Je, Unaiamini hadithi ya mnara wa Babeli?

Je, Unaiamini hadithi ya mnara wa Babeli?

Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
Kwa hiyo unajipinga mwenyewe ama umebadili msimamo wako?

Angani mpaka wapi?

Anga ni kubwa sana. Kuna layers nyingi sana.

Kujenga mnara mrefu kwenda juu angani mpaka layer ya Exosphere Haiwezekani.
Nachukulia haya maelezo yako kwamba umekubali; upo uwezekano huo wa kujenga mnara hadi angani.

Kisayansi, hiyo ni hatua muhimu sana katika utafiti.
 
Brainwashed
Hoja mkataa (dismissive arguments) kama hizi hazisaidii kitu. Mara nyingi ni kauli za waishiwa-hoja.

Nashangaa kwa nini msomi kama wewe hujagundua hilo.

Kama huna hoja kinzani, ukimya ni jambo la busara sana.

Do you have any evidence kuwa Bible au quran ni kitabu cha Mungu?
^Hard evidence^? Define hard evidence.

Je, ni uthibitisho unaoweza kuuamini wewe, ama ni ule ambao upo kihalisia?

Kwa sababu uwepo wa vithibitisho na kuviamini, ni mambo mawili tofauti kabisa.

Usinipe story za Roho Mtakatifu, nipe hard evidence out of Bible kuwa ni kitabu cha Muumba!
Unahitaji ushahidi, wakati huohuo unachagua utoke au usitoke wapi?

Maana yake umejaa nahaba (bias) hata kabla ya kuuona ushahidi wenyewe?

Pili, unahitaji vithibitisho kutoka nje ya Biblia na wala siyo ndani yake.

Huoni kwamba tayari umeshajichagulia nini cha kuamini na nini usiamini?

Kwa nini uwaamini waandishi nje ya Biblia, ilhali walioiandika Biblia unawaona hawafai?

Kwa nini ushahidi wote usitathminiwe kwenye uwanja na mawanda sawia?

Simply put, you can never be a scientist; may be a nominal one.
 
Hiyo ndiyo maana halisi ya ule msemo kwamba Mungu asemapo siyo, hakuna yeyote wa kupingana Naye.

Wakati wa vita vya pili vya dunia, Adolf Hilter alikuwa amekusudia kuwa mfalme wa dunia nzima.

Lakini alishindwa vibaya sana licha ya kuwa na jeshi imara, lenye ari na silaha madhubuti na za kisasa wakati huo.

Kwa nini? Kwa sababu Mungu alikuwa ameshatabiri kwamba himaya kubwa ya dunia baada ya Dola ya Rumi ingekuwa Marekani chini ya hisani ya upapa.

Hata China au Urusi tunayoiona leo ikielekea kama kuipiku Marekani, wote hao hawataweza kamwe kushinda.

Wataishia kuunda silaha nzito, za kutisha ambazo hazijawahi kuwepo ulimwenguni, lakini mwisho wa siku watatokomea kwa fedheha kama Adolf Hitler.

Marekani atabaki kuwa kinara ili kutimiza unabii pamoja na hisani wake Mvatikano.

Marekani yupo kuutekeleza mpango wa Mungu kwa mema au kwa mabaya hadi mwisho wa wakati.

Na anafanya hivyo vizuri sana ama anajua au hajui.

Mungu asemapo Ndiyo, hakuna mwanadamu wa kumpinga!
Kwahio hii mipango ni ya kumfurahisha nani ? Wengine wateseke, Wengine wafe, Watu wanafanywa watumwa, Wanabakwa sababu Mungu alisema / amesema ndio ? For whose benefit ?

Au wale walioshika mpini ndio wanaku-convince wewe uendelee kupigika na kunyonywa sababu ni mpango wa Mungu ?

Unaongelea America hili Taifa Jipya wakati kuna Empires zilishapita hata USA hawezi kunusa (ila empires rise and fall) hio ni kawaida; Ingawa wewe unaona Mungu alipanga watu (Europeans) waende kuwauwa hao Red Indians na kuwasubjugate ili neno lake litimie ?
 
Nami nikuulize swali?

Biblia inaposema kwamba utawala fulani wa dunia utainuka na kufanya mambo kadha wa kadha bila kuutaja jina lake (rejea Ufunuo 13, kwa mfano), unadhani tunapaswa kuutambuaje???
Roman
Ottoman
British empire.
Germany under Nazi
Soviet union
Unasema marekani kwa sababu upo saa hivi waliosoma huo mstari zamani walidhani ni ottoman walidhani ni uingereza etc so bado huna hoja ya kuniconvince zaidi ya brah brah tu
 
Mkuu, namna yako ya kuisoma Biblia ni ya mashaka sana.

