Mtanzania,
Mzalendo Mtanzania,
Umenichekesha sana juu ya kibali cha huyu bwana cha kuua watu . Na umenikumbusha Court Marsha moja Ruvu JKT ilimuhukumu afande moja kifungo kwa kuwa siku za nyuma alimwamuru kuruta ashike kinyesi. Jamaa alisota sana Lupango.
Du, huyu afande aliyefuatilia uraiani ndo kanimaliza sana. Hajui watu walikuwa wana namna zao za kupunguza makali ya jeshi. Kama unakumbuka ukiwa na C, unakuwa mlinzi wa Hanger.
Nakumbuka Jeshini nilibuni taaluma ya kuwa fundi wa kutengeneza vitanda vobovu mambo yanapokuwa magumu. Nilipokuwa Buhemba nikabuni kuwa Mimi ni Kocha wa Basket Ball. Jamaa wakanishtukia baada ya muda na kunipeleka Lwamkoma kulima Pamba. Ndugu yangu si mchezo, kuna mashamba yanaitwa EMBAKASI (Kwa maana ya Airport), unapewa tuta ukiwa katikati mwanzo huoni wala mwisho. Chakula mnaletewa huko huko.
Bro, nilitaka kutoroka jeshi kwa machungu. Kuna huyu afande wa Kimasai anaitwa Moreli akanidaka nilikuwa na mahindi ya kuchoma ya shamba la jeshi, alikuwa na kiboko cha kama chuma chembamba, jamaa alinipiga kama mwizi. Mkuu nilitaka nirudi home kwa miguuu nikagundua isingwezekana. Sasa hivi nikikumbuka naona raha tu. Someone should write a book of all these stories.