Uchaguzi 2020 Je, Tundu Lissu anaendelea na kampeni?

DaudiAiko

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2012
Posts
372
Reaction score
310
Wana Jamvi,

Kipindi ndio hiki, wakati ndio huu. Kama umelewa mchuzi wa Magufuli basi bado huja dondoka ila kama umelewa mchuzi wa Tundu Lissu basi amini usiamini ameanza kupigwa changa la macho na sasa hivi umeanza kusinzia porini. Ila kama wewe ni kama bendera na unafuata upepo basi bendera yako lazima ina peperushwa sana kwa uvumi na tetemeko la Tundu Lissu.

Wote tunafahamu kwamba tume ya uchaguzi ili chukua maamuzi ya kumzuia mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu kushiriki kwenye kampeni kwa muda wa siku saba lakini maamuzi haya tekelezwi ipasavyo na ndio maana tumekuwa na kama gumzo fulani mitaani. Lazima tukubaliane kuwa mikutano ya kampeni na mikusanyiko mikubwa yenye mihemko ya siasa ni vitu viwili visivyo kuwa na tofauti kubwa. Tundu Lissu anaweza akasema kwamba alikuwa sokoni na watu waka mfuata wenyewe lakini ukweli wa mambo ni kwamba yeye mwenyewe ndiye aliye hamasisha mkusanyiko huo wa watu. Jumanne wiki hii, Tundu Lissu ali zuiwa na polisi alipokuwa anaelekea kwenye mkutano wa chama.

Mambo kama haya ambayo lazima yakemewe vikali ni mfano wa mtiririko wa makosa ambayo yanaweza kumfanya akatwe kwenye orodha ya wagombea wa urais mwaka huu au mbaya zaidi kusababisha fujo na ukosefu wa amani kwenye kampeni au uchaguzi. Adhabu aliyopewa Tundu Lissu ni kama onyo kwasababu tume ya uchaguzi ingeweza kuchukua hatua kali zaidi.

Tujaribu kuchambua kwa kina zaidi hali ya uchaguzi sasa hivi na kampeni zinazo endelea. Je, unaamini kwamba Tundu Lissu atashinda uchaguzi?, Je, Tundu Lissu anaamini kwamba atashinda uchaguzi? Je, Tundu Lissu anahisi kwamba amewa shawishi Watanzania kwa kiasi kikubwa kwa njia zilizo halali?

Je, Tundu Lissu ana udhibitisho kwamba njia anayo itumia sasa hivi ni sahihi haswa katika kipindi ambacho ana tumikia adhabu ya tume ya uchaguzi. Ikitokea kwa njia moja au nyingine kwamba Tundu Lissu ana amini ana uwezo wa kushinda uchaguzi kwa njia halali na ana ongoza kwenye kampeni hizi, basi hana haja sana kutu pepesua kwenye wimbi hili la bahari. Lazima tuweze ku tofautisha "Policies" na nia nzuri kwa watanzania wote, "Political stunts" na "Con artistry" zinazo tumika kuwa potosha watu.

Mwisho wa siku maisha ya watanzania wote ni muhimu zaidi kuliko matakwa ya mtu mmoja.

Tafakari,
Jummah Kareem.

Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.
 
Hii nchi ina wapumbavu wengi sana.

Umeandika Utopolo mtupu.

Hujui Lissu ni Binadamu anahaki ya kutembea.

Je, angewanadi wagombea udiwani na ubunge kwa kofia ya makamu mwenyekiti?

Kachukue buku saba Lumumba
 
Tatizo hamtaki kukubali Tundu Lissu ana IQ kubwa sana kuliko nyinyi. Hivyo mnapo panga figusu zenu za kizamani za kutaka tu kumkomoa, mnatakiwa pia mjipange kisheria na mumtangulie mbele zaidi! Jambo ambalo hamliwezi.

Hivyo mumuache tu aendelee kuwanyoosha na kuwadhalilisha nyinyi mnaoitwa Wanasheria Wabobezi wa Serikali, Tume na wale polisi wa ccm. Wakati mwingine akili zenu zitawakaa tu sawa.

Lissu ni kiumbe wa dunia ya peke yake. Hivyo muacheni tu afanye vile anavyo ona inafaa. Amewazidi kika kitu.
 
Mshana Witch project
 
Kweli Lissu amewashika pabaya dadeki πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Kuna jambo kubwa linapangwa sirini dhidi ya wapinzani wenye nguvu hasa Tundu A. Lissu. CCM, Tanpol, tume, tiss, serikali, wakurugenzi, msajili wa vyama kwa uchache wanahusika kwenye usiri huo
 
Wahi kwa Mkapa ukasikilize ujenzi wa flyover. Bila kusahau wasanii 200 watatoa burudani live
 
Hahahahaha et nawee umeandika kwa mbaaaaali utadhan hauna akili. Mtu akikusogelea karibu nikweli hauna akili.


Umetumia muda mwingi kuandika utumbo
 
Watumishi wote na familia zao kura kwa lissu.Mmeteswa sana miaka 5 bila ongezeko la mshahara,kupanda madaraja,increments,malimbikizo n.k.

Mpigie lissu kura ubarikiwe pia.
 


Alishapuuzwa huyu
 
Nimesoma mara nne cjaelewa bandiko lako. Jifunze kuandika mkuu
 
Tukuulize na wewe, unaamini kabisa kuwa CCM wataiba kura
 
Ata aibu huna mwanaume mzima unamsifia mwanaume mwenzio eti duniani hakuna kama yeye ...maajabu
😁😁😁 greenwoods mwanaume kumsifia mwanaume mwenzie kuwa hakuna kama yeye ndio mambo ya faragha hayoπŸ˜³πŸ˜³πŸ˜³πŸ™Œ
 
Hii nchi ina wapumbavu wengi sana.

Umeandika Utopolo mtupu.

Hujui Lissu ni Binadamu anahaki ya kutembea.

Je, angewanadi wagombea udiwani na ubunge kwa kofia ya makamu mwenyekiti?

Kachukue buku saba Lumumba
Ninakubaliana na wewe unaposema kwamba matikiti yamejaa Kariakoo lakini miguu ya mtu mmoja inaweza kusababisha maafa makubwa. Chukua spana, fungua boneti!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…