Hebu nukuu andiko lako ili watu wakusaidie kufafanua; vinginevyo utaendelea na ujinga wako katikati ya bahari ya maarifa.
Maarifa yapi kwenye biblia,

Kusoma kwa ufahamu nako unakutilia mashaka!?

Unadhani kunukuu kutabadilisha mchanganuo wa andiko nliokuandikia hapo!?

Unaelewa kitu kinaitwa kusoma kwa ufahamu!?
 
Hakuna sayansi inayopinga dhana fulani bila kuwa na uthibitisho wake kamili.

Sayansi ingesema hakuna mbingu, maana yake ni kwamba imefanya utafiti wake na kujiridhisha hivyo.

BTW sayansi ya kweli inaafikiana na kile isemacho maandiko, kwa vile sayansi na maandiko vyote vyatoka kwa Mungu.

Uropokaji wa kupinga jambo kwa vile tu hukubaliani nalo au liko nje ya mawanda ya uelewa wako, siyo sayansi bali ulaghai wa kishamba.

Vilevile kukana na kupinga jambo fulani usilolipenda kwa kutarajia kwamba kwa kufanya hivyo litatoweka, ndio upumbavu wenyewe wa kimakusudi.

Umesema wewe ^kusema uongo ni haki^ yako. Lakini kwa bahati mbaya sana hatuko hapa kumeza uongo wako.
Kwani mbinguni ni wapi kama siyo hapo kwenye mawingu?
 
Mkuu, unadhani haiwezekani au haipo kihistoria?

Je, unaamini kwamba Nuhu alijenga safina iliyotumika kuwahifadhi watu 8 dhidi ya Gharika?

Je, unaamini kwamba enzi ya Nuhu kabla ya Gharika ulimwengu ulikuwa na mabilioni ya watu, tena wenye akili ndefu (in Manara's voice) na teknolojia bora mno?

Je, unaamini kwamba Adamu na Hawa ndio wazazi wetu wa kwanza?

Je, unaamini kwamba Mungu aliumba mbingu na nchi, na kwa muda wa siku sita akaratibu mazingira yake na kuwahuluku viumbe hai?

Je, unaamini kwamba Mungu yupo?

Sijui unanielewa???
Hapa Kiranga anaweza kukupa maswali counter ukakimbia kabisa
 
Hoja mkataa (dismissive arguments) kama hizi hazisaidii kitu. Mara nyingi ni kauli za waishiwa-hoja.

Nashangaa kwa nini msomi kama wewe hujagundua hilo.

Kama huna hoja kinzani, ukimya ni jambo la busara sana.


^Hard evidence^? Define hard evidence.

Je, ni uthibitisho unaoweza kuuamini wewe, ama ni ule ambao upo kihalisia?

Kwa sababu uwepo wa vithibitisho na kuviamini, ni mambo mawili tofauti kabisa.


Unahitaji ushahidi, wakati huohuo unachagua utoke au usitoke wapi?

Maana yake umejaa nahaba (bias) hata kabla ya kuuona ushahidi wenyewe?

Pili, unahitaji vithibitisho kutoka nje ya Biblia na wala siyo ndani yake.

Huoni kwamba tayari umeshajichagulia nini cha kuamini na nini usiamini?

Kwa nini uwaamini waandishi nje ya Biblia, ilhali walioiandika Biblia unawaona hawafai?

Kwa nini ushahidi wote usitathminiwe kwenye uwanja na mawanda sawia?

Simply put, you can never be a scientist -- may be nominal one.
Huwezi kutumia biblia ama quran kuthibitisha kuwa vimeandikwa na Mungu huyo!!

Kufanya hivyo utakuwa unafanya kosa kubwa la kimantinki.

Yaani unafanya circular argument, kwamba madai yanatumika kama uthibitisho.

Imagine biblia iwe kweli tu kuwa ni kitabu cha Mungu kwasababu ndani yake imeandikwa kuwa ni kitabu cha mungu!!

That is illogical.

Unaweza thibitisha Mungu yupo kweli na kwamba hizo hadithi za kwenye biblia na qurani si hadithi za uongo tu zilizotungwa na watu wajinga wajinga tu wasioelewa hata jua linaenda wapi usiku!?
 
Kwamba hapo mwanzo binadamu waliamua kujenga jengo kubwa na refu katika mji ule na kilele chake ni kifike mbinguni.

Kwamba Mpango huu haukumpendeza Mungu aliyewachanganyia lugha watu hao, wakashindwa kuelewana na baadae walilazimika kuachana na mradi huo.

