Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Mkuu tangu nitoke kule 93 sikwenda tena, ila Tanga nakwenda sema sijapata muda wa kwenda Maramba, lakini nadhani lile bwawa bado lipo
 
Acheni kabisa,nakumbuka 92-93 nilikuwa kambi ya Maramba Op Vyama vingi, CO akiwa Col Lyaruu,nilikuwa zamu nikaacha lindo langu mimi na mwenzangu SM Eradius Temba tukaenda kugonga chupa kadhaa za boha nikamix na mnazi, kumbe MP wa zamu L/Cpl Mwankenja alipata taarifa kuwa kuna baadhi ya walinzi wameacha vituo vyao na kwenda kunywa BOHA na MDAFU, siku hiyo sitasahau sekeseke nililokumbana nalo, tukiwa njiani kurejea kwenye vituo vyetu kupitia uwanja wa mpira uliokuwa karibu na kilabu cha boha wakati tunaingia kwenye shamba la mikokoa ili tuibukie hangani kubadilisha nguo ghafla tulisikia sauti simamaa!! kucheki nikamuona Mwankenja na baka lake la MP, sio siri MP alikuwa anaogopwa vibaya sana, nilijaribu kulala mbele lakini kutokana na kinywaji nilichogonga alifanikiwa kunidaka nilijaribu kujipapatua lakini ilishindikana ikabidi nijijenge tukaanza kupiga mkono yeye anapiga combat karate, mimi napiga mchanganyiko wa Shotokan, Gojoryu na Kun fu nilimpa vitu vya uso na mbavu alivyoona namzidi alipuliza filimbi kuomba msaada kwa vile eneo la mapigano halikuwa mbali na kambi, walitokea MP wawili zaidi Cpl Nyambo na Sgt Amani masharubu, aaaah! nilikula doso la hatari pigwa virungu sana na kwata mchanganyiko ikiambatana na vichura, Pushups na kukwepa ndege kufika Q/gurd niko hoi, doso likaanza upya pigwa tifu sana, MP mmoja wa kike L/Cpl Rukia akanionea huruma sana, wakati suluba ikiendelea nikamuona Eradius Temba naye akiletwa mlangoni akiwa chini ya ulinzi wa MP Sgt Sambangula, wale waliokuwa wananisulubu wakahamia kwa Temba wakaniacha ndipo yule MP wa kike Rukia aliponitoa pale kimtindo na kunipa fatiki ya kukwangua nyasi eneo la Ofisi ya MP, nikamsikia Temba akilia kama mbuzi kwa kibano alichokuwa akikipata. Nikiwa naendelea na fatiki nikamuona 2i/c OC wa kombania yangu Lt Songela akiwa na CSM Mteule Meshi wakija mlangoni mzee Songela akiwa ameshika fimbo, nilipomuona roho ikapasuka paa!! alikuwa mzee mtata sana, baada ya kufika pale alipewa maelezo na L/Cpl Mwankenja jinsi tukio lilivyokuwa, Aisee yule mzee akaanza kunishushia tena kipigo cha nguvu na ile fimbo aliokuwa nayo.
Mkuu huyu nyambo alikua sio mtu mzur kabsa,,, Mimi nilipita pale nilimkuta amekua staff sagent, anapiga virungu hatar,,,
 
Wale watu.. 834KJ Operation Tija.. Afande Mwiba.. Afande Nyeye.. Combania C
 
Ambari mzee wa kwata [emoji23][emoji23][emoji23] nakumbuka kutengeneza chokaa Na kumwagilia ziwani duuh kingine opp kikwete kunawengine bogi lilibaki walibaka sana mujibu washeria [emoji23][emoji23] yaani service man walikua wanaenda kula Serengeti wetu usiku wanavamia kama wasomali
Wesere , boya ana mikwara yule na limwili lake..[emoji23][emoji23]

Afande Ambari naye na lisauti lake!
 
Ambari mzee wa kwata [emoji23][emoji23][emoji23] nakumbuka kutengeneza chokaa Na kumwagilia ziwani duuh kingine opp kikwete kunawengine bogi lilibaki walibaka sana mujibu washeria [emoji23][emoji23] yaani service man walikua wanaenda kula Serengeti wetu usiku wanavamia kama wasomali
[emoji23][emoji23]Daah Chokaa nilibanwa gogo nusu ya kufa kisha nikala stiki za Mjerumani..

Serengeti wanakula sana mkunyenge siku ya kuhitimu.

Hivi CO mlikuta Mketo au alibadilishwa.?

RSM mtata : Mundeba daah mixer MP wa main gate Akyoo na kiherehere na mzenji.

Migazi na kuiba mapapai kule bustani 821kj sio poa .
 
Wakuu mdogo wenu hapa nimepangwa MAKUYUNI ARUSHA mwaka huu tujuzane kidogo
Maafande Hawa bado Wapo? Luten Lukinga, Rissa, mazije, Kimaro. CO bado ni major maresa? Vipi Hawa Maafande kina Kevin, Hugo, stsgt makame stsgt kajimala??
 
Operesheni Tujisahihishe, 1977, Ruvu JKT, Eagle Coy platoon 3 ya Afande Chokela. Huyu afande alikuwa akiogopwa kwa adhabu na hasira za kurekure kwao. Akakuta siku moja vitanda havijatandikwa vizuri na havipo kwenye foleni. Hivyo akatoa demo na pia adhabu kwetu makuruta akaiita kusalimia kitanda. Yaani unaweka mikono kwenye chuma kile cha kichwani na miguu yako inakuwa imekita kwenye chuma kile cha nyuma halafu unaanza kupiga push up! Sasa ole wako uwe mfupi kama alivyokuwa mwenzetu tukimuita Short, utapata taabu sana kwa Afande Chokela, maana mikono itafikia chuma cha mbele lakini miguu hata nusu ya kitanda haifiki. Short alipata shida kweli. Lakini taarifa zikamfikia Makame na adhabu hiyo ikapigwa marufuku kabisa.
 
Maafande Hawa bado Wapo? Luten Lukinga, Rissa, mazije, Kimaro. CO bado ni major maresa? Vipi Hawa Maafande kina Kevin, Hugo, stsgt makame stsgt kajimala??
afande ward, njovu, kapugi, captain nduguru, martin, na wengne weng
 
Nilipita pale ila 2017 mkuu. Sehemu saafi kabisa Operation Tanzania ya Viwanda
Wale waliopita kambi ya JKT Mlale, Operation Kujihami kiuchumi mwaka 1982/83 .... Tukutane hapa tukumbushane suruba tulizozipata na MM zilizotumika kuziepuka .... Hasa SM/SW wa B-Coy!.... Karibuni.
 
Back
Top Bottom