Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Bubu Msemaovyo,
Dah- Mkuu kumbe ulipita Mafinga ... na Mimi nilipita hapo. Mlimbila namkumbuka sana... Nilikuwa namkatia pesa ili nitoroke kurudi Dar.. Alikuwa ndio anaangalia kombania yetu, akiwa chini ya afande mmoja mchaga anaitwa Ndosa.

OC Rweikaza naye alikwepo, tulikuwa tunamuita "MALAYA RWEIKAZA"; sababu alikuwa amewapitia wanaweka wote wa pale kombania. Alikuwa ni mpole, ila kwa wanawake ni balaa; na ugomvi wake ni "kuruta" ulikuwa akikukuta na mwanamke .
 
Ndo maana vijana wa sasa .
Hamtopewa nafasi kwenye ukamanda mmezidi kutoa siri
 
sintosahau mkesha wa 'usiku wa mwafrika' pale ruvu uliosimamiwa na luteni chahe akishirikiana na kapteni mhagama na akitanda
 
Reactions: Gru
Mimi nilikuwa OPERESHENI TIMIZA 1976 pale Ruvu. Nakumbika kama ni siku ya kombania yetu kupika basi siku hiyo ilikuwa pia ya kuchinja ng'ombe kama kumi hivi. Nakumbuka tulikuwa tunajongea porini kwenda kuchoma nyama tuliyoiba wakati tunaendelea kuchinja na kutayarisha nyama ya kupika ya siku hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…