Jayfour kumbe ni wewe? Wewe si ulikuwa ujenzi na akina Edward Nzigula na yule Engineer mwingine mjita mlikuwa mmetoka naye Mbeya Technical, alikuawa anaitwa Ngosi kama sikosei! Kole Sadiki yuko wapi?
Aisee mbona hujanitaja aisee babaangu? Au kwa vile niliwaacha kombania nikahamia chokaa kwa afande Mayila? Kazi inaisha saa 4 halafu tunaanza kuogelea ziwani, afande Jogoo na Makere wakija hatuelewi kitu.
Kule tulikuwa na akina Reuben Nkori, Busagala Masale, Haule, Mbuna, Chambo.
Wakati niko kombania mimi ndiye nilikuwa natangulia pale mbele ya mstari tukiwa na Karume Mbulwa ambaye baadaye alikuja kuwa ni RP, halafu wanafuatia wengine kama akina MC Nyamhanga, Commandoor Katani. Nawakumbuka sana wasichana wa Danger Coy akina Winifrida Bita, Eda (mnapata kichere mnakwenda kaseke), Esther Koroti, Yasinta John (kasheshe yake na afande Pima kwenye chenja unaikumbuka?, alirudia kutaja jina kama mara mia pale mbele ya hanga la wavulana D-coy).
Siku moja nikaokota filimbi. Niko na jamaa alikuwa anaitwa Mbogo Mnubi usiku katikati ya mahanga ya D na C, kule nyuma, nikawa napuliza filimbi "fiii" halafu Mbogo akawa anasema "ruka, ruka", halafu mimi naruka kichura na buti zangu pwaaa pwaaa, mahanga yote yakatimua mbio usiku chaga za vitanda zinadondoka chini watu wakadhani ni ma MP wako around. Baadaye na sisi tukakimbia kuogopa kibano sababu watu waligundua kuwa tumewachezea akili.
Mabigula ya usiku kwenda kuzima moto, tumeingia uchaka sana unaondoka na Blanketi mbili, kurudi majaliwa.
Mimi ndiye niliyekuwa naigiza sauti ya yule afande giant msukuma coplo alikuwa anaitwa Bujiku wa uvuvi. Akikukamata push-up una kosa anakwambia, "nipe zangu mbili, OC, Sir Major wa kombania naye tatu, OC naye nne,.... yaani we acha tu".
Halafu siku moja tunapiga kwata uwanja wa damu, mzee wa kadebula a.k.a commandoor Makoba akaingia ghafla halafu lisichana limoja la D-coy likaropoka "Cock up", mama yangu, kumbe amesikia! Akaanza, " nani amesema cock-up hapa, eeh nai,....jenga reli,... yaani ilikuwa ni issue, choka mbaya! Jeshini we acha tu, hadi nilitaka kuwa kujiunga nikasomee u-Rubani wa ndege szile ndogo za jeshi, Mungu hakujalia!