Je ukiwa mpagani, siku ukifa hauzikwi?

Je ukiwa mpagani, siku ukifa hauzikwi?

Kuna wale ambao hawaendi kanisani wala msikitini na hawana vyama au vikundi wapo wapo tu. Hawa wakifa huzikwa kimya kimya bila ibada. Inaweza ikatokea mchungaji fulani from no where akauteka msiba na kuendesha ibada ya mazishi as if marehemu alikuwa mshirika wake, lengo likiwa ni kuwahubiria habari za injili / wokovu walio hai
 
Mtu atazikwa kwa heshima kulingana na status yake aliyo nayo katika jamii alimoishi nayo. Uliacha kwenda kanisani mchongo utafanywa ili tu uzikwe kikristo kwa heshima yako. Kama ni kapuku hujulikani ulikuwa unajumuika na kikundi gani basi utazikwa hivyo hivyo kama desturi ya kuzika mfu ilivyo, mradi tu ufukiwe
 
Kuna viongozi wa dini hufanya ibada ya mazishi nusu au hukataa kabisa kufanya ibada hiyo na kuzua sokomoko na kasheshe msibani. Hudai marehemu alikuwa si mhudhuriaji kanisani wala jumuiya alikuwa haendi, michango yake haijulikani alikuwa anatoa wapi. Nusura kiongozi mmoja wa dini apigwe kwa kukataa kwenda kumalizia ibada makaburini. Aliokolewa ghafla kwa kutoroshwa eneo la msiba kulikokuwa na waombolezaji wenye hasira wakihoji kwa nini akatae kumalizia ibada ya mazishi kwa madai hayo? Waombolezaji wakauchukua mwili kuelekea makaburini huku wakiimba parapanda italia, wakauzika na kuweka mashada bila mahubiri ya kidini
 
Habari?
Ni wazi mazishi mengi hapa tz yanaitimishwa chini ya dini mbalimbali hata km mhusika alikuwa sio mshirika mzuri basi inaundwa michongoko ili kumlinda na atimaye azikwe kwa iman fulani
Je yule asie na imani ya kidini hata kidogo akifa ni nan husimamia ilo,
Binafsi sijawahi kuona mazishi ya raia wa kawaida yakiendeshwa na serikali hata ya mtaa
Kwani kinachozikwa ni imani au nyamafu?
 
Waislam nao ni walewale wa kukataa kuzika mwenzao kikamilifu. Jamaa mmoja alikufa maji, kwenye msiba sheikh mmoja akasema watamfanyia mambo ya msiba nusu, mengine ndugu zake watajua huko watafanyaje. Sheikh alidai marehemu alikuwa haendi msikitini wala hahudhurii kwenye vikao vya waumini wao. Akasema watamzika kwa taratibu za kidini ila mengine huko nyumbani kwake hawatamfanyia
 
Mi bwana nachukia sana unafki wa binadamu.ukiwa hai hakuheahimu,dharau matusi,mara kakuzushia hili mara akufanyie fujo.
Siku ukifa wanahangaika oh azikwe Kwa heshima,heshima za mwisho,mara tumuombee heri.
Umekufa umelala ndani huna hata chakula na dawa ila masaa machache ukifa watu watakula na kusaza.
Ndio dunia
 
kuna mtu alijifia kichakani, shughuli pevu ikawa ni kutafuta ndugu zake, suluhisho ikawa ni jina lake liliakisi dini gani? Wakaona ni uislam. Fasta akazikwa kwa dini ya kiisl
je bila dini mtu hawez zikwa, kwanini dini?
Yote NI Yale Yale, hizi DINI zimeshawaharibu akili
Ndo hapo najiuliza maana kuzaliwa haiulizwi dini ila kuzikwa had dini
 
Juzi kati kuna jamaa alikufa kwa ajali ya bodaboda. Tukajiuliza atazikwa kwa taratibu gani? Huko nyuma alikuwa mkristo ila aliacha kwenda kanisani kitambo sana. Kwa kuwa aliwahi kuwa mkristo msiba wake kulipigwa nyimbo za maombolezo za kikristo sambamba na nyimbo za chama fulani. Wachungaji hawakujitokeza badala yake viongozi wa chama ndio waliochukua nafasi za wachungaji wakamzika kichama huku wakiwa wamevaa sare za chama na sanduku likifunikwa kwa bendera ya chama.
ila alizikwa
 
Habari?
Ni wazi mazishi mengi hapa tz yanaitimishwa chini ya dini mbalimbali hata km mhusika alikuwa sio mshirika mzuri basi inaundwa michongoko ili kumlinda na atimaye azikwe kwa iman fulani
Je yule asie na imani ya kidini hata kidogo akifa ni nan husimamia ilo,
Binafsi sijawahi kuona mazishi ya raia wa kawaida yakiendeshwa na serikali hata ya mtaa
Labda uje na kaburi lako, Tanzania yametengwa makaburi ya waisilamu na ya wakiristu, sasa wewe mpagani uzikwe wapi?
 
Habari?
Ni wazi mazishi mengi hapa tz yanaitimishwa chini ya dini mbalimbali hata km mhusika alikuwa sio mshirika mzuri basi inaundwa michongoko ili kumlinda na atimaye azikwe kwa iman fulani
Je yule asie na imani ya kidini hata kidogo akifa ni nan husimamia ilo,
Binafsi sijawahi kuona mazishi ya raia wa kawaida yakiendeshwa na serikali hata ya mtaa
Mi nikifa wanitupe ziwa Tanganyika niwe chakula cha samaki
 
Kuna viongozi wa dini hufanya ibada ya mazishi nusu au hukataa kabisa kufanya ibada hiyo na kuzua sokomoko na kasheshe msibani. Hudai marehemu alikuwa si mhudhuriaji kanisani wala jumuiya alikuwa haendi, michango yake haijulikani alikuwa anatoa wapi. Nusura kiongozi mmoja wa dini apigwe kwa kukataa kwenda kumalizia ibada makaburini. Aliokolewa ghafla kwa kutoroshwa eneo la msiba kulikokuwa na waombolezaji wenye hasira wakihoji kwa nini akatae kumalizia ibada ya mazishi kwa madai hayo? Waombolezaji wakauchukua mwili kuelekea makaburini huku wakiimba parapanda italia, wakauzika na kuweka mashada bila mahubiri ya kidini
Aisee
 
Back
Top Bottom