Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Safi sana my dear. Nimejifunza hapa.Nikipika wali naa kuku naa.
Nakuna nazi moja kwanza ambayo ni ya mboga. Naweka matui mawili la kwanza zito na la pili sio zito. Naweka mafuta kidogo then kitunguu maji hoho na carrot za kukata box vikichemka kidogo maweka kuku pilipili na saumu. Kisha nyanya, ikiiva naeka chicken masala halafu tui la pili naacha ichemke lipungue kidogo ndio naweka tui la kwanza ikichemka naipua.
Machicha yake nakunia nazi nyingine ya wali kwa juu. Nakamua kiasi kitakachotosha kuivisha mchele. Nabandika jikoni tui langu likichemka natia chumvi na iliki ya unga naweka mchele na carrot ya kusaga. Na kama kuna kamchicha nakawekea tui iliyobaki kidogo ile ya wali ambalo sio zito.
Napenda sana chakula cha nazi.
Hahahaaa. Kwa hivyo lazima uwe mzito kupika Pacha.
Mimi kwangu Pacha tupo wa kutosha hivyo kuingia jikoni lazima niwe naingia jikoni.
Ewaaa. Na magimbi yakikolea nazi yanakuwaje matamu.Magimbi ya nazi
Nachemsha magimbi yakilainika naweka tui la kwanza na chumvi then nayapika kwa moto mdogo had yakiiva vzuri tayari kwa kuliwa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Upate na maharage ya nazi hapo,unaweza kushiba had ushindwe kunyanyukaEwaaa. Na magimbi yakikolea nazi yanakuwaje matamu.
Kabisaa. Na ukishazowea itokee tu kupika kwa kutumia mafuta kwani ukipika na mafuta unaona kama chakula hakina taste ki viile.Me too napenda chakula cha nazi,kinakua kitamu + kinanukia vzur[emoji39]
Sent using Jamii Forums mobile app
Gaucho uko vizuri sana.Nikipika wali na maharage ya nazi.
Wali natumia lile tui jepesi la pili.
Maharage natumia tui zito lile la kwanza.
Sinaga mambo mengi hapo nimemaliza, nakuwa na mchicha wa kukaanga pembeni.
Hata nikimix njegere na nyama nafanyaga hivyo hivyo. Sinaga mbwe sijui tui la kwanza na lapili me ni moja tu.
Safi sana Mtani. Ladha yake si huwa unaiona ilivyotulia?Nikipika wali na maharage ya nazi.
Wali natumia lile tui jepesi la pili.
Maharage natumia tui zito lile la kwanza.
Sinaga mambo mengi hapo nimemaliza, nakuwa na mchicha wa kukaanga pembeni.
Hata nikimix njegere na nyama nafanyaga hivyo hivyo. Sinaga mbwe sijui tui la kwanza na lapili me ni moja tu.
AiseeeHahahaa. Ndio hivyo tupo mbali Pacha.
Ila ukija unitafute Pacha nikupikie vyakula vya nazi ule mpaka ujilambe. 🙈🙈🙈
Acha kabisa my dear. Vyakula vya nazi ni balaa.Upate na maharage ya nazi hapo,unaweza kushiba had ushindwe kunyanyuka
Sent using Jamii Forums mobile app
😀😀Mara moja moja nikiukumbuka mkono wangu.Gaucho uko vizuri sana.
Safi sana my dear. Nimejifunza hapa.
Nieleweshe kidogo mwaya hilo chicken masala ni kwa ajili ya kuku pekee au hata mchuzi wa nyama naweza eka?
Mimi mwisho wangu ni chai na uji😀😀Mara moja moja nikiukumbuka mkono wangu.
Hongera kwa huyo Mdada. Hivyo hapa ulivyoandika hamu imerudi. LolDaaahhh kuna mdada alikuja akanipikia wali Nazi... Njegele Nazi....maini akayakaanga , alafu nyama akaiwekea pia Nazi.
Sitosahau ,nilikula nikashibaaaaa , lkn bado nikawa hamu yakula haiishi ..
Hongeraaaa akina Dada !!