Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Afande molel yupo kimbiji jkt now
 
Siri za jandoni zinabakia jandoni. Msiwafanye watoto wakaogopa kujiunga na mafunzo ya awali ya kijeshi wakihofia hizi stories.
Kuna mengine yako so exciting unapojikuta unakabiliana nayo bila kuwa na Intel yoyote "KUNYWA MAJI MENGI MOYO UELEE"
Ok hizi ni stories za JKT ila hutakuta waliopita RTS/ walioko chomboni wakisimulia haya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli kabisa maiki tango.
 
uzi upo gud Mgambo JKT nilikuwa combania B chin ya afande shija,( matron grace, afande Idd, Bahati volotia leader walikuwa wana roho mbaya) afande kibakuli saivi ni comando, afande kafufi aliamishiwa tabora, afande james balaa lake ni hatari na afande kishoka mzee wa mchanganua alikuwa anapenda rushwa, ukimsifia tuu mkesha unapungua makili sasa bc mkiimba chelume combania zikingine wanasema sisi wachawi siwezi maliza yote.................................................
 
Kutoka Ruvu JKT kombanila "C", mimi kabugira na Athanas kutoka Lindi tumechaguliwa kwenda kuchunga ng'ombe siku inayofuata. Asubuhi baada ya kuchinja ng'ombe wa kitoeo tukafanikiwa kupewa maini pamoja na kopo la kimbo lililoisha mafuta, tukaondoka na ng'ombe kwenda machungoni. Tukiwa huko tukakaanga yale maini tukala tukatosheka. Jioni tumerudi baada ya kuwafungia ng'ombe zizini, tukapita usawa wa jikoni na kukuta gudulia la nyama linatokota jikoni, nikaingiza Messtin nikachota nyama! Kumbe nimeonwa na MP bhana, nikatupa ule Messtin, lakini ajabu ilidondoka na nyama zote zimo intact, MP kachukuwa kama kielelezo. Tulirushwa kichura toka getini hadi C coy usawa wa ngedere!!! [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

kutoka: 22D Arnold st.
 
Mkuu wee ndio tulikuita mlinzi wa kudumu? Wait fulani hici au sio? Afande Erick alikuwa anakapenda ka chenja "shebele zanjaro"

Mimi ndio nilikwepa kombati alizonichagulia ahaz akanirushia zikaanguka chini nikaenda kuchukua nyingine kwa afande mgeni ,mkaanza kumzomea ahaz halafu mkala doso kipind nishakimbilia michungwani
 

Haha yule mwingine alikuwa mweupe anaitwa kev mm ni anga la chini
Unamkumbuka ciprian ngereza kama sijajosea jamaa alikuwa analala f coy ila ni b coy alikuwa doja kinyamaa


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Haha yule mwingine alikuwa mweupe anaitwa kev mm ni anga la chini
Unamkumbuka ciprian ngereza kama sijajosea jamaa alikuwa analala f coy ila ni b coy alikuwa doja kinyamaa


Sent from my iPhone using JamiiForums
Namkumbuka ngereza alikimbia akawa anatafuta kinoma.Kumbe alihamiaga f coy bhana.Yule matron msela hivi alikuwa anafungwa sana anaitwa laida unamkumbuka?
 
dah mkuu umenikumbusha afande nusu mungu ...yesu na maria noma sana..tulikua nae msange jkt huyo MTU ..anamikwala mizito sana nakumbuka siku yakupangiwa kombania walijipanga ma sir meja watano watu wakawa wanafolen nyuma yao ndo kombania yako..bas jamaa akawa anapiga mikwala sana ye kashamsulubu kawawa ..anaweza kukubadilisha vyovyote kashindwa roho tu ukimix na sula yake kama nduli amini...watu wakawa wanakimbia kufolen kwake ..dah wengne tukafolen ivo ivo kwake kinyonge ..mwisho wa siku tukaja kujua kumbe ni mtu poa t sana ...ana mikwala tu mingi..
 
Acheni kabisa,nakumbuka 92-93 nilikuwa kambi ya Maramba Op Vyama vingi, CO akiwa Col Lyaruu,nilikuwa zamu nikaacha lindo langu mimi na mwenzangu SM Eradius Temba tukaenda kugonga chupa kadhaa za boha nikamix na mnazi, kumbe MP wa zamu L/Cpl Mwankenja alipata taarifa kuwa kuna baadhi ya walinzi wameacha vituo vyao na kwenda kunywa BOHA na MDAFU, siku hiyo sitasahau sekeseke nililokumbana nalo, tukiwa njiani kurejea kwenye vituo vyetu kupitia uwanja wa mpira uliokuwa karibu na kilabu cha boha wakati tunaingia kwenye shamba la mikokoa ili tuibukie hangani kubadilisha nguo ghafla tulisikia sauti simamaa!! kucheki nikamuona Mwankenja na baka lake la MP, sio siri MP alikuwa anaogopwa vibaya sana, nilijaribu kulala mbele lakini kutokana na kinywaji nilichogonga alifanikiwa kunidaka nilijaribu kujipapatua lakini ilishindikana ikabidi nijijenge tukaanza kupiga mkono yeye anapiga combat karate, mimi napiga mchanganyiko wa Shotokan, Gojoryu na Kun fu nilimpa vitu vya uso na mbavu alivyoona namzidi alipuliza filimbi kuomba msaada kwa vile eneo la mapigano halikuwa mbali na kambi, walitokea MP wawili zaidi Cpl Nyambo na Sgt Amani masharubu, aaaah! nilikula doso la hatari pigwa virungu sana na kwata mchanganyiko ikiambatana na vichura, Pushups na kukwepa ndege kufika Q/gurd niko hoi, doso likaanza upya pigwa tifu sana, MP mmoja wa kike L/Cpl Rukia akanionea huruma sana, wakati suluba ikiendelea nikamuona Eradius Temba naye akiletwa mlangoni akiwa chini ya ulinzi wa MP Sgt Sambangula, wale waliokuwa wananisulubu wakahamia kwa Temba wakaniacha ndipo yule MP wa kike Rukia aliponitoa pale kimtindo na kunipa fatiki ya kukwangua nyasi eneo la Ofisi ya MP, nikamsikia Temba akilia kama mbuzi kwa kibano alichokuwa akikipata. Nikiwa naendelea na fatiki nikamuona 2i/c OC wa kombania yangu Lt Songela akiwa na CSM Mteule Meshi wakija mlangoni mzee Songela akiwa ameshika fimbo, nilipomuona roho ikapasuka paa!! alikuwa mzee mtata sana, baada ya kufika pale alipewa maelezo na L/Cpl Mwankenja jinsi tukio lilivyokuwa, Aisee yule mzee akaanza kunishushia tena kipigo cha nguvu na ile fimbo aliokuwa nayo.
 
Maramba pale nlifanya msala mmoja wa hatari sana
 
Mimi operation Kambarage 1990/1991. Oljoro/Makuyuni. Naomba niandikie mistari yote ya wimbo wa kulekule kwa chinoma/chinova! nimeusahau. Namkumbuka sana Afande Kunesa/Salum wa jikoni. Ukimwambia chakula kidogo anakujibu, mwaga kanywe maji kalale.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…