Je, Unaiamini hadithi ya mnara wa Babeli?

Je, Unaiamini hadithi ya mnara wa Babeli?

Hiyo ndiyo maana halisi ya ule msemo kwamba Mungu asemapo siyo, hakuna yeyote wa kupingana Naye.

Wakati wa vita vya pili vya dunia, Adolf Hilter alikuwa amekusudia kuwa mfalme wa dunia nzima.

Lakini alishindwa vibaya sana licha ya kuwa na jeshi imara, lenye ari na silaha madhubuti na za kisasa wakati huo.

Kwa nini? Kwa sababu Mungu alikuwa ameshatabiri kwamba himaya kubwa ya dunia baada ya Dola ya Rumi ingekuwa Marekani chini ya hisani ya upapa.

Hata China au Urusi tunayoiona leo ikielekea kama kuipiku Marekani, wote hao hawataweza kamwe kushinda.

Wataishia kuunda silaha nzito, za kutisha ambazo hazijawahi kuwepo ulimwenguni, lakini mwisho wa siku watatokomea kwa fedheha kama Adolf Hitler.

Marekani atabaki kuwa kinara ili kutimiza unabii pamoja na hisani wake Mvatikano.

Marekani yupo kuutekeleza mpango wa Mungu kwa mema au kwa mabaya hadi mwisho wa wakati.

Na anafanya hivyo vizuri sana ama anajua au hajui.

Mungu asemapo Ndiyo, hakuna mwanadamu wa kumpinga!
Wapi bible imetaja marekani au papa ulete verse usilete mafumbo
 
Kwahiyo Mungu aliogopa kwamba asipowachanganya lugha huo mnara utamfikia mbinguni?
Hapana. Aliwaona wanazidi kuwa wapumbavu kadiri siku zilivyokuwa zikiendelea.

Unajua chanzo hasa cha kuujenga mnara wa Babeli ni tukio la Gharika lililokuwa limetokea kama miaka 300 hivi kabla ya hapo.

Wakidhani kwa kufanya hivyo wangeepuka hukumu nyingine ya Gharika -- licha ya kwamba Mungu alikuwa ameahidi kutoiangamiza dunia kwa Gharika tena kamwe.

Ni sawa na leo wanasayansi wanadhani kwa kuhamia sayari zingine au hata kujichimbia mahandakini, wanaweza kuuepuka mkono wa Mfalme wa wafalme.

^Niende wapi ili niiepuke Roho Yako?
Niende wapi ili niukimbie uso Wako?

Kama ningepanda juu mbinguni, Wewe upo huko;
Iwapo ningepafanya kuzimu pawe maskani yangu, hata uko nako Wewe upo.

Ningepaa kwa mbawa kunako asubuhi, nikaenda hadi pande za mwisho za bahari, huko nako mkono Wako utanifikia.

Giza nalo halikufichi kitu, bali Kwako usiku huangaza kama mchana;
Giza na mwangaza Kwako ni sawasawa.^ ~ Zaburi 139:7-12.
 
Kwamba hapo mwanzo binadamu waliamua kujenga jengo kubwa na refu katika mji ule na kilele chake ni kifike mbinguni.

Kwamba Mpango huu haukumpendeza Mungu aliyewachanganyia lugha watu hao, wakashindwa kuelewana na baadae walilazimika kuachana na mradi huo.

Nawasilisha[emoji120]
Mungu alitaka wanadamu watawanyike duniani kote wasiishi eneo moja, wao wakiongozwa na Nimrodi walitaka wasalie eneo moja tu
 
Eti Mungu anatumia USA kukamilisha maneno yake, hizi ni chai, kikubwa ni kuamini tu ilimradi siku zisonge.
Ngoja nikuweke sawa ewe mwana wa uasi.

Iko hivi: watu wote, kila mtu, na hata kila kitu (Yesu alisema hadi mawe pia) hutimiza makusudi ya Mungu.

Lakini kuhusu makusudi makuu ya utawala wa dunia, Marekani ndiye ameshikilia fimbo hiyo.

Tangu zamani, hata wakati wa nabii Danieli na kuendelea zilikuwepo falme zenye nguvu zilizoitawala dunia ya wakati huo, kama Asiria, Babeli, Umedi & Uajemi, Misri, Rumi, nk.

Hizo zote ziliinuka na hatimaye zikasambaratika na kutoweka kwa mujibu wa maandiko.

Waliojaribu kuinuka kinyume na unabii hawakuweza. Kwa mfano akina Musolini na Hitler.

Wasovieti walijaribu, wakashindwa. Urusi na China sasa zinainuka, lakini hazitashinda.

Kwa nini? Kwa sababu haziko kwenye nafasi nzuri ya kuutimiza mpango mkuu wa Mungu kama ilivyo Marekani.

