Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Mi nakumbuka adhabu ya mwendo wa kukwepa ndege kule Makutopora operesheni imarisha. Sitakuja kaa nisahau nilivyozika nguruwe peke yangu chini ya Afande SemiGod
 
Nilikuwa KJ 288 OLJORO Junta Kusoma Tanzania.F/N.Z6346 Eagle Coy Operation Kambarage.Nakumbuka kuchonga matofali ya mawe kule kwa Laseko na jinsi Wamasai walivyotusumbua kwa kuchoma nyasi kwenye eneo la Rench hadi tukapewa ruhusa ya kuwafunza adabu kwa kuwachapa mikanda.
 
Hizi operations zenu za jana! Sisi za kwetu za seventies zilikuwa ndio zenyewe. Tuliokwenda 'kwa mujibu wa sheria! (yaani after college) siku chache za mwanzoni tulipata shida kidogo ku-'adjust' Lakini baada ya kuzoea it was absolutely fantastic
 
Daaah, nakumbuk six weeks nlitoroka nikaenda kwa mama hidaya pale kwa dosa (ruvu 832kj). Sasa nimerudi nayumba baada ya kunywa kachaso niko maeneo ya uwanja wa vikwazo kumbe si mp ndomba ametake cover anangoja kufanya ambush? Kilichotokea ndio kilipelekea nipewe a.k.a ya ninja mpaka leo hii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulikuwa Operesheni ipi?
 
Tarama yupo wapi siku hizi? jirani yangu kule Suca kwenye bomoa bomoa
 
Ndoa ya Urio na Makame ilikaa miaka kadhaa nafikiri. Nilikuwa Ruvu Operesheni Miaka 30 na Urio alikuwa CO, nikahamia Mlalakua baada yakuwa Serviceman na Makame ndio alikuwa Mkuu wa JKT.

Yule afande mnyakyusa alipata msanga... alikuwa anatembea na kuruta mwenzetu na walipata ajali mbaya sana yule dada nasikia ali-paralyze sina uhakika kama Afande alipona au alitutangulia
 
Mwamasangula aliletwa C Coy... F mlikuwa na warembo wengi...nakumbuka...
 
Kijana Kombania yenu ilikuwa ya wanyonge wa Vibwende. Mambo yote yalikuwa Alfa.
Hivi F ndio walikuwa wanakaa kule jirani na kiwanda cha nguo au wale walikuwa Special Coy? Nyundo alikuwa kwenu au B? OCwenu alikuwa poa sana...C tulikuwa na Mama Moshi lakini mambo yote yalikuwa nawarrant officer Sanga.. Mnamkumbuka afande Filipo alikuwa anacheza handball? Merdad alikuwa C Coy. na yule korokoro mwingine Mmasai
 
Du zamani sana!, Enzi hizo Baba wa taifa JKN ndio POURT, waziri mkuu ni Edward Moringe Sokoine,Gen Musuguri ndio Kinara pale juu majeshini. Kambi yangu ya ni uzalishaji mahindi JKT Mlale,Operation 'kujihami kiuchumi baada ya vita', Mkuu wa kambi ni Luteni kanali Kajembe, Meja Mandwa mkuu wa operation zote kambini, B-Coy ndio ilikuwa kombania yangu, platoon ya kwanza section ya demo ya kina Nkayamba Abeid,Nko,Solomon,Mwasha mim na kina Nyihirani, Makamanda akina Bahati, Sondora mutini kalikaka, na afande Before!, chini ya Sir major Ndaga na Lt Ndangura. Kama niliowataja wamo humu tujikumbushe jinsi tulivyohenya wakati huo. Najivunia sana kuwa katika jeshi la akiba hadi leo.
 
Section ya mananga wa demo[emoji23] [emoji23]
 
Kumbe wazee wengi humu JF!
 

Operation gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…