Je unakumbuka ulipokua shule ulikua na cheo gani? Na faida ya hicho cheo ni ipi?

O level kipindi nipo form two nilichaguliwa na HM kuwa mgonga kengele,faida niliyo ipata nikuwahi shule mapema

Form three nikajiuzulu baada ya head master kwenda masomoni.

A level na chuo sikuwa na uongozi wowote
 
Wanafeligi sana sijui kwanini asee,
Kuna jamaa A-level alikua nabii kabisa
Ila tokeo sasa.
 
Hii tabia ya monitor kuwachapa wapiga kelele nilikutananayo huko kanda ya ziwa nikiwa primary nilikuwa nashangaa sana, mwanafunzi anamchapaje mwanafunzi mwenzie!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanafeligi sana sijui kwanini asee,
Kuna jamaa A-level alikua nabii kabisa
Ila tokeo sasa.
Praise and worship haijawahi kuleta akili kichwani. Kazi kupiga vyombo vya mziki na kukesha uko eti wanalinda vyombo. Sometimes kuzurula kwenye matamasha na makongamano ya imani. Mkifunga watu wanaenda kukata mapindi wale watumishi wanaenda kwenye kambi za kuhubiri. Unajua kupenda kitonga kwa wachungaji kunatokea uku
 
PRIMARY.
Std la 5 - 7, taaluma na maktaba.
Faida.
Nilkua nasimamia masuala yote ya taaluma upande wa wanafunzi, pia kuazima wanafunzi vitabu. Kuwa na amri au mamlaka fulani kwa wanafunzi..

SECONDARY.
O LEVEL.
4m 1 - 2, usafi na mazingira.
Faida.
Kusimamia masuala ya usafi na mazingira na mandhari kwa ujumla ktk shule. Kuwa na amri au mamlaka fulani kwa wanafunzi, Kuheshimiwa.
4m 3, Nidhamu na malezi.
Faida.
Kusuluhisha migogoro baina ya wanafunzi, kusimamia maadili na nidhamu kwa wanafunzi, Kuheshimiwa.

A LEVEL.
Nidhamu na malezi.
Faida.
Kusuluhisha migogoro baina ya wanafunzi, kusimamia maadili na nidhamu kwa wanafunzi, kuheshimiwa.

CHUO.
Hakuna..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…