Vhagar
JF-Expert Member
- Jun 8, 2015
- 20,550
- 39,949
Yaani si mchezo aisee mtani, hapo unakuta na jioni naenda kumnyoa mtu goal 4😀😀Safi sana Mtani. Ladha yake si huwa unaiona ilivyotulia?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yaani si mchezo aisee mtani, hapo unakuta na jioni naenda kumnyoa mtu goal 4😀😀Safi sana Mtani. Ladha yake si huwa unaiona ilivyotulia?
Usitake nipae ss hvHahahaa. Ndio hivyo tupo mbali Pacha.
Ila ukija unitafute Pacha nikupikie vyakula vya nazi ule mpaka ujilambe. 🙈🙈🙈
Kupika mbona wala si kazi ni kuamua tu. Me ugumu nauonaga kwenye kuosha vyombo tu.Mimi mwisho wangu ni chai na uji
Na mm nimetega hapa kama ww nataka nione hayo maufundi walionayo watu 😊Aje na yeye atupe mawili matatu. Sababu kupika kwa nazi kupo kwa kila aina.
Hahahaa. Lol. Uje tupike siku moja Pacha.Usitake nipae ss hv
Unajua kupika asee hadi hamu imekuja ghafla..Nikipika wali naa kuku naa.
Nakuna nazi moja kwanza ambayo ni ya mboga. Naweka matui mawili la kwanza zito na la pili sio zito. Naweka mafuta kidogo then kitunguu maji hoho na carrot za kukata box vikichemka kidogo maweka kuku pilipili na saumu. Kisha nyanya, ikiiva naeka chicken masala halafu tui la pili naacha ichemke lipungue kidogo ndio naweka tui la kwanza ikichemka naipua.
Machicha yake nakunia nazi nyingine ya wali kwa juu. Nakamua kiasi kitakachotosha kuivisha mchele. Nabandika jikoni tui langu likichemka natia chumvi na iliki ya unga naweka mchele na carrot ya kusaga. Na kama kuna kamchicha nakawekea tui iliyobaki kidogo ile ya wali ambalo sio zito.
Napenda sana chakula cha nazi.
Daaahhh kuna mdada alikuja akanipikia wali Nazi... Njegele Nazi....maini akayakaanga , alafu nyama akaiwekea pia Nazi.
Sitosahau ,nilikula nikashibaaaaa , lkn bado nikawa hamu yakula haiishi ..
Hongeraaaa akina Dada !!
Keshaolewa Mkuu, mke wamtu anamtoto mmoja saizi.
Basi nikishayachemsha na maji yakaiva hayo maharage huwa nakatia kitunguu maji kikishachemkia na maji na kuweka maji kidoogo, yakikauka huwa naweka lile tui la pili ambalo wakati wa kuchuja lilikuwa la kwanza nakoroga kisha naweka chumvi ya saizi yangu baada ya hapo namalizia lile tui la nazi la mwanzo ambalo hapa huwa la mwisho kisha naliacha lichemke kidogo baada ya hapo maharage yanakuwa tayari kwa kuliwa.
Na vile azam wameturahsishia mambo bas hata ukiona uvivu wa kukuna unakimbia kwa mangi fasta kuchkua pakti yako ikamilishe mapishiKabisaa. Na ukishazowea itokee tu kupika kwa kutumia mafuta kwani ukipika na mafuta unaona kama chakula hakina taste ki viile.
Kwakweli kile chakula hakichoshi...Hongera kwa huyo Mdada. Hivyo hapa ulivyoandika hamu imerudi. Lol
Haijawahi kutokea chakula cha nazi kilichopikwa kikapikika kikawa kinaisha hamu kirahisi rahisi na huwa si ajabu kama mpikaji yupo karibu ukawa unataka kila mara arudie kupika. 😀😀
Hahahaa hutaki mbwembwe nyingi, ila uko vzuri hapo unatoa msosi wa ukwelNikipika wali na maharage ya nazi.
Wali natumia lile tui jepesi la pili.
Maharage natumia tui zito lile la kwanza.
Sinaga mambo mengi hapo nimemaliza, nakuwa na mchicha wa kukaanga pembeni.
Hata nikimix njegere na nyama nafanyaga hivyo hivyo. Sinaga mbwembwe sijui tui la kwanza na lapili me ni moja tu.