Je, Usafirishaji wa Wanyama nje ya nchi itachangia ongezeko la Watalii au tunaenda kuua soko la Utalii ndani ya nchi?

Je, Usafirishaji wa Wanyama nje ya nchi itachangia ongezeko la Watalii au tunaenda kuua soko la Utalii ndani ya nchi?

The Supreme Conqueror

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2017
Posts
458
Reaction score
1,280
Wizara ya utalii imetoa tamko la serikali kuondoa zuio la kusafirisha wanyama nje ya nchi katika mashamba yaliyokuwa na vibali maalumu ya kusafirisha wanyama hao nje ya nchi.

Je, unadhani hii itachangia watalii wengi kuja nchini kwajili ya kuwekeza katika mashamba ya umiliki wa wanyama na utalii kwa ujumla au itachangia kwa namna moja au nyingine kuua soko la utalii nchini Tanzania?

Karibu tuchangie uzi wana JF.
 
Kama Tanzania tumenunua vipande vya ardhi huko Ng'ambo kwa ajili ya kuanzisha bustani za wanyama huko chini ya Wizara ya Maliasili ili kukuza kipato. Hakuna shida.

Shida ninayoiona, ni kukwamishwa ama kucheleweshwa mradi wa Bucha rasmi za wanyama pori hapa nchini kama tulivyoahidiwa.
 
Wizara ya utalii imetoa tamko la serikali kuondoa zuio la kusafirisha wanyama nje ya nchi katika mashamba yaliyokuwa na vibali maalumu ya kusafirisha wanyama hao nje ya nchi....
Usipende kuandika kitu ambacho huna ufahamu nacho.

Ukisikia wanyama pori akili yako inskupeleka kwenye big five kumbe hujui kuna biashara ya mijusi, vimyonga ndege and likes, hayo ni maish ya watu tena Watanzania, mbona hamshupazi shingo madini kuuzwa nje?
 
Wizara ya utalii imetoa tamko la serikali kuondoa zuio la kusafirisha wanyama nje ya nchi katika mashamba yaliyokuwa na vibali maalumu ya kusafirisha wanyama hao nje ya nchi...
Kama wanyama, tena hai, wanapelekwa huko, ina maana watakuwa hifadhi zao. Waje huku kuangalia nini tena?
 
Back
Top Bottom