Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Aisee mimi nlikua nakereka na jambo moja tuuu yaan

SIKU YA JUMAATANO NI UGALI NYAMA MCHANA SASA ULE MDA WA CHAKULA ULE MNAAMBIWA KURUTI UELEKEO KUZIMA MOTOO

Wale jamaaa sijui walikua wanawasha moto makusudi duuh[emoji119][emoji119][emoji119][emoji119]yan ikifika jtano mzee kinanuka unakuta pori linateketea mzee

824Kj hioo[emoji119][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119]
841Kj kila ukifika mda wa kula siku ya nyama ni bigula la moto,unaambiwa moto unaunguza misitu ya sao hill
 
Bila kusahau ulikuwa unapewa ''warrant'' ili utumie kusafiri kwenda, na pia wakati wa kurudi.
Mimi warrant nikiitumia wakati wa bogi from Msange CTS (central training school zilikua nane tu enzi hizo) kwenda Luwa kambi ya mkoa. Kutoka Luwa kurudi uraiani walinipa cash money.
Nikapanda TRC bus kutoka S'wanga mpaka Mbeya. 12 hours.
Kutoka Mbeya Sasa ndio enzi zile Scandinavia Zina Anza Anza. Bus refu mlango wa abiria katikati. Enzi hizo hakuna tochi, Wala gavana Wala trafiki maana safari Ni usiku.
Mby Kuna madereva aisee. Hii route ya Arusha Dar Ni wanafunzi Tena wa VETA. Wazee waliotoka usafirishaji wako route ya mby Dar.
Hatahuku kwa wasukuma Mwanza hakuna madereva wa mabasi.
Toka mby jioni kumi na moja alfajiri tuko mnazi mmoja. (Stendi kuu enzi hizo) kwa mabasi ya mby songea TANGA na Iringa.
Usweken stend zao zilikua kariakoo. Moshi na Lindi mtwara na mafia Ni kisutu.
 
Kuamka saa 10 usiku na kuanza mchakamchaka pale Ruvu. Kuna Maafande mfano Issa Machibya(RC Mstaafu), Afande Kijanga, Afande Londo, Afande Agnes, Afande Mmari walikuwa noma sana tukiwa kwenye OPERATION TIMIZA.
 
Jasho mzinguaji [emoji3], commando kipingu wa Charlie coy unamkumbuka? Madoso miyeyusho? Koplo Rambo wa Danger? Mkorofi daily analala mahabusu, matron kikosi je?
[emoji3]

Capt Moshi miyeyusho sana
Daaaah we jamaa hao makatili, Rambo alishanipiga Kofi kwenye kwata mzeee[emoji23][emoji23]

Palikuwepo na Afande Devi, Afande Namwao

Ila Cpt Moshi amefariki mwaka Jana mkuu
 
841Kj kila ukifika mda wa kula siku ya nyama ni bigula la moto,unaambiwa moto unaunguza misitu ya sao hill
Nawe ulikuwa unaenda kumbe.

Kuna siku ikitokea tifu kati ya service mens na kurutas kisa kuanzisha moto nyakati za usiku
 
Daaaah we jamaa hao makatili, Rambo alishanipiga Kofi kwenye kwata mzeee[emoji23][emoji23]

Palikuwepo na Afande Devi, Afande Namwao

Ila Cpt Moshi amefariki mwaka Jana mkuu
Rambo mtata yule mzee, halafu amekomaa kisela yani yule mwamba.

Capt Moshi alifariki kumbe dah! Apumzike kwa amani aisee..

Alipatwa na nini? Mbona umri ulikua bado kabisa dah
 
Kulikuwa na ile issue ya kwenda pukucha mahindi kule kwenye ghala lao wakati wa usiku aiseee ilikuwa ni nouma unapigwa na baridi Hadi mikono inshindwa pukucha mahindi
 
Rambo mtata yule mzee, halafu amekomaa kisela yani yule mwamba.

Capt Moshi alifariki kumbe dah! Apumzike kwa amani aisee..

Alipatwa na nini? Mbona umri ulikua bado kabisa dah
Nasikia kurogana kaka kisa madaraka mkuu.

Rambo ulikuwa ukitaka umuweze muungishe biashara yake tu[emoji23][emoji23]
 
Rambo mtata yule mzee, halafu amekomaa kisela yani yule mwamba.

Capt Moshi alifariki kumbe dah! Apumzike kwa amani aisee..

Alipatwa na nini? Mbona umri ulikua bado kabisa dah
Unamkumbuka Afande Shitindi wa B coy, afande Urassa wa kwetu A coy, Mwizarubi, Cpt Runje, Cpt Shehoza
 
Kuamka saa 10 usiku na kuanza mchakamchaka pale Ruvu. Kuna Maafande mfano Issa Machibya(RC Mstaafu), Afande Kijanga, Afande Londo, Afande Agnes, Afande Mmari walikuwa noma sana tukiwa kwenye OPERATION TIMIZA.
Huyo RC mstaafu Issa Machibya nimesoma na mwanae shule Moja advance alikuwa mkorofi naye alikuwa anaitwa Issa Machibya Jr.
 
Alikuwepo mmoja Msange CTS miaka ya mid 80s.
Kila siku anaingia Serengeti kiuchawi na kubaka wasichana.
Kumbuka kipindi kile wasichana mbele ya maafande Ni Kama maharage ya Mbeya. Jinga kulikua linabaka kiuchawi
[emoji23][emoji23][emoji23]simpati mkuu
 
Back
Top Bottom