Wakuu nimecheka mpaka mbavu zinauma.
Jamani enzi zile haki za binadamu ilikuwa vipi? Pale Makutupora kuna makruta walikamatwa usiku wamesimamisha minazi...wakaswekwa lupango.Kesho yake, duh! MP aliwachukua akawa awakimbiza kila mahali wakiimba " sisi ni malaya wa kikosi". Kila kulipo na kundi la watu wanapitishwa wakitroti na kuimba kawimbo hako!. Baada ya hapo waliachiwa, lakini kweli walidhalilika.Likatokea bogi la kwenda Bulombora, hawakuwemo lakini wakaomba..wakaunganishwa haoooo...Bulombora.
Tulipofika tu, tulipewa tips za kuishi jeshi na maservice waliokuwa wamebaki. Mfano, mkiwa wengi na afande akaita mtu mmoja au wwawili waje...basi kauka tu...maana unweza jitolea ukakuta kuna anakuitieeni bonge la kazi. Siku moja pale combania A afande alikuwa kwenye hanga letu akachunguliwa akesema, 'watu waili waje hapa". Mimi nilikuwa tu karibu na mlango nikajua nikikauka ngoma inaweza ikawa nzito kwangu..nikaenda. Nakumbuka jamaa mmoja aliitwa Mwinyijuma alikuwa mwisho kabisa wa hanga naye akaje..wengine wamekauka kauu! Tulipofika kwake akatumbia kachukueni mizigo yenu mnahamia kwenye kibanda cha shamba la zabibu nyeupe. Salaaaale! balaa yageuka bahati..maana tulishapewa dili hiyo kwamba huko ndiko raha zilikogunduliwa. Tuliporudi hangani jamaa wakatuuliza, vipi kwapa kazi gani? Tukajibu, kitengo cha zabibu nyeupe. Kila mtu alijilaumu kwa nini hakuenda wakati afande Hamis aliita. Walijua ni kushusha magunia ya maharage kwenye gari(maana ndi thadhari tuliyopewa)
Huko kwenye kitengo laifu ilikuwa bombaaaaaaa...kula zabibu nyeupe kwenda mbele.Kwa wasiozijua zabibu nyeupe...mmmh, ni tamu mpaka saa nyingingine vindege unaweza vikamta vinang'ang'ani.
Jamani kwa wale wa makutupora, kula nyanya mbichi mnakumbuka? Unamwagilia nyanya chini ya ulinzi mkali wa afande, akiangalia pembeni kidogo, unachokua nyanya na kupeleka direct mdomoni. imeoshwa? mmmh saa ingine unaweza lenga uliyoiona mbivu kumbe umechukua mbichi na ukaizamisha mdomoni. Kazi kuitema maana afande anaweza geuka akakuona...unameza tu.
Kombania A kulikuwa na kiafande kinaitwa Mwashamba..ebwana hiki kijamaa noma kweli. ati mchakamchaka kinakuja kutuamsha kwa kurusha mchanga kiduchu kwenye bati halafu nduki...wale watakosikia ndio haohao....kinahesabu namba na kuleta fadhaa.
Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, kwa wale wasienda JKT hawataelewa hiyo experience tuliopata....lakini ilikuwa na very exiting experience japo kwa sasa ingekuwa disaster hasa ukiangalia hili janga la Ukimwi.
Jambo afandeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.