Je, ulitumia mbinu gani kuingia kinyemela shuleni na kitu kisichotakiwa?

Je, ulitumia mbinu gani kuingia kinyemela shuleni na kitu kisichotakiwa?

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Kuna dogo anasoma shule zenu za kishua ila zenye mitambo ya kukagua na ina walimu wanoko ila kaingia (kazama) getini na bangi na simu bila kugunduliwa na najua muda huu wa saa 4 kuelekea saa 5 ndiyo huwa mida yake ya kuvuta na kutupigia simu sisi washkaji na kaka zake wa mtaani tupige story mbili tatu.

Vijana wa siku hizi ni wajanja na wana akili na mbinu kali sijapata kuona hakyanani.

Nilikuwa sijui kazi ya foili zile tunazofungiwa kiepe (chips) ambazo wanafunzi wengi wa shule za boarding (bweni) hupenda kununua chips, kuku na mayai na kulazimisha kwenda (kurudi) nazo shuleni kwao pale ama wakitoka likizo au wakiwa wameomba ruhusa ya muda ya kurejea makwao.

Nimeamini mwanafunzi hachungiki.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hata sijui niliwezaje.
 
Bange mbichi hii imeandika huu ujuha...
 
Shule yetu ilikua na mfereji wa kuingiza maji huo tuliutumia kuvusha kila aina ya magendo kuanzia chapati,kitimoto,simu ,bange na vinginevyo visivyotakiwa
 
Shule yetu Kwanza hata geti na uzio haikuwa nao. Full freedom wewe tuu....akili kumkichwaa.
 
Back
Top Bottom