Uchaguzi 2020 Je, utabiri wa Mwalimu Nyerere kuwa upinzani wa dhati nchini utatoka ndani ya CCM kuanza kutokea katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu?

Uchaguzi 2020 Je, utabiri wa Mwalimu Nyerere kuwa upinzani wa dhati nchini utatoka ndani ya CCM kuanza kutokea katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Katika moja ya hotuba zake muhimu kwa nchi hii wakati wa uhai wake Mwalimu Nyerere aliwahi kutoa utabiri kuwa upinzani wa dhati nchini utatoka ndani ya CCM.

Kutokana na kujitokeza kwa mwanasiasa, Bernard Membe kudai kuwa amepania kuchukua fomu ya kugombea Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, kwa tiketi ya CCM, ndiko kunakonifanya nione kuwa utabiri wa Mwalimu Nyerere unaweza kuanza kutimia katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Kwa maelezo anayotupa yeye mwenyewe, Bernard Membe, kuwa amepania kugombea nafasi ya Urais kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu, kwa tiketi ya CCM, tena akiendelea kusisitiza kuwa Kuna kundi kubwa sana la wanaccm linalomwunga mkono kwa uamuzi wake huo, ila kwa sasa hatawataja kwa kuhofia kuwa watafukuzwa ndani ya CCM, kutokana na uendeshwaji wa chama hicho ambao umejaa vitisho na kutotaka kusimamia Katiba ya chama chao kwa hivi sasa.

Ingawa Mheshimiwa Membe, anaweza hesabika kuwa siyo mwanachama tena wa CCM, kwa kile kinachodaiwa kuwa amefukuzwa uanachama wa CCM, hata hivyo yeye mwenyewe amekaririwa akisema kuwa kikao kilichomfuta uanachama cha Kamati Kuu ya CCM ni batili, kwa kuwa kikao pekee cha kumfukuza yeye uanachama wake kilipaswa kuwa cha Halmashauri Kuu ya CCM, ambacho hadi sasa hakijakaa.

Pamoja na madai yake ya uvunjaji huo wa wazi wa Katiba ya CCM, katika kuvuliwa uanachama wake, Mheshimiwa Membe, kwa ujasiri mkubwa.na bila unafiki, ameendelea kudai kuwa yeye bado ni mwanachama halali wa CCM, kwa mujibu wa Katiba ya CCM.

Katika hali halisi inaonekana kuwa wapo wanaccm wengi nchini, ambao hawaafiki kwa mambo yanavyoendeshwa hapa nchini, ya uminywaji wa haki za binadamu, ukandamizaji wa demokrasia, kuvifungia vyombo makini mbalimbali vya habari na matumizi ya vyombo vya dola kuminya upinzani, kwa manufaa ya chama cha CCM , kwa hiyo wapo nyuma ya Mheshimiwa Membe, ambaye amejitokeza bila hofu yoyote, pamoja na hatari anayoiona kwake ya utawala huu wa "mkono wa chuma" kwa lengo la kuiokoa nchi yetu, isiendelee kuzama katika utawala huu usiozingatia Katiba ya chama chao wala Katiba ya nchi, ambayo viongozi wakuu wote wa nchi, waliapa kuitii na kuitekeleza kabla hawajaanza utumishi huo wa Umma

Hebu tusubiri tuone kama alivyotuambia yeye mwenyewe, Bernard Membe, kuwa lolote linaweza tokea, kati ya hivi sasa hadi mwezi October mwaka huu!
 
Huo Msemo ukiutafakari sana,Utakuja kuelewa ni kama Siri aliyowaachi Marais wote,na ndio pekee wanajua ukweli wa huo msemo,
Ila tafakari kidogo,Kwanini kila uchaguzi lazima Ccm wenyewe Wasigane,lazima atokee mgombea haelewani na mwenyekiti...
Toka enzi za kambona,mtei,Mrema,Mamvi,ni kama tunaimbishwa nyimbo zile zile kila siku,na tunazicheza vizuri tu..
Ni kama secret code flani,ila wenye kuuelewa huo msemo ni marais tu,trust me,sio msemo wa kawaida...
Siasa bongo tunachezeshwa gere tu........
 
KUWA MZALENDO SHIRIKI UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2020 (RAIS, WABUNGE NA MADIWANI) KWA MAANA NI HAKI YAKO YA MSINGI SANA KIKATIBA
 
Mleta uzi usitegemee lolote toka ndani ya ccm. Hiyo mitazamo ya Nyerere ni ya karne iliyopita wanaccm walipokuwa wanaoongozwa na itikadi. Sasa hivi mambo yamebadilika, utashi na maono binafsi ya mwenyekiti wao ndio itikadi ya ccm. Sasa hivi vyombo vya dola ndio vinafanya siasa na sio siasa kujiendesha yenyewe. Hivyo yoyote aliye nje ya nguvu ya dola, ana nafasi ndogo sana ya kutekeleza hiyo ndoto ya Nyerere.
 
