Chukwu emeka
JF-Expert Member
- Jan 12, 2018
- 24,314
- 38,919
Kumbe ni rahisi hivi mkuu,weekend hii nitajaribu.........Kwa wali unachemsha maji pamoja na nazi yakichemka unaweka mchele + chumvi then unapika kwa moto mdogo had vikiiva tayari kwa kula
Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio hayo hayo my dear sema saa nyingine wakati unalichemsha lile tui zito pembeni unaweza kuweka binzari ile ya njano mpauko ndio inanoga sema sharti lake lile tui usiache kulikoroga mpaka lichemke kwani ukiliacha linakuwa kama maziwa mgando. (Linakatika)
Unachemsha maharage yakishaiva unayamimina kwenye chombo pembeni. Kisha kwenye ile sufuria uliyochemshia maharage unaweka lile tui la pili sema inabidi liwe chache ili maharage yasiogelee kisha unalichemsha kwa kuweka kitunguu maji na chumvi likishachemka unamimina maharage yako yakishakauka unayaepua baadae sasa ukikaribia kula ndio unalimwagia juu lile tui zito ulilolichemsha peke yake.
Na hii unaweza kufanya hata kwenye mbaazi mbichi pia.
Yeah very simpo,em jaribu then uje kuleta mrejeshoKumbe ni rahisi hivi mkuu,weekend hii nitajaribu.........
Sawa,kesho nitafanya hii assignment.....then nitasubmitt kwako mwalimu
Yaani nilisemea kuyamimina kwenye bakuli ni ile saa ambayo sufuria uliyochemshia maharage unatumia kuchemshia lile tui la pili na kitunguu maji na chumvi kisha hayo maharage unayatoa kwenye bakuli na unayamiminia mule mwenye tui ambapo yanachemka pamoja mpaka lile tui likauke kisha unashusha chini.[emoji39][emoji39][emoji39] haya mapishi mapya ntayajaribu...kwahyo nikishapakua kwenye kibakuli maharage wakati wa kula ndo namimina hlo tui au nalimiminia kwenye sufuria nliyoungia maharage?
Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo naona kuna viazi vitamu....navyo wanapikiaje nazi? maana sijawah kuona nmezoea mihogo tuHabarini Wakuu. Leo nataka tupeane mawili matatu ya namna ya kupika kwa kutumia nazi hapa haijalishi nazi iwe ni ile ya kukuna mwenyewe au zile zinazouzwa madukani.
- Je unaandaa tui lako katika sehemu ngapi?
- Au hata kama ni zile tui za kununua madukani unapikaje pikaje au unaliweka kwenye upishi wako wakati gani?
- Je unaungaje wewe mpaka kikawa tayari hicho chakula chako cha nazi?
-Unatanguliza nini kisha unamalizia na nini?
- Pia unaweka nini na nini kwenye huo upishi wako ambao ndani yake unaweka nazi?
Mfano: Mimi nikitaka kupika maharage ya nazi huwa naandaa tui langu katika makundi mawili moja lile zito na lingine la kawaida tu ila chache.
Basi nikishayachemsha na maji yakaiva hayo maharage huwa nakatia kitunguu maji kikishachemkia na maji na kuweka maji kidoogo, yakikauka huwa naweka lile tui la pili ambalo wakati wa kuchuja lilikuwa la kwanza nakoroga kisha naweka chumvi ya saizi yangu baada ya hapo namalizia lile tui la nazi la mwanzo ambalo hapa huwa la mwisho kisha naliacha lichemke kidogo baada ya hapo maharage yanakuwa tayari kwa kuliwa.
Haya wenzangu mnapikaje iwe ni
- Maandazi
- Ubwabwa
- Mboga za majani
- Mchuzi wa samaki
- Dagaa wa nazi
- Njegere
- Makande
- Ndizi
- Viazi vitamu
- Visheti
- Mkate wa Mchele
- Mihogo
- Magimbi
- Maharage
Yaani chakula chochote kile ilimradi ndani yake unaweka nazi.
KARIBUNI TUBADILISHANE UJUZI.
Hahahahaaa ndo uweke kambi hapa upate maujuzi kama ni mpenz wa mapishi laknHahaha naona malue lue tu mtani
Maana nachojua pika ni chai na uji
Basi mi nimezoweaga vibaya yaani ubwabwa wangu wa nazi mpaka ukishakauka niweke lile tui zito hapo ndio naona nazi inakolea.Kwa wali unachemsha maji pamoja na nazi yakichemka unaweka mchele + chumvi then unapika kwa moto mdogo had vikiiva tayari kwa kula
Sent using Jamii Forums mobile app
GoodSawa,kesho nitafanya hii assignment.....then nitasubmitt kwako mwalimu
Aah hapo nmekuelewa vema,asante sana nikijaribu yakitoka bomba ntakupa mrejeshoYaani nilisemea kuyamimina kwenye bakuli ni ile saa ambayo sufuria uliyochemshia maharage unatumia kuchemshia lile tui la pili na kitunguu maji na chumvi kisha hayo maharage unayatoa kwenye bakuli na unayamiminia mule mwenye tui ambapo yanachemka pamoja mpaka lile tui likauke kisha unashusha chini.
Baadae ukishachemsha lile tui zito kwenye sufuria nyingine pembeni nalo likishaiva unalishusha hivyo zinakuwa sufuria mbili.
Saa ya kutaka kupakua ndio lile tui zito unalimimina juu ya yale maharage yakiwa mule mule kwenye ile sufuria yake. Huyatoi.
Basi mi nimezoweaga vibaya yaani ubwabwa wangu wa nazi mpaka ukishakauka niweke lile tui zito hapo ndio naona nazi inakolea.
Hivyo tui lile la kawaida huwa nalikadiria lisiwe lenye kuivisha ubwabwa mpaka ukatota yaani naacha kiini kigumu kidogo ili nikiweka tui zito dkk ngapi tu nafunikia kiive.
Ngoja wamalize kabisa,bado dk 4 za nyongeza tupo mbele 1-0Hahahaaa. Letaga updates kule kwenye uzi wetu mana leo niko mbali kidogo.
Vile mimi nikipika huwa nikishavimenya navikata kata halafu naweka kwenye sufuria na kuvibandika jikoni kisha naweka maji kiasi ili vianze kuiva lengo baadae muda wa kuchuja nazi nichuje chache ili vikolee nazi navichemsha viazi huku nimeweka tui mbili kama kawaida vikishaanza kuiva kama maji yalikuwa mengi nayapunguza kisha natia tui lile la kawaida na chumvi kidogo baada ya lile tui kukauka naweka lile zito likishachemka kidogo nashusha na hapo vinakuwa tayari kwa kuliwa. Hivyo tu mwaya.Hapo naona kuna viazi vitamu....navyo wanapikiaje nazi? maana sijawah kuona nmezoea mihogo tu
Hua navipika kwa kuvichemsha then vikichemka naweka mafuta + carrots nakwangua+ vitunguu+chumvi then navipika kwa moto wa wastani had vikiiva vzuri....kwa nazi unapikaje
Sent using Jamii Forums mobile app
Karibu my dear.Aah hapo nmekuelewa vema,asante sana nikijaribu yakitoka bomba ntakupa mrejesho
Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo kikubwa ni kukadiria lile tui la mwanzo basi yaani inatakiwa ukishaweka mchele mpaka likikauka ubwabwa uwe na kiini kigumu kidogo ili ukiweka lile tui zito ndio kiini kinakuwa cha saizi.Mmh hapo lazima wali utoke umekolea nazi,hata mboga isipokua na nazi msosi unakua wa maana.
Itabd nijaribu hyo ya kuweka tui la kwanza sema hapo kwenye kukadiria sasa ndo kasheshe...najua mwanzoni lazima nitoe boko,had nikizoea
Sent using Jamii Forums mobile app
Vile mimi nikipika huwa nikishavimenya navikata kata halafu naweka kwenye sufuria na kuvibandika jikoni kisha naweka maji kiasi ili vianze kuiva lengo baadae muda wa kuchuja nazi nichuje chache ili vikolee nazi navichemsha viazi huku nimeweka tui mbili kama kawaida vikishaanza kuiva kama maji yalikuwa mengi nayapunguza kisha natia tui lile la kawaida na chumvi kidogo baada ya lile tui kukauka naweka lile zito likishachemka kidogo nashusha na hapo vinakuwa tayari kwa kuliwa. Hivyo tu mwaya.
Hivi kumbe viazi vitamu huwa vinapikika vya mafuta? Huwa najuaga vya kuchemshwa na hivyo vya nazi tu mwenzio. [emoji85][emoji85]
Viazi vitamu vilivyochepwa kisha vikaanikwa juani na kukauka.Hiyo Michembe ndio nini Mkuu?
Yeah ntajaribu dear, i hope utatoka bombaHapo kikubwa ni kukadiria lile tui la mwanzo basi yaani inatakiwa ukishaweka mchele mpaka likikauka ubwabwa uwe na kiini kigumu kidogo ili ukiweka lile tui zito ndio kiini kinakuwa cha saizi.
Jaribu mwaya naamini hutashindwa
Vinapikwa na vinakuwa na rojo zuri tu yaani waeza jilamba tena kama unaweza unaweka na iliki kidogo yaani unaitwanga inakuwa laini kisha unamiminia ule muda umeweka tui la kwanza. Vinakuwa na harufu nzuri tu.Eeh me napikaga vya mafuta,natakataka vipande vidogo vidogo kias....
Yaan mapishi haya,mwenyew nlikua sijui kama vinapikwa na nazi. Nmeongeza ujuzi
Sent using Jamii Forums mobile app