Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane hapa

Hatuwezi kulima matikiti "ORGANICALLY"? Yaani kulima bila kutumia mbolea za viwandani? Kwani najua kuna wanunuzi wengine na wengipia hawapaendi mazao yanayotokana na hizi mbolea za viwandani. Naomba ushauri kwa msingihuo = wa kulima bila kutumia mbolea za viwandani. Natanguliza asante zangu.
 
@kilimomaarifa.tajiri na ndugu @NINA IMANI kuna kitu nadhani tunachamganya hapa!! Je unamwagilia masaa 24 maji kiasi gani??? milimiter ngapi za maji??? Je @NINA IMANI unatumia drip irrigation au????

NB: KAMA UNATUMIA FURROW IRRIGATION (UMWAGILIAJI KWA KUTUMIA MFEREJI) SIKUSHAURI UMWAGILIE KWA MFEREJI KWA MASAA 24!!!
 
mwanao akimaliza form 4 mzazi mnunulie simu au laptop awe anaperuzi jamii forums, kuna elimu ya kivitendo inayoendana mazingira ya kitanzania ya sasa hivi, hizi elimu za college na university pamoja na ajira ngumu naona kunampotezea muda mwanao.....anamaliza na miaka 25 alafu ndio anaanza maisha kutoka 0
 
Mkuu Kilimo.maarifa, asante sana kwa darasa suri.

Je, kwa Dar es salaam ni duka gani lenye kuuza mbolea za kuaminika (zisizo fake) ?

Happy New Year.
 

Asante sana mkuu kwa majibu yako mazuri nitafuatilia.

Naomba vile vile kama kuna wadau wamewahi kununua MBOLEA au MADAWA ya mimea ya kuaminika jijini Dar wajitokeze.

Asante kwa msaada.
 
Habari kaka mimi Ni Mkulima ila cjawa mzoefu ndio kwanza nataka kuanza kutokana na darasa hili linalo endelea ...nitaanza na eneo Dogo tu la robo eka 1000m² ....nasari tayari nimeshataarisha ..kutokana na ugumu wa upatikanaji wa mbegu nimeamua kutumia mbegu ya Tanya ...na nasari nilitaarisha tarehe 26/12/2015... Na tarajia January kupandikiza ...mbolea nitakayo tumia Ni ya samadi mavi ya mbuzi pamoja na ngombe ....sasa kidogo Nina swali ??
#Je mbegu niliotumia kwa kipindi hiki Ni sahihi???
#Ardhi yangu INA matatizo ya nematode japo c kwa kiwango kikubwa nini nifanye????
#then vp naweza kujikinga na wilt sababu wakulima wengi wanakilio hiki..
Heshima kwako.
 
Heri ya mwaka mpya kilimomaarifa.tajiri...hali ya Nyanya zangu imezidi kuwa worse zile nilizokuwa nimeanza kuchuma zimezidi kukauka kilichobaki Ni kung'oa na kuchoma Kama ulivyosuggest. Zile ndogo naona kwa mbaali vimajani vinaanza kuwa brown ingawa nilizipiga dawa ya wadudu na ukungu toka ziko kitaluni na nikarudia tena baada ya kuhamisha!
 

SHUKARNI SANA,
 
NAOMBA KUULIZA,JE FORT SULOTASTE 19-19-19+Mg0 na Mult K 19-19-19 zinafanya kazi sawa kwenye nyanya, au ipi yenye ubora zaidi. Asante.
 
Asante Sana kilimomaarifa.tajiri kwa kweli umepatia Sana utakuwa Ni mnyauko maana ulienda kwa viportion Tu na Nyanya zimekauka zikiwa na matunda take mengi! Hizi ndogo vimajani vinaanza kuwa brown ya rangi ya udongo Si kijani, ujue hats hizi zilizokauka zilianza kwa style hii! Chokaa kupata ndio changamoto sasa duh!
 
DAH KWELI MIMI NAFUATILIA UZI, JAMAA ANAJIBU SWALI MOJA HATA MARA 10 NA WALA HACHOKI, MOYO WA AJABU SANA HUU
 
Yah!! Darasa La NGUVU Mno Mkuu, Asante Kwa Elimu!! Hapa Ndio Nauona Umuhimu Wa Kuwa Na ARDHI Ya Kutosha!!!! ARDHI Ndio Mtaji Mkuu!!!!
 
Mkuu nakushukuru sana. Sasa nimeenda KIBO Moshi kutafuta Yara miller winner imewaishia. Ila nimekuta wana NPK CEREAL 23-10-5+35 2MGO+0.3ZN ambayo wameshauri ni nzuri pia. Nataka kuotesha naweza uteshea hii then baadae winner ikija niendelee nayo mkuu?
 
Asante sana sana, je mult k au polyfeed natakiwa kuweka vijiko vingapi kwenye maji ya lita 20 ninapotaka kupiga? Maana vipimo vya gramu vinanisumbua. Asante.
 
shukrani kwa elimu unayoitoa mkuu, nimefuatilia na kuchukua notice uzi mzima,
mimi nataka kuanza kulima mwezi wa 5,nikipiga hesabu zitakua zina matunda kuanzia mwezi wa 8 hadi wa 10,

kwanza ningependa kujua changamoto za soko kwa sisi tunaoanza zikoje na unawezaje kuziepuka kwa kua wewe una experiece sana soko unalielewa

pili umesema nyanya tokea ipandwe inachukua miezi 3-5 kuanza kuvunwa, je hili gepu la muda wa miezi miwili linatokana na nini? ni msimu, utunzaji au aina ya mbegu? shukrani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…