Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Sanctus,

Mimi niliamua kukwepa kwenda Tabora na kuamua kwenda Oljoro kwasababu nilikuwa na kakangu mjini Arusha. Nikajua nikitoroka nitakuwa na sehemu kwa kubugia ugali.

Basi kufika Oljoro, tukamkuta afande Dauda, (sijui kama linaandikwa hivyo) alikuwa ndio mkuu wa mafunzo. Akasema mwaka jana alitoa kibali cha kuua kruta watano, akasema aligundua haikutosha, anawaamrisha maafande mwaka huu kuua kruta mpaka 15.

Kesho yake watu kibao wakatoroka na kwenda ku report kambi zingine. Isingelikuwa kuwa na brother hapo mjini na mimi ningelirudi kule Tabora usiku huo. Baada ya muda tukaja gundua kumbe Dauda ndiye alikuwa afande poa kuliko wengine wote.

Tulikuwa na afande mmoja Mhehe alikuwa anaitwa Mduda. Alikuwa anajifanya anajua jeshi kweli kweli. Akaopoa mtoto wa maana sana. Siku moja tumemaliza jeshi tuko mlimani, akaingia mlimani hall D na magwanda, kaja kufuata mtoto wake. Maskini yule msichana alikuwa terrified, akajificha. Jamaa akasubiri pale wee, mpaka akaamua kujikata. Alifikiri yale ya jeshini yanaendelea uraiani. Tulimsanifu kweli siku hiyo.

Looh! ni miaka karibu 20 toka wengine tuondoke JKT lakini naona michapo yake inakuja tu. Waswahili tungelikuwa tunaandika vitabu, tuna mengi ya kusimulia.
Oljoro na Mgulani - Operation vyama vingi 1991 - 1992.
Commanding Officer (CO), Major Miruddy (RIP)
Kombania D (Danger Coy). Mkuu wa kombania, sajenti Kinama.
Mgulani - CO, Colonel Sanga (RIP)
RSM, Warranty Officer I Kitomari (RIP).
Oljoro ilikuwa ni marufuku kula bila kachumbari. Nyanya zilikuwa kibao. Tulilima shamba 'dunia' na kuchonga tofari kwenye miamba. Tofali zilijenga nyumba za askari pale kikosini. Kuni tulifuata 'shimo la Mungu'. Mwanzo maisha yalikuwa magumu kwani tulitoka mjini. Baadae maisha yalikuwa safi mno mpaka tukanenepa. Chakula kingi, unapiga kazi mwili unajengeka. Hakuna unachowaza zaidi ya kula na kazi tu. Wasichana unawaona kama 'wanaume' wenzio tu. Matamanio hakuna kabisa. Tumeiba sana mahindi shambani kwa tajiri Lasseko na kuyakaanga bisi porini kwenye madebe. Kulenga shabaha tulitumia Semi Automatic Rifle (SAR), Sub Machine Gun (SMG) AK47, 'silaha ya msaada' Light Machine Gun (LMG), G3 na machine pistol (MP7). Wengine hizo mnaziona kwenye 'action movies' tu!
Kilimo kilivyochachamaa Oljoro 'nikatorokea' mjini Mgulani. Maisha ya mjini yakawa magumu mno. Chakula hakikuwa makini kama Oljoro! Maharage yana wadudu na ugali 'mchinjo' mpaka nilikonda! Kazi ilikuwa ni kukata michongoma mpaka unanukia 'majani'! Deal ya maana ilikuwa kwenda kwenye sherehe kufunga mahema hasa majumbani kwa VIPs. Nakumbuka mzee Kingunge alikuwa na sherehe kwake akaja kikosini kwa ajili ya mahema. Tukaambiwa twende kwake tufunge mahema kisha turudi kikosini mara moja. Kufika kwa mzee Kingunge (RIP), tukapiga kazi tukamaliza baada ya masaa machache tu. Tukaenda kumuaga mzee turudi kikosini. Mzee akatuambia tubaki kwenye sherehe tumsaidie kufanya doria wakati wa sherehe pale nyumbani. Tukapewa 'mtungi' wa kufa mtu! Sherehe ikaisha usiku wa manane mzee akaturuhusu turudi kikosini Mgulani tuko 'mchupa' mbaya! Kufika 'mlangoni' mzee MP akashtukia tuko pombe. Wacha tugaragazwe!
Haya ni machache tu! Sijuti kupitia JKT!
 