Mleta uzi usitegemee lolote toka ndani ya ccm. Hiyo mitazamo ya Nyerere ni ya karne iliyopita wanaccm walipokuwa wanaoongozwa na itikadi. Sasa hivi mambo yamebadilika, utashi na maono binafsi ya mwenyekiti wao ndio itikadi ya ccm. Sasa hivi vyombo vya dola ndio vinafanya siasa na sio siasa kujiendesha yenyewe. Hivyo yoyote aliye nje ya nguvu ya dola, ana nafasi ndogo sana ya kutekeleza hiyo ndoto ya Nyerere.
Acha uongo na kupotosha umma. Ccm inaendeshwa kwa kufuata misingi ya katiba yake,itikadi zake na. matakwa ya wanchama. Ndio maana maamuzi yanafanywa kwa kuzingatia vikao na mikutano ya wanachama. Sio mali ya mtu mmoja kama Chadema.
 
Acha uongo na kupotosha umma. Ccm inaendeshwa kwa kufuata misingi ya katiba yake,itikadi zake na. matakwa ya wanchama. Ndio maana maamuzi yanafanywa kwa kuzingatia vikao na mikutano ya wanachama. Sio mali ya mtu mmoja kama Chadema.
chagu wa malunde
Hebu tuambie namna mlivyomfukuza uanachama wake Membe , ndivyo inavyotakiwa katika Katiba ya CCM?
 
1593051685968.png
 
Rejea ya EL na JK2 baada ya Muhula wa kwanza wa JK na ya EL na Magufuli session 1
 
Mwalimu Nyerere sio Mungu, utabiri wake hauna maana yoyote na usiwafunge akili watanzania.
 
Siasa za Nyerere umezisoma ila hukuwapo..
Ni worse than this.... ila woga ulitawala.

Karatasi ya kura ilikuwa picha na kivuli....

Hapana... hapana mwingine zaidi yake
Ndio... tumemkubali anafaa aongoze milele
Mleta uzi usitegemee lolote toka ndani ya ccm. Hiyo mitazamo ya Nyerere ni ya karne iliyopita wanaccm walipokuwa wanaoongozwa na itikadi. Sasa hivi mambo yamebadilika, utashi na maono binafsi ya mwenyekiti wao ndio itikadi ya ccm. Sasa hivi vyombo vya dola ndio vinafanya siasa na sio siasa kujiendesha yenyewe. Hivyo yoyote aliye nje ya nguvu ya dola, ana nafasi ndogo sana ya kutekeleza hiyo ndoto ya Nyerere.
 
Nyerere alifukuza wangapi na aliwafukuzaje mkuu?
Aliwafukuza kwa mujibu wa Katiba ya CCM.............

Yaani kwa kutumia vikao halali vilivyoainishwa katika Katiba ya CCM

Sivyo afanyavyo Jiwe, ambaye wala hafuati Katiba ya CCM, wala Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Yeye ni kutembeza ubabe na vitisho kwa kwenda mbele..................
 
chagu wa malunde
Hebu tuambie namna mlivyomfukuza uanachama wake Membe , ndivyo inavyotakiwa katika Katiba ya CCM?
Mwenyewe Membe kasema kamati kuu haina huo uwezo , sasa kufukuzwa kwake kunatoka wapi??
Hivyo kufukuzwa kwake ni batili na yeye anasubiri Mkutano Mkuu,
Njia nyingine angeandika barua ya kupinga kufukuzwa, kwake kama alipata barua ya kufukuzwa kwake na yeye akiwa ni "mbobezi" haya mambo ni ya wazi kwake.
Na kama hakupewa barua ya kufukuzwa basi yeye bado ni Mwanachama na kwakuwa haogopi kesho/Leo wakifungua offisi akachukua fomu si ni haki yake ?
Wakimnyima aende mahakamani.
 
Mwenyewe Membe kasema kamati kuu haina huo uwezo , sasa kufukuzwa kwake kunatoka wapi??
Hivyo kufukuzwa kwake ni batili na yeye anasubiri Mkutano Mkuu,
Njia nyingine angeandika barua ya kupinga kufukuzwa, kwake kama alipata barua ya kufukuzwa kwake na yeye akiwa ni "mbobezi" haya mambo ni ya wazi kwake.
Na kama hakupewa barua ya kufukuzwa basi yeye bado ni Mwanachama na kwakuwa haogopi kesho/Leo wakifungua offisi akachukua fomu si ni haki yake ?
Wakimnyima aende mahakamani.
Mkutano mkuu au Cc?
 
Mwenyewe Membe kasema kamati kuu haina huo uwezo , sasa kufukuzwa kwake kunatoka wapi??
Hivyo kufukuzwa kwake ni batili na yeye anasubiri Mkutano Mkuu,
Njia nyingine angeandika barua ya kupinga kufukuzwa, kwake kama alipata barua ya kufukuzwa kwake na yeye akiwa ni "mbobezi" haya mambo ni ya wazi kwake.
Na kama hakupewa barua ya kufukuzwa basi yeye bado ni Mwanachama na kwakuwa haogopi kesho/Leo wakifungua offisi akachukua fomu si ni haki yake ?
Wakimnyima aende mahakamani.
Asipindishe maneno alishafukuzwa na Cc ilishalidhia.
 
Back
Top Bottom