Hizi supapawa zingine ziko tu kubalansi nguvu ya Marekani na kulizuia wimbi la uovu kwa muda, lakini kamwe haziwezi kuipiku Marekani!

Siyo kwamba hazina uwezo huo. Hapana!

Sababu pekee ni kwamba hilo liko kinyume kabisa na mpango wa Mungu.

Watajaribu lakini hawataweza katu.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Wapi bible imetaja marekani au papa ulete verse usilete mafumbo
Nami nikuulize swali?

Biblia inaposema kwamba utawala fulani wa dunia utainuka na kufanya mambo kadha wa kadha bila kuutaja jina lake (rejea Ufunuo 13, kwa mfano), unadhani tunapaswa kuutambuaje???
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Mambo ya dini samutaimu yananichanganya..
Kuna kipengere Kwenye biblia kinasema samehe 7x70, kipindi hicho Adamu na Eva wake walikula tunda moja tu wakapewa adhabu kali sana bila kusamehewa na tena Kwa kosa la kwanza tu🤔
Sidhani kama unajua kuisoma hiyo Biblia hata.

Iwapo Mungu angetekeleza adhabu halisi, Adamu na mwasi mwenzie wangefutiliwa mbali palepale!

Maana yake ni kwamba mimi na wewe tusingekuwepo leo.

Ukweli ni kwamba hakuna mwanadamu ambaye amewahi kupewa rehema kubwa mno kama Adamu na mkewe.

Kumbuka hao walifinyangwa moja kwa moja mikononi mwa Mungu.

Hao ndio wanadamu pekee waliobahatika kumwona Mungu wakingali kwenye utimilifu wa usalihi wao (perfection of their innocence).

Walifundishwa na Mungu moja kwa moja na pia walifanya ushirika na malaika watakatifu.

Sasa kumwasi Mungu katika mazingira kama hayo, ilikuwa dhambi kuu isiyokadirika. (Ni kama leo ambapo wanadamu wana nuru na uzoefu wa miaka zaidi ya 6,000 lakini wamefumba macho yao kimakusudi ili tu wasiuone ukweli!)

Hata hivyo Mungu mwenye rehema tele akawapatia wanandoa hao nafasi ya pili!

Ndio wakati ambapo walitamkiwa ahadi ya ujio wa Kristu (Mwanzo 2:15) kwa kufanyika mwanadamu.

Na mavazi aliyowatengenezea Mungu yalikuwa ishara ya Mwanakondoo wa Mungu ambaye angekuja kusulubiwa msalabani ili azichukue dhambi za ulimwengu.

Hivi mtu anawezaje kudiriki kusema eti hakukuwa na msamaha kwa Adamu na Hawa?
 
Nashawishika kudhani kwamba maana ya uongo kwako ni kitu chochote usichojua au kilicho nje ya upeo wa uelewa wako.

Kwa mantiki hiyo, hata mavumbuzi na magunduzi mengi ya sayansi pengine yalikuwa uongo kwako hadi pale yalipogundulika.

Au, mwenzetu, huenda umewahi kuzurura huko angani kote ukathibitisha hakuna mbingu?

Ni upumbavu usioponyeka kujitia upumbavu kimakusudi.
Logic Ad hominem!

Acha kutumia feelings katika kujibu hoja kubwa, wewe una uthibitisho kuwa kuna mbingu angani?

Kama hauna uthibitisho kwanini unaniita mimi mpumbavu?

Mimi kusema uongo ni haki yangu maana mimi nina amini katika science research, na mpaka sasa hakuna mwana-science aliyekuja na hata theory tu ya kusema there's heaven on the sky..

Wewe unayepinga hilo kwamba sio uongo ungekuja na points zako hapa zilizoshiba kuthibitisha mbingu ipo angani na sio kuanza kuni-attack
 
Kwamba hapo mwanzo binadamu waliamua kujenga jengo kubwa na refu katika mji ule na kilele chake ni kifike mbinguni.

Kwamba Mpango huu haukumpendeza Mungu aliyewachanganyia lugha watu hao, wakashindwa kuelewana na baadae walilazimika kuachana na mradi huo.

Nawasilisha🙏
Wewe unaona hii ni kweli si story za watoto wadogo hizooo
 
Niliwahi kukuuliza kwenye ule uzi wa Israeli vs Palestina iwapo unaamini kuna UWEZEKANO wa uwepo wa Mungu, ukasema Ndiyo.
Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
Sasa hizi taarifa zingine kuhusu Babeli na zinginezo ni baadhi tu ya vithibitisho husika.

Labda nikuulize na hili leo.

Je, unadhani upo uwezekano wa wanadamu kuujenga mnara mrefu kwenda angani kama isemavyo Biblia?
Angani mpaka wapi?

Anga ni kubwa sana. Kuna layers nyingi sana.

