Umemaliza kila kitu MTU asipoelewa hayo maelezo basi atakuwa na matatizo ya akiliPossibility ipo,lakini itategemea na uhitaji wa jeshi kwa wakati huo.Nijuavyo mimi,kwa sasa jeshi linahitaji sana wataalamu wa afya,kilimo,uhandisi na wasanifu majengo na marubani na wapiganaji(wale darasa la saba na form four)
Kimsingi ,usiende jeshini kusaka ajira..Utateseka,utaumia na utajutia..Kamaa unalipenda jeshi kutoka moyoni,nenda,lakini kama unaenda kwa sababu kitaa hapasomi,utatoroka depo
"Kama huwezi chezaa katafute refa wa kukubeba " by DARASAWakuu kwanza nashukuru kwa thread hii..Mimi Nina swali kwenu mliopita jkt,je Mara MTU unapokuwa umeapply kujiunga jkt kwa wilaya yako,je no utaratibu gan hutumika kuwaita watu kwenye interview?msaada tafadhar wakuu,
Dodoma interview tarehe 5 watu wanaambiwa njoo siku ya interviewWakuu kwanza nashukuru kwa thread hii..Mimi Nina swali kwenu mliopita jkt,je Mara MTU unapokuwa umeapply kujiunga jkt kwa wilaya yako,je no utaratibu gan hutumika kuwaita watu kwenye interview?msaada tafadhar wakuu,
Umenikumbusha mbali sana mie niliudhuria ile miaka ya mwishoni ya themanini (1989/90) Pale kambi ya Ruvu kombania ya B kuna afande alikuwa anaitwa Nyundo. Huyu afande hatukubahatika kumuona akiwa amefurahi kila siku sura yake ili kuwa ya kazi kazi. Mwenyewe alikuwa anajiita ndio handsome wa kwao.
Nakumbuka moja ya wimbo ambao alitufundisha muda wa disco ulikuwa wa Malela.... na mwingine ulikuwa nadhani wa kishona kama sijakosea unaitwa Kule kule kwa chinoma....
Kitu kingine nakumbuka ni ufugaji wa kuku kule phase 2 pamoja na kusimamisha minazi serengeti muda wa jioni.
Unakumbuka Enzi za JKT kamanda kikosi ndie alikuwa mwenyekiti wa CCM wa tawi hilo, kwa hiyo kuna siku mnakaa naye kama mwenyekiti wa chama hahahahahahahahNaam tulijengewa mioyo ya Uzalendo,tofauti zetu ziliwekwa kando (ukabila,udini,utajiri,umasikini) Wote tulikuwa kitu kimoja.
Kama hii JKT ya zamani ingeendelezwa na humo ukaongezwa mfumo wa taaluma mbalimbali za kujiajiri na ujasiriamali Cum VETA,........CUBA na China wasingelitupata.
Bado namkumbuka Col.Mlay , Ndani ya Mafinga.
Au VOP!!
Oljoro nakumbuka mashamba ya Dunia na Embakasi. Siku moja tukaenda kulima miraba shamba la njiani kama unakwenda Farm, tukiwa na A Coy. Uji ukaletwa na tata la jeshi. Bravo Coy wakashusha uji wakanywa wote na A coy. Tifu baada ya hapo lilihamia hadi kwa maafande. Kulikuwa hakuna namna maana uji ushanyweka [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38]Wale wa Makutupora na Ol joro.....
Mduda [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38]. Anajifanya anaujua mpiraaa [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38].Sanctus,
Mimi niliamua kukwepa kwenda Tabora na kuamua kwenda Oljoro kwasababu nilikuwa na kakangu mjini Arusha. Nikajua nikitoroka nitakuwa na sehemu kwa kubugia ugali.
Basi kufika Oljoro, tukamkuta afande Dauda, (sijui kama linaandikwa hivyo) alikuwa ndio mkuu wa mafunzo. Akasema mwaka jana alitoa kibali cha kuua kruta watano, akasema aligundua haikutosha, anawaamrisha maafande mwaka huu kuua kruta mpaka 15.
Kesho yake watu kibao wakatoroka na kwenda ku report kambi zingine. Isingelikuwa kuwa na brother hapo mjini na mimi ningelirudi kule Tabora usiku huo. Baada ya muda tukaja gundua kumbe Dauda ndiye alikuwa afande poa kuliko wengine wote.
Tulikuwa na afande mmoja Mhehe alikuwa anaitwa Mduda. Alikuwa anajifanya anajua jeshi kweli kweli. Akaopoa mtoto wa maana sana. Siku moja tumemaliza jeshi tuko mlimani, akaingia mlimani hall D na magwanda, kaja kufuata mtoto wake. Maskini yule msichana alikuwa terrified, akajificha. Jamaa akasubiri pale wee, mpaka akaamua kujikata. Alifikiri yale ya jeshini yanaendelea uraiani. Tulimsanifu kweli siku hiyo.
Looh! ni miaka karibu 20 toka wengine tuondoke JKT lakini naona michapo yake inakuja tu. Waswahili tungelikuwa tunaandika vitabu, tuna mengi ya kusimulia.
Namkumbuka Afande Mutu na Maganga wa Danger Coy Maktupora (1983). Na Afande Doto alivyokuwa anamsumbua John Pombe Magufuli
Duh 1983 wengi wetu humu tulikuwa hatujaliona jua.Mkuu ulienda jeshini kambi moja na JPM?
Unaikumbuka kauli hiiOljoro nakumbuka mashamba ya Dunia na Embakasi. Siku moja tukaenda kulima miraba shamba la njiani kama unakwenda Farm, tukiwa na A Coy. Uji ukaletwa na tata la jeshi. Bravo Coy wakashusha uji wakanywa wote na A coy. Tifu baada ya hapo lilihamia hadi kwa maafande. Kulikuwa hakuna namna maana uji ushanyweka [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38]
Basi tupeni heshima zetu,Duh 1983 wengi wetu humu tulikuwa hatujaliona jua.
Ndiyo maana hili jukwaa linaheshimika sana, kuna mchanganyiko mzuri sana (wazee, watu wazima na vijana). Safi sanaBasi tupeni heshima zetu,
Nakumbuka sana. RSM anakuja usawa wa kombania na mpo kwenye pilika za kwenda usawa wa gudulia saa saba mchana lakini mnalifikia gudulia saa tisa wakati kutoka kombania hadi usawa wa gudulia ni 70 au 80 [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38].Unaikumbuka kauli hii
''Leo chakula mtakula MBAUDA''
Mita 70 au 80Nakumbuka sana. RSM anakuja usawa wa kombania na mpo kwenye pilika za kwenda usawa wa gudulia saa saba mchana lakini mnalifikia gudulia saa tisa wakati kutoka kombania hadi usawa wa gudulia ni 70 au 80 [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38].
Afande anakwambia mmeacha magunia mangapi ya mahindi kwenu unakimbilia ugali wa jeshi, halafu anamalizia na tusi: Deemkuuk [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38]
Hahaa mkuu umenifanya nicheke kwasauti sana aseeenzi zile makamanda hawakuwa na shule kabisa na walijitahidi kukariri maneno machache ya kingereza na kuyatumia kila mara.....nakumbuka ile adhabu ya push up!!!!!afande atakwambia ....haya...chini!down!chini!down....akimaanisha juu ..chini sasa ujifanye hujamuelewa!!!cha moto utakiona kwa kujifanya msomi!!!