Op Vyama Vingi ilikuwa 92-93 mhenga mwenzagu, hiyo ya 91-92 nafikiri ni 30 ya Uhuru.
 
Mimi nimepita 821 KJ kwenye OP Miaka Hamsini ya JKT.Nilikua kombania F chini ya sargeant major Abednego na O.C wetu alikua Lt Ntwa (RIP) baade Lt. Sheng'oma Wakati huo C.O alikua Major Mrosso ambae alistaafu mwaka uliofuata.

Namkumbuka private mwenye visa na vituko sana anaaitwa John a.k.a Wezele Wezele ,namkumbuka matron Manento ,namkumbuka Lt. Minzi na Mwakibinga na private mnaa wa kwata kikosi kizima anaitwa Tarimo

Moments za bustani,shamba la mahindi na mkesha pale uwanja wa damu.Mbio za cross country na mazoezi ya pori na kupiga risasi bandia kule kwenye vijiji vya raia

Kikubwa kuliko vyote nakumbuka chenja aisee

Namkumbuka afande RSM Mundeba E.B[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ana mikwara ni hatari
Aisee 821 jk op miaka 50 ya muungano
Combania A ya makamanda ambari, chacha na msafiri huyo ambari ni Fundi wa kwata hatar huyo chacha mnaa hatari akichafukwa nyongo
Ha ha ha msafiri yake matusi utaskia Ku......Ku.......kumaaaaaaae foleni c.o alikua mketo na-miss moments za mabio kwata chenja askwambie mtu
 
Op miaka 50 ya jkt.......824kj kanembwa ya demo...........ego coy pale......kulikuwa na private mmoja anaitwa magesa (R.I.P) hatari saaana....mwendo n wa kuchomeka.......uelekeo American village...........muda wa kwata uso kwa uso na dakanyama(R.I.P) hilo kwata la hatariiii.........tano la kutosha kutoka kwa sirmajor kitalekwa (R.I.P) maisha yalikuwa rahaaaa!!!! Hasa kwa sie tuliokuwa ma ST!!!!!
Kurutu sifa kutimia zen nnawamwaga!!!!
Tulikuwa pamoja mkuu, ego coy.
 
Aisee 821 jk op miaka 50 ya muungano
Combania A ya makamanda ambari, chacha na msafiri huyo ambari ni Fundi wa kwata hatar huyo chacha mnaa hatari akichafukwa nyongo
Ha ha ha msafiri yake matusi utaskia Ku......Ku.......kumaaaaaaae foleni c.o alikua mketo na-miss moments za mabio kwata chenja askwambie mtu
Afande Ntwa alifariki kumbe?? Dahh

Afande mamboleo alikua mnaa balaa..

Nimemiss sana 821 KJ .. Kwa mujibu wa sheria op miaka 50
 
Op miaka 50 ya jkt.......824kj kanembwa ya demo...........ego coy pale......kulikuwa na private mmoja anaitwa magesa (R.I.P) hatari saaana....mwendo n wa kuchomeka.......uelekeo American village...........muda wa kwata uso kwa uso na dakanyama(R.I.P) hilo kwata la hatariiii.........tano la kutosha kutoka kwa sirmajor kitalekwa (R.I.P) maisha yalikuwa rahaaaa!!!! Hasa kwa sie tuliokuwa ma ST!!!!!
Kurutu sifa kutimia zen nnawamwaga!!!!
American village noma sana [emoji1][emoji1]yale matofari ya wakimbizi yalikuwa mazito si mchezo.
 
Mimi nimepita 821 KJ kwenye OP Miaka Hamsini ya JKT.Nilikua kombania F chini ya sargeant major Abednego na O.C wetu alikua Lt Ntwa (RIP) baade Lt. Sheng'oma Wakati huo C.O alikua Major Mrosso ambae alistaafu mwaka uliofuata.

Namkumbuka private mwenye visa na vituko sana anaaitwa John a.k.a Wezele Wezele ,namkumbuka matron Manento ,namkumbuka Lt. Minzi na Mwakibinga na private mnaa wa kwata kikosi kizima anaitwa Tarimo

Moments za bustani,shamba la mahindi na mkesha pale uwanja wa damu.Mbio za cross country na mazoezi ya pori na kupiga risasi bandia kule kwenye vijiji vya raia

Kikubwa kuliko vyote nakumbuka chenja aisee

Namkumbuka afande RSM Mundeba E.B[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ana mikwara ni hatari
Ww kweli ni wa Burombola
 
Back
Top Bottom