Je, uliwahi kuwa maarufu shuleni?

Je, uliwahi kuwa maarufu shuleni?

Sana kabisa.
Primary sababu nilikua kichwa halafu nilikua napenda kusoma magazeti ya udaku balaa.

Olevel: Nilikua napenda michezo halafu nikawa nawashikia namba moja kuanzia form one mpaka form four. Hapo tulikua tunachukuliwa idadi ya wanafunzi wote kama 200+ tunapangwa namba moja mpaka wa mwisho. Walikua wanashangaa ninavyoonekana na ninavyowaongezea.

Advance: Nilikua social Prefect kwahiyo shule nzima lazima wanijue. Pia nilikua sistaduu wa darasani kwetu. Nilikua PCM ila nalala HGL na marafiki zangu walikua watu wa arts.
Wengi walijua form six nitazungusha maana ninachosoma na mimi hatufanani halafu sikuaga msongo

Chuo: Sikua maarufu kiviile sema kampani yangu tulikua maarufu maana ndio lilikua kundi la wala bata konki kabisa. Class nako walikua wananijua sababu wa mwisho kuingia wa kwanza kutoka na kwenye pepa nakaaga mbele kabisa au nyuma kabisa na nakuaga wa kwanza kumaliza pepa so wengi wakawa wanajua mimi sistaduu kilaza ila wakirudi September conference sipo.

Actually shape yangu (basi kuna wapumbavu watasema najisifia sijui najishaua) na akili yangu havifanani ndio maana nakuaga maarufu ninaposomaga sababu naonekana tofauti na vitu ninavyosomea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Primarily
Nlkuwa doja nalala vichakan sitakaa nisahau siku hiyo nililalia kinyesi cha binadamu nlikuwa nalala ukifika mda wa kutoka naenda home, nlkuwa kama sio kujificha vichakan nashinda kwenye majumba mabovu sitakaa nisau wazazi walikuwa wanajua naenda shule kumbe nimetega almost mwezi mzima siku walijua baada ya barua kufika home hilo lilinipa umaarufu still nlifaulu shule nzur ya mkoa

O-level
Tabia haina dawa form 1 nilianza vizur na form lakin sjawah kuwa kipanga nlvyofika form 3 nkaanza kutega nashinda vichakan pembezon mwa mji nachoma viazi nkajulikana kwa jina la mkimbizi nlkuwa nikionekana siku ya matukio tu kama mitihan nilianguka vibaya mmno kimasomo ikabidi nibadilike kwa huo mwaka 1 uliobakia baada ya bi maza kugundua f4 nikafaul kwa daraja zuri still hakuamini yale maajabu"mabadiliko daima huanza na wewe kama unapokwenda siko uliza usichelewe " still walimu hawaamin Yule mtukutu alieshindikana alifanya mabadiliko kwa mda mfupi

A-level
Nlifaulu mchepu wa sayansi shule Fulani hivii ipo ndichii porini kabisaa nlkuwa maarufu kwa kutafutwa na walimu nlkuwa nadoji siingii vipindi siendi assembly tunashinda Chaka na wahuni naonekana sikumoja sikumoja au kweny prepo za mchana wakanipachika jina jambazi kuu. Nilivyofika form 6 nikaaribu nakumbuka mock nlipiga div 4. Disemba sikwenda home nkabak scull nipige msuli na wadau wangu nawakumbuka Sana ila ukwel nlkuwa sio msomaj kivile nikishika daftar dk 5 nasinzia still necta nikafanya wonder zaidi ya o level


JKT
Kama kawaida baada ya Zile six week za mateso nikawa dojaa marufu nlkuja kuwa mng'ao au kugundulika na maafande dakika za mwisho namalizia mafunzo nlkuwa naonekana mida ya rokoo na chakula cha usiku mda wote niko chaka nachoma ndizi viazi nakula maparachichi saa 9 usku tukishituliwa nakimbia huko na shuka langu kulala nlijulikana Kama afisa tanapa au Tarzan kwa kushinda Chaka wanangu wa D coy 825 kj wananikumbuka for privacy reasons sitotaja op na mwaka nilifahamika na nlipata marafiki wengi

CHUO
Nlipangiwa chuo flani hivi haha wanakiita secondary au form 7,university of assignments, wenye chuo wanakijua hapa movie kamili ya maisha yangu ilianza huko kote ilikuwa ni beginning nlichokikuta huko sio poa niishie hapa tu



Kitu ambacho najiuliza nilipata wapi ujasiri wakukaa porin mwenyewe, si ningezurika mm sikuwa kipanga sikuwa msomaji still nlipeform vizur Sana darasan .Mungu alinilinda

You determine your life story by the choices you make

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom