Je unawakumbuka herbalist maarufu wa kitambo hicho?

Je unawakumbuka herbalist maarufu wa kitambo hicho?

Huyo profesa Matunge alikuwa 'jiniaz' kuweza kucheza na akili za watu maisha yake yote mpaka kufa!

Je kuna mtu anayefahamu kuwa alikuwa hajasoma na alikuwa siyo mganga?
duh kama ni kweli basi huyu jamaa alikuwa mbele sana ya wakati maana hata mm ndo nasoma apa kama jamaa hakuwa na chembe ya uganga maana jamaa alikuwa smart sana kimavazi suti black mda wote na afro lake amechana safi na hata matangazo yake yalikuwa yamenyooka sana na anapost gazetini kila leo daah kumbe alikuwa chenga tupu🙆‍♂️🙆‍♂️.
 
Matunge alikuwa anatangaza nimefikia Guest Fulani maeneo ya Forest ya Zamani Mbeya kama una shida wahi mapema
 
Jaman kama hii list isingemtaja Isaac ndodi mimi ningejiuzulu, huyu bwana nlikuwa namwita Dr haleluya, kipindi anaaza, alikuwa anasema ukimkuta mtu ana kitambi piga viboko vya kutosha, alikuwa kakondeana hana hela alivyopata hela kanenepa kawa wa duara ukimuuliza imekuwaje unakula matusi....nimeweka picha ya wakati anaweza career yake na kusema tupigwe viboko na alivyo sasa 😂😂😂. Nlikuwa nkikaa star tv kwa kipindi chake nacheka sana....
sasa apa kavaa suti kitambi hakionekani vizuri 🤣🤣pata picha aliyochomekea shati
 
Matunge alikuwa anatangaza nimefikia Guest Fulani maeneo ya Forest ya Zamani Mbeya kama una shida wahi mapema
iyo ndo ilikuwa mikwara yao🤣eti yupo kwa wiki hii tu baada ya hapo humpati tena atakuwa mkoa mwingine🤣watakaowahi kuna bei ya punguzo
 
yalivoingia mambo ya makanisa ya miujiza yamechukua kazi zao hawa jamaa na wengine wakalazimika kufungua makanisa yao
 
Back
Top Bottom