wamtaje jina au wakwepe kumtaja jina hawamuondolei chochote legacy yake iko hai inaonekana inamtetea yenyewe hakuna mwananchi anaepita njia ya ubungo kibaha bila kuona maendeleo makubwa yaliyofanyika awamu ya tano,hao wanaopata vigugumizi kumtaja ukiwauliza wamelifanyia nini Taifa hawana la kusema ni bla bla tu
 
Inamaanisha wakati alipokuwa waziri wa ujenzi?.
Unamkumbuka nyumbanyeupe alikuwa nani kipindi hicho ama unajitoa akili.

JPM hakuwa na uwezo wa kununua hiyo meli bila idhini ya mkuuwake wa kazi.

Sawa Mkuu basi Yeye na huyo wa Jumba Jeupe warishiriki katika Upigaji.....Wapigaji ni Mawaziri ila mshiko wanampa na mkuu wao....ndiyo maana Kangi Lugola(Nyoka wa shaba) alivyopiga deal peke yake bila kumshirikisha JPM akalisanua...Kwahiyo wapigaji ni mawaziri.
 
Wana balaa sana, 2025 watalitaja tu. Watake wasitake.

Mtu kafanya makubwa lakini hawataki kuelewa ila wananchi wakielewa imetosha.
 
Vp kuhusu hii ya kufanyia marekebisho kwa 7.5B kivuko cha 8B?by theway hakuna speedbot ya Bahharesa ya 4B acheni story za vijiweni ingekua rahisi hivyo hio biashara matajiri wengi wangeifanya, ingekua km biashara ya mabasi ya mikoani.
1. Marekebisho kwa 7.5B ni weezy tu kama wizi mwingine.

2. Mkuu wewe ndiyo unaleta story za vijiweni ,SSB kanunua mwenyewe kwa 4B ,ebu jaribu kugugo utoe tongo tongo.
 
Narudia tena asingekuwa Magufuli, makao makuu yasingehamia Dodoma, kulikuwa na ujanja ujnaja mwingi wa kuhamia huko, lakini aliyetekeleza ni yeye. Hata kama Nyerere alitoa hoja kulikuwa hakuna mkakakti wa makusudi kabisa. Yaani ofisi za wizara ziliendelea kujengwa Dar. Huku mdomoni tunasema tunahamia Dodoma
 
Muulize Prof Assad ndiyo aliofichua huo wizi mpaka mkamfukuza.
Ona sasa unavyounga unga.

Hujui hata sababu za Assad kutoongezewa mda.

Ndio maana umekalili wizi.

Iko hivi; Prof Assad hakuongezewa mda baada ya kwenda nje ya nchi na kufanya siasa za ukaguzi wa hesabu kwenye media za kitaifa kulikandia bunge. over.
 
Kwa imani yangu, bila shaka JPM ni mmoja wa Watakatifu waliopo huko Mbinguni. Hii ni kutokana na uongozi wake wa kuguswa sana na shida za Watanzania.

Yes sometimes imani ikivuka mipaka unakuwa delusional
 

Tumia Ubongo wako vizuri na pia tumia fedha ulizolipiwa na walipa kodi kukusomesha ili kusaidia nchi na sio kubwabwaja tu.

Unataka kuniambia kesi aliyofungua zitto kuhusu kufukuzwa kazi Prof Assad na "Mtu furani" ambayo inakiuka katiba haijui hukumu yake?
 
R.I.P MWAMBA WA AFRIKA JPM
Sema mwamba wa chato, ivi JPM alifanya nn Cha kukumbukwa kwa Africa Hadi mnampa jina kubwa ivyo? Aliwahi kwenda hata AU akatoa hotuba ya kutisha kwa ajili ya Afrika? Au UN akathubutu kunguruma kule hata wakamjua? Yule ni mwamba wa chato, ndani ya miaka mitano aliitoa kwenye hadhi ya Kijiji Hadi mji, angemalizia mi5 ingekuwa manispaa
 
Achana nao, wanatumia Masabiri kufikiri, ndege imeshikiliwa uholanzi huko tunadaiwa, mbili hazifanyi kazi sababu ya tatizo ambalo alionywa kabla hajanunua akapuuza akisema wanaomuonya siyo wazalendo. Yaani ushamba....??
 
