambalo haliko sawa. Hivyo ni ngumu mtu kusema zinatosha au hazitoshi bila kusema eneo utalojenga likoje
 
Ni sawa mkuu, lakini swala la wewe kudownload movie au nyimbo ni kweli na ukidownload kisha usiipende haitokigharimu chochote kuifuta na kujaribu kudownload nyingine, lakini ukijenga nyumba kwa ramani isiyokidhi ubora au mahitaji ya site yako jiulize ni gharama kiasi gani utahitaji kutatua tatizo, ni kama mtu anaelima kwa mara ya kwanza anawekeza 2M+ kisha anaona tabu kutoa pesa kidogo kwaajili ya consultation kwa mkulima mzoefu, au mtu anaeingia mkataba wa mamilion kisha anaona tabu kutoa pesa kwa mwanasheria kumsaidia na kumshauri, kuna watu wengi wanatapeliwa viwanja kisa tu aliona tabu kuiweka hiyo kisheria au hata kuwalipa kidogo serikali ya mtaa kwenye mauziano, matokeo yake unapoteza million 5+ kisa eti uliona gharama kutoa laki moja. Haya mambo yapo na watu wataendelea kuumia na wabongo wepesi wa kusahau na tunapenda sana shortcut.
Unajenga nyumba ya 30+ unaona tabu kulipia ramani Tsh laki tatu, ufanye kitu cha uhakika zaidi na ushauri wa mambo ya msingi ya kuzingatia ikiwemo na namna ya kupunguza gharama za ujenzi wako

Mimi ramani imenigharimu 2M nashangaa watu hapa wanazunvumza mambo ya elf10 !? Akili za hovyo kabisa
 
Profession inayoringa kipindi hiki cha uchumi wa katikati siioni labda wale wanaolazimisha rushwa barabarani ya kubrashi viatu wengine wote kapuuuut chaliiiii njaa mbaya huyo wa kukupa 150,000 kwa ramani ya nyumba hayupo
 
Profession inayoringa kipindi hiki cha uchumi wa katikati siioni labda wale wanaolazimisha rushwa barabarani ya kubrashi viatu wengine wote kapuuuut chaliiiii njaa mbaya huyo wa kukupa 150,000 kwa ramani ya nyumba hayupo
Kila mtu analipwa kutokana na thamani aliyojijengea. Na kila mtu analipa kutokana na thamani anayohisi au anategemea kuipata. Bei standard ya ramani kwa nyumba ya kawaida ni laki tatu na kwa nyumba ya ghorofa ni million moja. Hata hiyo laki na nusu ni ndogo na watu wanafanya kazi na zinalipiwa. Binafsi nisisitize kuwa kukwepa gharama sio tatizo ila muhimu ni ujue unachokifanya
 
hizo tofali mimi nimejengea nyumba kubwa sana hapo Mbezi, ina masta moja, chumba cha binti yangu, sebule kubwa, dining, jiko, choo cha ndani chenye korido ndogo ya kufulia pamoja na veranda mbili (kwa mbele na nyuma).

ukiwa na uwezo wa kupata hayo matofali hebu anza ujenzi, usijiulize sana kama yatapelea ni mbele kwa mbele, wewe anza nayo hayo hayo
 
Unaenda mbali sana, ramani siku hizi tunapata kwa 10K.
Kadri siku zinavyoenda ndio umuhimu wa ramani zenu unapungua, watu waliosoma Civil Eng nao wanachora ramani siku hizi, architects nao wanachora unakuta mpaka masela wangu wa electrical nao wamo. Yaani ilimradi vurugu tu.

Auto CAD na zinginezo zimekuwa kimeo, kuna jamaa yangu kasoma account naye saiv anachora ramani tena za hali ya juu.

Sikukatishi tamaa ila hiyo bei umeweka kwa matarajio makubwa sana[emoji23][emoji23][emoji23]
🤣 🤣 🤣 🤣
 
mi i
Unaenda mbali sana, ramani siku hizi tunapata kwa 10K.
Kadri siku zinavyoenda ndio umuhimu wa ramani zenu unapungua, watu waliosoma Civil Eng nao wanachora ramani siku hizi, architects nao wanachora unakuta mpaka masela wangu wa electrical nao wamo. Yaani ilimradi vurugu tu.

Auto CAD na zinginezo zimekuwa kimeo, kuna jamaa yangu kasoma account naye saiv anachora ramani tena za hali ya juu.

Sikukatishi tamaa ila hiyo bei umeweka kwa matarajio makubwa sana[emoji23][emoji23][emoji23]
mimi sijasoma civil wala mama ake auto cad drawing lakini ninatools nakuchorea ramani chap
 
hajui kutafuta bado, hajui waliokuwa juu walitafuta kuanzia chini, Hata General alianza kwa kuwa Private.
 
Nawezaje kujifunza kuchora ramani ? Nidowload programme gani zinisaidie natamn sanaa niweze kujifunza hili
 
Back
Top Bottom