Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane hapa

Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane hapa

Mkuu Hizi Nyanya Kipato F1 Nitachuma Kila Baada Ya Wiki Moja Ndio Nauliza Naweza Chuma Hivyo Kwa Muda Gani Ni Kweli Inaweza Fika Miezi 6? Au Wewe Ulivyosema Michumo 3-5 Umemahanisha Miezi 3 Hadi 5? Naulizia Kuanzia Siku Ya Kwanza Kuchuma
 
Mkuu Ahsante Nimepiga Finisher Leo Maana Matunda Yanakaribia Kukomaa,na Nyanya Zina Maua Sana Ila Kulikuwa Na Tatizo La Maji Kutotosheleza Hivyo Matunda Yalianza Kuoza Vitako Machache Nikawaambia Wafanyakazi Waongeze Maji Na Nikaweka CAN,kufuatia Ushaur Wako Kuwa Huzuia Kuoza Kitako.

Ila Pia Baadhi Ya Mistari Ilikuwa Na Matawi Madogo Ila Saivi Nimeona Kuna Changes Sasa Nitaka Kujua Je Tatizo Hilo La Uchache Wa Maji Linaweza Kuathiri Muda Wa Uchumaji Wa Nyanya?

Kwa Maana Ya Kuchuma Kwa Muda Mfupi? Au Baada Ya Kurekebisha Utiaji Wa Maji Hakutakuwa Na Tatizo Lenye Kuathiri Mfumo Mzima?
 
KIONGOZI
NTAKUELEZA ZAIDI KATIKA MATIKITI MAANA NIKO NA UZOEFU NAYO

KAMA MAZAO YOTE YANATAMBAA SI VIZURI SANA UKICHANGANYA

TIKITI,

UDONGO NA JOTO


Usiwe wa kutuamisha maji
Ukiwa Tifutifu, AU kichanga Tifutifu (Clay loam) na hali ya joto kiasi angalau 15- 35 degree inatosha sana
Linahitaji maji mengi mwanzoni lakini kadri linavyoendelea maji unapaswa kupunguza


MUDA WA KUOTA


Ukisia mbegu huchukua siku 5 hadi 10 kuota


KAMA SHAMBA LIKO TAYARI BY NOW, UKIPANDA SIKU 75 HADI 90 (AINA ZA MBEGU ZILIZOPO SOKONI KWA SASA NI HYBRID -ZEBRA, 1. SUKARI F1, 2. MSHINDI, 3. JULIANA ETC) UNAVUNA TIKITI KWA HIYO UNAMIEZI 3, OKT, NOV NA DEC WAKATI TUNAKABIA MWAKA MPYA UNAVUNA.


KWA TIKITI JITAHIDI SANA KUPANDA KWA NAFASI


KAMA UTALIMA MATUTA BASI TUTA LIWE LIMEINUKA KIASI KUJA JUU WALAU SM 20 HIVI LIWE NA UPANA WALAU WA SM 45 HADI 60, UPANDAJI, KUTOKA SHIMO HADI SHIMO SM 90 HADI 100, NA KUTOKA KATIKATI YA TUTA HADI TUTA LINGINE NI MITA 1.5=SM 150, KWA HIYO KWA MATUTA YANAYOFUATANA TIKITI ZIIKIANZA KUTAMBAAA UNAZILAZA ZINAKUTANA KATIKATI YA HIZO TUTA MBILI


KAMA UTAAMUA KUPANDA KWA MAJARUBA KAMA HAYA YA MPUNGA, AMBAPO WATU WENGI HUMWAGIA KWA KUTENGENEZA MITALO YA KIENYEJI YA UMWAGILIAJI BASI, JARUBA LAKO LINAPASWA KUWA NA UPANA WA MITA 3 NA UREFU WOWOTE ULE HATA WA MITA 5 ILI MRADI UWEZE KUMUDU KUINGIZA MAJI.


SASA KWA JARUBA TUNAPANDA PEMBENI KATIKA ANGLE HIZO. KUTOKA SHIMO HADI SHIMO NI HIZO SM 90 (=futi tatu), AMBAPO SASA YAKIAANZA KUTAMBAA UTAYALAZIA KATIKATI HAPO KATIKA HUO UPANA WA MITA 3, SO YA KULIA YATAKUJA HAPO CENTRE, YA KUSHOTO , KASK, NA KUSINI HIVYO HIVYO YANAKUJA KULALA HAPO


MBOLEA ZA KUPANDIA NI MUHIMU SANA


UKIPATA YARA MILA WINNER ( NAMBA HIZI 15:9;20 AINA YA NPK) ITAKUFAA KILA SHIMO UNALOWEKA MBEGU MOJA WEKA GRAMA 10 YA MBOLEA SWA NA KIJIKO KIMOJA KIKUBWA CHA WALI. ZITAOTA BADA YA SIKU 5 HADI 10


AFTER ONE MONTH, UTAWEKA MBOLEA YA KUKUZIA KAMA CAN AU UREA


MAUA YAKIJA JITAHIDI UPATE BOOSTER (HIZO NI MAALUMU KWA AJIRI YA MAUA NA MATUNDA


ZIPO BOOSTER ZINAITWA STAARTER- MFANO HALISI ZILIZOPO MADUKANI NI POLYFEED STARTER-HIZO HUTUMIKA KUPIGA MAUA WAKATI WA MAUA


MATUNDA YAKIJA UTAWEKA POLYFEED FINISHER-HIYO NI KUIMARAISHA MATUNDA, NA PIA UTAFUTE MBOLEA INAITWA YARA NITRABOR (HII INA Calcium na Nitrojen kwa wingi) , husaidia kuzuia tikiti kunyauka, na kuzoa katika kitako-Ugonjwa unaitwa Blosom End Rot

WAKATI WOOTE WA MAISHA YA TIKITI USISAHAU DAWA ZA WADUDU, WANAOKATA MAUA , NA KUTOBOA MATUNDA, DAWA KAMA DUDU ALL AU SELECRON, AU MATCH, AU KARATE MOJA WAPO YATOSHA KUMALIZA WADUDU


LAKINI WAKATI WA KUPIGA HIZI DAWA KUWA MAKINI SANA USIPIGE MCHANA, UTAUWA NYUKI WA KUFANYA UCHAVUSHAJI KUTOFANYIKA-HAPO UTAPATA DIFORMALITIES NYINGI SANA KAMA SHAPELESS KATIKA MATUNDA, PIGA ASUBUHI SANA AU JIONI SANAA,




PIA KAMA UTAONA KUNA HALI YA UKUNGU (UNYEVU NI MWINGI AU BARIDI USIKU AU MCHANA) NI MUHIMU KUWEKA DAWA ZA JAMII YA COPPER, KAMA BLUEE COPPER, AU EBONY KUZUIA UKUNGU,


NI MUHIMU SANA KUHAKIKISHA TIKITIKI ZAKO ZINAPATA MAJI WALAU MARA 3 KWA WIKI, ILI KUPUNGUZA WATER SRESS


GHARAMA ZA MBEGU

KWA EKARI MOJA UTAHITAJI Gram 300 za mbegu , ambapo jumla ya gharama za mbegu ni kati ya tsh 200,000 hadi tsh 300,000

MAVUNO

Kwa kuwa kwa nafasi tajwa hapo juu utakuwa na mashimo yasiyopungua katiya 2000 hadi 3000 Kwa ekari moja. Hivyo kila shimo au kila kamba ya tikiti ikikupa matikiti matatu means utakuwa na mavuno ya vichwa vya tikititi kati ya 6000 hadi 9000, ambayo ni sawa na wastani wa tani 12 hadi 18 kwa ekari moja

Karibu Kiongozi

Hayo matikiti yanayo chukua miezi 3 nimbegu gani mbona naona kila unachosema kipo tofauti nasisi tunavyolima
 
Kuna watu wanasema eti ukitaka kupata mavuno mengi kwenye viazi au zao lolote pandia mbolea aina ya sa, wanasema mbolea hiyo ina nguvu kuliko dap ila inaharibu ardhi je mkuu ni kweli?
 
Mkuu Kuna Tofauti Ya Kiasi Cha Mbolea Inayowekwa Kwenye Mmea(nyanya) Wakati Wa Kupanda Kukuzia Au Wakati Zina Matunda? Nimekuwa Nikitumia Kizibo Cha Chupa Ya Soda Muda Wote Je Ni Sahihi? Uliposema Muda Wa Maua Matunda Au Ukianza Kuvuna Mmea Unatakiwa Ushibe Na Uwe Na Lishe Ya Kutosha Ulimaanisha Nn?
 
