Je, unamfahamu mnyama anayeitwa Nyegere/Honey Badger? Mnyama mwenye wivu kupindukia

Ila nilisikia kuwa eti ukimpiga na ubua au kuni kavu kabisa anakufa au anakimbia na kukuacha uendelee na safari yako
 
1.Ni mnyama mdogo anayekula nyoka, kenge, majani, matunda, kenge, mizoga ya binadamu, chui, simba, duma, ndege n.k...kwa kifupi anakula kila kitu
Huyu kama angepewa ukubwa hata wa mbwa tu,ingekuwa kazi.😀
 
MJUE NYEGERE MNYAMA MWENYE WIVU KUPINDUKIA!!!!

Nyegere ni moja kati ya wanyama wenye wivu sana hapa duniani. Chakula chake kikubwa ni asali,yeye hupanda juu ya mzinga wa asali na kuujambia, baada ya mashuzi yake nyuki wote hulewa na yeye kupakua asali na masega yake na kula. Mwili wake una ngozi ngumu sana kiasi hata nyuki akimuuma hakuna chochote kinatokea

Nyegere ni mnyama mwenye wivu na mapenzi makubwa sana kwa jike lake, hutembea nyuma ya jike huku akiwa ameziba sehemu za siri za jike, hata jani tu likiigusa sehemu ya siri ya jike litararuliwa na kupokea kichapo cha hatari,maana wivu wake ni kuwa jani laitakuwa "limefaidi utamu" wa jike

Nyegere anaweza kununua ugomvi mpaka kijiji cha sita, walina asali ndio waathirika wakubwa wa hasira za Nyegere,anaweza kuujambia mzinga akala kidogo asali na kupeleka kwa mke,mlina asali akifika na kupakua, nyegere ana uwezo ya kufuatilia harufu ya aliyeiba asali yake mpaka nyumbani, na akifika anavunja mlango na kuingia ndani na kumvamia mwizi wa asali yake(ukizingatia milango ya vijijini si imara). Watu wengi vijini wameuwawa kwa namna hii.

Nyegere ndio mmoja kati ya "fearless animal" duniani, huweza kuwakabili Simba na Chui zaidi ya mmoja na kuwashinda,anasaidiwa na ngozi yake ngumu na kucha zake, awapo katika hatari ya kushambuliwa hukakamaa na ngozi yake kuwa ngumu kama "defensive mechanism" yake.

Kuna makabila ambayo waganga wa kienyeji hutumia mchanganyiko wa Nyegere kutengenezea limbwata,Yaani wamama huchukua dawa hiyo kuwawekea waume zao ili wawe na "upendo" wa Nyegere.

Wivu wa Nyegere hufanya awachukie sana binadamu wanaume,mwanaume ukiwa porini ukakutana na Nyegere akiwa na jike lake jiandae kupata kibano, huona wivu kuwa utamtamani jike,hivyo hukimbilia kumvamia mwanaume sehemu za siri akiamini ndizo zinazokupa jeuri ya kumtamani jike lake.

Nyegere hula nyoka wa aina yoyote,ana sumu kali ambayo akimng'ata nyoka wa aina yoyote haponi.

Ogopa sana kukutana na mnyama mwenye wivu Nyegere...
 
Kiongozi nadhani hapa unammaanisha 'honey badger' ni kweli ni fearless animal lakini umegawa chai sana humu ndani mfano.

1: Yeye hajambii mzinga ni anaingia na kuanza kula huku nyuki wapo humo humo.

2: Hana ngozi ngumu na wala haikakamai ila ngozi yake ni nene hivyo hata mikuki na meno ya nyoka yanashindwa kutoboa na kufanya any fatal damage, kwa nyoka kama 'puff ader' ambao wana meno marefu hawa nyegere miili yao inaruhusu kudevelop antivenom within a short time hata kipind ambacho nyoka anashambulia.

3: Chui na simba wanashindwana nae kutokana na swala la ngozi, yaani kipindi umembana tumboni yeye ngozi yake inamruhusu kugeuka 180 degrees na akafanya fatal damage.

4: Hachukii binadamu wanaume ila wanyama ni territorial akikuona eneo lake lazima mtagombana lakini pia urefu wa huyu mnyama kwenda juu na ukali wa kucha zake ndiyo unafanya alenge pumbu pekee na si sehemu nyingine.

Nyegere mwenyewe huyu hapa.

 
Ukikaona kwa picha unakadharau
Sikuwahi kusikia sifa zake
Ahsanteni sanaaaaa
 
Nyegere hana sumu sema hata kama nyoka mwenye sumu akibahatika kumtia sumu huwa inamdhuru kwa muda mfupi halafu anazinduka anaendelea.
 
Ha ha ha ha ha kweli JF kiboko....Nimecheka sana,kwamba hicho kijamaa hata jani likigusa Ikulu tu ya mkewe ni mtiti mzito!!ha ha ha ha Nyegere uje huku kumbe ndio tabia zako
Hivi nyegere ndo kicheche?
 
Mkuu hii ilishaletwa humu kitamboo....Mleta mada yupo hapa
 

Nimecheka sana. kumbe funzo jiamini na ulicho nacho bila kujali udhaifu wako. Du!!! anapambana na simba kadhaa bila kushindwa. Lakini Binadamu na simba tunatoka mbio!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…