Uchaguzi 2020 Je, Unaweza kupita Ubungo Interchange usiseme asante Magufuli? Mtakubaliana na mimi, asante stahiki ni kura zote kwa Magufuli

Uchaguzi 2020 Je, Unaweza kupita Ubungo Interchange usiseme asante Magufuli? Mtakubaliana na mimi, asante stahiki ni kura zote kwa Magufuli

Hatumpi kura, anaruhusiwa hata yeye kupita kwenye hiyo flyover, na akitoka pia madarakani wengine watajenga vingine na atakuwa na haki ya kuvitumia bila kulazimishwa awapigie kura. Asante yake sio kwenye kura, bali atalipwa mshahara mpaka atoke duniani.
 
Na sisi wa kyakairabwaaa nanjirinjiiii mtakujaa tunaruhusiwaa kusherekea hili jambo au tuendelee kupambana na tope zetu
 
Paskali, from mwanahabari nguli to mlamba viatu. Kilichojenga flyover ni fedha za walipa kodi wa Kitanzania. Hatukuwahi kumsikia Mwalimu Nyerere akijisifu kuhusu "kutuletea uhuru" au Mwinyi kujisifu kuhusu "kuruhusu mitumba" au Mkapa kujisifu kuhusu "daraja la Mkapa" au Jk kujisifu kuhusu "utitiri wa vyombo vya habari." Tatizo lako bwana Paskali kwa upande mmoja ni NJAA na upande mwingine UKABILA. Ndio sababu ya kuweka akili makalioni. Ovyo kabisa 😡
 
1601915018276.png
 
Kaka sitaki kabisa kuamini kama hili andiko ni la nguli wa habari Pascal Mayala tunayemfahamu, Mwandishi wa kujitegemea ambaye aliwahi muuliza JPM swali gumu wakati akitangaza baraza lake la kwanza la Mawaziri alipoingia madarakani, Mzee akachanganyikiwa na lile swali na kuamua kufuta Press conference zozote na waandishi wa habari hadi leo hii.
Kwanini nasema kuwa hili andiko sio la Pascali

1. Pascal Mayala ninayemfahamu anaelewa kuwa serikali kujenga miundo mbinu sio kutenda wema bali ni wajibu wake na Pesa inayotumika ni kodi yetu wananchi. Alichokifanya Magufuli kupitia Bunge letu ni kutimiza wajibu wake kama anavyotakiwa na sheria pengine angetoa Pesa yake ya mshahara kujenga hayo madaraja hapo sawa angekuwa amatenda wema.

Aliyeiba account ya Pascal Mayala tafadhali usifanye hivyo unamdhalilisha nguli wa habari hapa nchini.

Naamini hii account ni FAKE..Pascal hawezi andika ujinga huu hata kama anafuta Ukurugenziau Ukuu wa Wilaya kwani zipo njia nyingi anazoweza kutumia kutokana na weredi wake katika Tasnia ya habari lakini sio kwa kuandika upuuzi huu!
 
Mbona kuna habari kuwa utafungiwa ukienda kinyume cha JF? Kwa sasa bora Paskali ukae kimya hadi November 2020 vinginevyo.
 
kwani hiyo interchange Magufuli kaijenga kwa fedha zake toka mfukoni,si ni kodi zetu wananchi ,ujue mnakera Sana nyie MATAGA kwa jinsi mnvyomsujudia Jiwe utafikiri hela anazitoa mfukoni mwake mnakera mnoo[emoji34][emoji34]
 
Yani mtu kateka watu, kabambizia watu kesi, kaua watu , kaharibu biashara za mazao huko wakulima wanakufa masikini si kahawa, chai, korosho, tumbaku, mbaazi na mahindi!!

Kafilisi watu kwa chuki zake hadi wamefunga biashara na wengine wamekufa alafu nije kumshukuru kwa mradi aliouanzisha kikwete na ukajengwa kwa fedha za Bank ya Dunia ambazo tutalipa kwa kodi zetu?

Jinga kabisa wewe!! Ndo mana wana CCM kawe walikutosa vibaya!!
 
Wakati wa jk tulikaa kwenye folen tukiwa na ela mfukoni

Wakati huu tunapita juu hapo ubungo tukiwa na mawazo ya kesho nakula nn

Mshahara ule ule gharama zimepanda Mara Mia
Mwendokasi imejengwa na shangazi yako
 
Kaka sitaki kabisa kuamini kama hili andiko ni la nguli wa habari Pascal Mayala tunayemfahamu, Mwandishi wa kujitegemea ambaye aliwahi muuliza JPM swali gumu wakati akitangaza baraza lake la kwanza la Mawaziri alipoingia madarakani, Mzee akachanganyikiwa na lile swali na kuamua kufuta Press conference zozote na waandishi wa habari hadi leo hii...

kuwa mtu wa uhalisia, acha hizo theory. Kwa nini hii interchange ya Ubungo haikujengwa miaka 50 iliyopita. Ili tuendelee tunahitaji mambo manne; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Rais Magufuli ameonesha uongozi bora chini ya siasa safi ya CCM. Chagua Rais Magufuli, Chagua Maendeleo.
 
Juzi nimepita Ubungo interchange toka Mwenge kwenda Buguruni, it is an amazing experience.

Kwenye family context, kuna wababa wana hela ila wanakula bata wao pekee yao japo ni wajibu wana watoto wao wafurahi sehemu ya fedha anazopata mzee in the course of working.

Kwa kazi chache za kujenga barabara na madaraja ikiwamo Ubungo interchange; tuna wajibu kama wanafamilia Tanzania kumsifu na kumshukuru JPM kwa kutimiza wajibu wake kujenga.

Kongole mwanakwetu JPM, unastahili mi5 tena
 
Ahsante shujaa Dr John Pombe Magufuli, umefanya yale yaliyooneka miujiza hayawezekani. Watu wenye mawazo mafupi hawawezi kuelewa lakini baada ya muda watakula matunda na kuimba nyimbo za kukupongeza
 
kuwa mtu wa uhalisia, acha hizo theory. Kwa nini hii interchange ya Ubungo haikujengwa miaka 50 iliyopita. Ili tuendelee tunahitaji mambo manne; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Rais Magufuli ameonesha uongozi bora chini ya siasa safi ya CCM. Chagua Rais Magufuli, Chagua Maendeleo.
Kwahiyo kwakuwa haikujengwa kwa miaka 50 inakuwa hisani ya Magufuli au? Kwahiyo Magufuli ana siasa safi na uongozi bora? Kama unaamini hivyo basi ni miongoni mwa watanzania wanaoongeza vichwa kwenye nchi.
 
Back
Top Bottom