Kujenga mnara mrefu kwenda juu angani mpaka layer ya Exosphere Haiwezekani.
NB: Sikuulizi iwapo mnara ulijengwa au la. Nazungumzia uwezekano kwa kipindi tajwa katika Biblia.
Jibu kisomi. Achana na hoja mkataa (dismissive arguments), maana hazisaidii kitu.
 
Mnara kweli usingefika mbinguni.

Ila kilichomshtua Mungu ni ile dhamira ya Binadamu kumtafuta akawasambaratisha.

Kama wangeendelea katika hali ile wangefanya mambo mengi dhidi yake.
 
Kwamba hapo mwanzo binadamu waliamua kujenga jengo kubwa na refu katika mji ule na kilele chake ni kifike mbinguni.

Kwamba Mpango huu haukumpendeza Mungu aliyewachanganyia lugha watu hao, wakashindwa kuelewana na baadae walilazimika kuachana na mradi huo.

Nawasilisha🙏
Sikiliza hapa


View: https://www.youtube.com/watch?v=zpDGyH_BhgE&pp=ygUfdGhlIHVuZmluc2hlZCBvYmVsaXNrIGF0IGJhYWJlaw%3D%3D



View: https://www.youtube.com/watch?v=8tnrkahCLHw&pp=ygUfdGhlIHVuZmluc2hlZCBvYmVsaXNrIGF0IGJhYWJlaw%3D%3D


View: https://www.youtube.com/watch?v=NiiHnWOUMw0&pp=ygUfdGhlIHVuZmluc2hlZCBvYmVsaXNrIGF0IGJhYWJlaw%3D%3D
 
hivi unajua huko juu upepo unavuma kiasi kipi?je huo mna unaweza kuhimili hizo purukushani za upepo?mungu hakuziona ndege?bibilia imeandika na kujijibu mwisho ikasema kuwa mungu hataleta tena gharika na ameweka upinde ili kukumbuka agano kwani huyu mungu wanaesema ni mzee au mgojwa wa kumbukumbu?

sometimes unaona mungu anamuuliza adamu upo wapi yaani mungu anauvaa binadamu ndiyo maana yule mshenzi alexandra I alimpa mungu akili na uhai wa binadamu eti,mungu ana nafsi 3.

upuuuuziiiii
 
Mnara kweli usingefika mbinguni.

Ila kilichomshtua Mungu ni ile dhamira ya Binadamu kumtafuta akawasambaratisha.

Kama wangeendelea katika hali ile wangefanya mambo mengi dhidi yake.
hapana binaadamu alitaka kutengeza historia na sio kutafuta mungu hivyo ndivyo bible inavosema.
 
Mimi kusema uongo ni haki yangu maana mimi nina amini katika science research, na mpaka sasa hakuna mwana-science aliyekuja na hata theory tu ya kusema there's heaven on the sky..
Hakuna sayansi inayopinga dhana fulani bila kuwa na uthibitisho wake kamili.

Sayansi ingesema hakuna mbingu, maana yake ni kwamba imefanya utafiti wake na kujiridhisha hivyo.

BTW sayansi ya kweli inaafikiana na kile isemacho maandiko, kwa vile sayansi na maandiko vyote vyatoka kwa Mungu.

Uropokaji wa kupinga jambo kwa vile tu hukubaliani nalo au liko nje ya mawanda ya uelewa wako, siyo sayansi bali ulaghai wa kishamba.

Vilevile kukana na kupinga jambo fulani usilolipenda kwa kutarajia kwamba kwa kufanya hivyo litatoweka, ndio upumbavu wenyewe wa kimakusudi.

Umesema wewe ^kusema uongo ni haki^ yako. Lakini kwa bahati mbaya sana hatuko hapa kumeza uongo wako.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Mkuu, unadhani haiwezekani au haipo kihistoria?

Je, unaamini kwamba Nuhu alijenga safina iliyotumika kuwahifadhi watu 8 dhidi ya Gharika?

Je, unaamini kwamba enzi ya Nuhu kabla ya Gharika ulimwengu ulikuwa na mabilioni ya watu, tena wenye akili ndefu (in Manara's voice) na teknolojia bora mno?

Je, unaamini kwamba Adamu na Hawa ndio wazazi wetu wa kwanza?

Je, unaamini kwamba Mungu aliumba mbingu na nchi, na kwa muda wa siku sita akaratibu mazingira yake na kuwahuluku viumbe hai?

Je, unaamini kwamba Mungu yupo?

Sijui unanielewa???

Brainwashed
 
Hii ni kwa mujibu wako. Kauli tu bila vithibitisho vya maana ni pumba tupu.

Do you have any evidence kuwa bible au quran ni kitabu cha Mungu ?

Usinipe story za Roho mtakatifu, nipe hard evidence out of bible kuwa ni kitabu cha muumba !
 
Back
Top Bottom