Hongera sana mkuu,na asante sana kwa elimu yaani umeeleza kama mkazi wa njombe,mimi ni mwenyeji wa njombe kijiji cha uwemba ,kiukweli nimeelimika kwani kutokana na kusikia kuwa mbolea ya sa inaleta pato kubwa nami nilipanga msimu wa kilimo mwakani nitumie hiyo mbolea kumbe hao wanao ongea hawajui upande wa pili wa mbolea hiyo. Asante sana mkuu ubarikiwe.
 
Mkuu Ahsante Kwa Elimu,naomba Kujuzwa;nyanya Zilianza Vitumba Napuliza Starter,maua Napuliza Mult K(busta Ya Maua) Na Zikianza Matunda Napuliza Finisher,sasa Je Ni Sahihi Nikifanya Hivi,zikianza Vitumba Napuliza Starter,zikianza Maua Nachanganya Starter Na Mult K Na Zikianza Matunda Napiga Zote Tatu Ya Starter,mult K Na Finisher? Halafu Pia Ni Sahihi Kuwa Nachanganya Busta Dawa Za Wadudu Za Ukungu Na Supergro Wakati Wa Kupuliza? Na Mwisho Naomba Kujua Umuhimu Wa Kitaalamu Wa Hii Super Gro.Ahsante Mkuu
 
mkuu ningependa kujua ipi mbegu bora ya nyanya ambayo ikipandwa nje ya greenhouse pia hufanya vizuri zaidi kuliko nyingine? kati ya kipato, assira na Eden au hata na nyingine.... mana naamin lazima zitakua zina ubora tofauti kimavuno ..
 
Ok Ahsante,sasa Mkuu Nafanyaje Ikiwa Nyanya Zina Matunda Na At The Same Time Zinatoa Maua Na Zinaendelea Kuchipuza Na Kutoa Vitumba Nipulize Busta gan Na Mbolea Ya Kuweka Ni CAN pekee?
 
Naomba kuuliza mbolea aina ya npk inasaidia nini katika kukuzia, kwa sababu kuna mkulima wa nyanya kaniambia kuwa yeye huwa anapandia dap,anakuzia can nyanya zikiwa na wiki 2 tangu kupandikiza na zikiwa na wiki nne anakuzia npk. Asante.
 
Asante,kwa hiyo mara ya kwanza kwenye nyanya utakuzia mbolea aina ya can na mara ya pili utakuzia can tena?
 
Utofauti wa mavuno ya nyanya utakuweje nikikuzia can mara mbili na nikikuzia can kisha npk? Asante.
 
Mkuu Aman Iwe Juu Yako,naomba Kujua Umuhimu Wa Kuondoa Majani Chakavu Na Matawi Yanayogusa Chini Kwenye Nyanya.Pia Naomba Kujua Dawa Za Ukungu,wadudu Na Busta Zinapulizwa Kila Baada Ya Siku Ngapi Kitaalam Kwenye Nyanya? Na Mbolea Nayo Kama Umeweka Ya Kukuzia Inatakiwa Ukae Siku Ngapi Uweke Nyingine?
 
Nataka kununua yara miller winner kwa ajili ya kupandikizia nyanya,je hiyo yara miller winner ya kupandia nyanya haina makundi ya namba,kwani naogopa nisije nunua ambayo sio sahihi na muuzaji akaniuzia ambayo sio kama ulivyosema mbolea ya npk ina makundi. Asante.
 
Asante sana kwa maelezo mazuri,naomba kuuliza tena. Je kati ya hizi booster ipi ni bora kushinda zote.mult k,vitimax ,makromix ,polyfeed starter na finisher
 
kilimo maarifa uko vizuri sana mkuu, duuuh mungu akubariki sana, ebu weka namba yako hapa nikutumie japo kipesa cha muda wako na kiinternet unachotumia, tungekuwa na watu 100 tu kama wewe nchi ingekuwa mbali sana hii hii. hongera sana.
 
Back
Top Bottom