Nawasilisha🙏
Je? Unaamini pyramid zilijengwa na wanadamu?
 
Kwa hiyo unajipinga mwenyewe ama umebadili msimamo wako?
Hakuna sehemu nilisema hivyo.
Nachukulia haya maelezo yako kwamba umekubali; upo uwezekano huo wa kujenga mnara hadi angani.

Kisayansi, hiyo ni hatua muhimu sana katika utafiti.
Nakwambia hivi Haiwezekani kujenga mnara mrefu kwenda juu angani mpaka layer ya Exosphere.
 
Sijui ni mimi tuu, ila habari za kwenye biblia haziniingii kabisa akilini achilia mbali kwenda kanisani
Mkuu, ni kwa vile hujatulia ukaisoma Biblia vizuri.

Tafuta likizo moja tulivu hivi, jitafute peke yako na Biblia, utakuja kunishukuru baadaye.
 
Natamani nikwambie mambo ya Yale ma pyramids pale misri kua ndo mnara wenyewe Ila kwa sababu najua utabisha ngoja tu kikae kimya
 
Maarifa yapi kwenye biblia,

Kusoma kwa ufahamu nako unakutilia mashaka!?

Unadhani kunukuu kutabadilisha mchanganuo wa andiko nliokuandikia hapo!?

Unaelewa kitu kinaitwa kusoma kwa ufahamu!?
Awali uliuliza swali la Biblia, nikakutaka unukuu andiko ulikotoa swali lako, ili ujibiwe.

Mbona tena maelezo mareefu babu!?
 
Mkuu, unadhani haiwezekani au haipo kihistoria?

Je, unaamini kwamba Nuhu alijenga safina iliyotumika kuwahifadhi watu 8 dhidi ya Gharika?

Je, unaamini kwamba enzi ya Nuhu kabla ya Gharika ulimwengu ulikuwa na mabilioni ya watu, tena wenye akili ndefu (in Manara's voice) na teknolojia bora mno?

Je, unaamini kwamba Adamu na Hawa ndio wazazi wetu wa kwanza?

Je, unaamini kwamba Mungu aliumba mbingu na nchi, na kwa muda wa siku sita akaratibu mazingira yake na kuwahuluku viumbe hai?

Je, unaamini kwamba Mungu yupo?

Sijui unanielewa???
Hujajibu hoja ya mleta uzi
 
Kwani mbinguni ni wapi kama siyo hapo kwenye mawingu?
Ni kweli.

Katika Biblia mawinguni nako ni mbinguni, japo siyo kwenye makao halidi ya Mungu kwa mujibu wa maandiko.

Lakini hebu nikupe faida ya mashaka kwamba uko sahihi.

Je, kufika tu hapo angani ndipo kuthibitisha kwamba hamna mbingu halisi?

Unajua pakoje hasa? Panaonekana kwa macho haya ya nyama?

Nadhani tufike hatua kama wanadamu tukiri tu kwamba kuna mambo yako nje kabisa ya upeo wetu.

Kukiri hivyo siyo udhaifu bali ni hekima. Kushupalia tusichokiweza ni sawa na kupiga ngumu ukutani.
 
Hakuna sehemu nilisema hivyo.
Je, unanithibitishia kwamba kuna hoja halisi ya uwepo (argument of existence)?

Namaanisha kwamba uwepo wa viumbe ni nadharia tu ama ni halisi?

Au tu akili zetu zinaota, na kwamba hakuna chochote kilicho yakinifu/halisi (kama wadaivyo wengine -- jambo ambalo wala halihitaji kufikiri ili kubaini kwamba haliwezekani)?

Nakwambia hivi Haiwezekani kujenga mnara mrefu kwenda juu angani mpaka layer ya Exosphere.
Majibu yako yameshathibitisha kwamba umekubali kuna uwezekano huo (rejea maelezo ya awali).

Huenda hujaelewa swali (japo umejibu kwa usahihi).

Nimeuliza (mfano): Unaweza kuruka?

Umejibu: Siwezi kuruka zaidi ya mita 2.

Hitimisho ni kwamba naam, unaweza kuruka!
 
Hujajibu hoja ya mleta uzi
Mkuu, sijui kama umegundua kwamba mleta-mada hajauliza swali lolote wala kuomba msaada?

Nimeona maelezo tu, nikajua anatualika kuingia uwanjani freestyle, ndiyo maana mie nikaamua kumswalisha.

Nasimama ili nirekebishwe! 🙂
(Niko radhi ku...)
 
Dini zimewajaza hofu na uongo mwingi Mungu yupo juu tukifa tunazikwa chini kwa nini Mungu asiwavurugie lugha watengeneza Rockets na setilites
 
Back
Top Bottom