Mimi kwangu huyu mzee alikuwa 50%50%. Alikuwa mchapakazi mzur na mthubutu mzur ila kwenye uchumi 0. Hashauriki na alikuwa mbaguz hasa hili ndio lilimletea shida zaidi. Aliruhusu wezi kuibia watu kwa kisingizio cha uhujum uchumi hasa hela za maduka ya kubadilishia hela. Kama Mungu wake angemjalia kutokuwa mbaguz au huo wiz au angekuwa anashaurika angekuwa bonge la rais. Cntakaa nisahau cku moja natoa container la viatu mimi najiran yangu nae alikuwa anatoa the same container. Baada ya kumaliza kila kitu mzigo ilivyoruhusiwa tu ikakamatwa tena siijui hamkukadiriwa kihalali. Mi nikapigwa faini million 22 jamaa yeye jina lake la kisukuma akaulizwa we ni msukuma kasema ndio. Wakamwambia bahati yako wakampiga faini ya milion 2. Mind u mshikaji duka lake na langu ni pua na mdomo. The same product.na hiyo ndio sababu ya mimi kufungua duka lusaka na Lubumbashi. Ila yote na yote Mungu wake amsamehe makosa yake ampe pumziko la amani. Kwangu mimi kila kitu hutokea ni la kujifunza.
 
Zitto alifungua kezi zidi ya nani?

Hukumu ilitolewa lini na nani alikuwa anaisimamia?

Zitto unamuelewaga wewe?

Zitto alikuwa anasimamia kutoongezewa kwa mda kwa Prof Assad, kwa katiba alitakiwa aongezewe, lakini haikufanyika hivyo, na sababu ya kutoongezewa ni kwa sababu ya kuleta siasa kwenye profesional ya ukaguzi. Prof anajionaga yeye hakosei, alipopata nafasi ya kwenda marekani akakaa kwenye media na kutema nyongo zake zidi ya bunge na serikali kisa tu mambo yake hayajafanyiwa kazi yote kama livyo pendekeza.

Swali; Tangu kuanzishwa kwa nchi hii ni lini Bunge na Serikali lilishafanyia kazi mapendekezo yote kama yanvyosomwa na CAG? una mambo mengine hayawezekani, sana sana Serikali itafanya mabadiliko ya uongozi tu. either kwa kutumbua ama kwa kuhamisha ili kuleta usanifu.
Na ndio maana hadi leo unaona tu madudu yapo.
 
JPM ulifahamu yaliyokuwa yanaendelea nchini katika utumishi wako wa miaka ishirini na tano kwenye medani ya siasa. Wakati wa uongozi wako ulijali Sana wananchi wa daraja la chini ambapo tulinunua mchele tsh. 1200/= kwa kilo; kwa utawala wa Sasa unaojipambanua kwa kuingiza magari 60 ya Mwigulu Lameck Nchemba kwa siku moja; kilo moja ya mchele kwa Sasa tunainunua kwa tsh. 3500/=. Hakika tutakumbuka baba ila uliokuwa umeziba mirija yao ya matumizi mabaya ya fedha ya umma daima wataendelea kukulaani bila kufahamu kuwa ulishalala milele na hakuna siku amabayo utaweza kuwajibu.

Wamebaki wanasiasa uchwara akina Hussein Bashe wasiofahamu hata jembe linashikwaje lakini eti leo Bashe ndye waziri wa kilimo. Wananchi tunaumia Sana Tena Sana lakini BEPARI Bashe anajinasibu kuwa mazao sio Mali ya serikali kwa hiyo wakulima waachwe wauze wanavyotaka. Mkulima wa kawaida hanufaiki na kauli ya kijinga, KEJELI, DHIHAKA na KIZANDIKI ya bepari Hussein Bashe bali anawapaka mafuta kwa mgongo wa chupa kwani wanufaika wakuu wa mfumuko Mkubwa na wa kutisha wa Bei ya chakula Ni bepari Bashe na washirika wake.

Wakati wa uongozi wako hakukuwa na nyongeza ya mshahara lakini maisha yaliendelea bila shida kutokana umakini wako wa kudhibiti mfumuko wa Bei ya chakula. Leo mtu anaona vema kuhudumia watoto wa jirani wake wakati nyumbani kwake watoto wa wanalala njaa!. Daima tutakumbuka JPM.
 
7. Alipiga marufuku Mikutano, Warsha nk nje ya sehemu za kazi kuwa ni upotevu wa muda na fedha za umma. Lakini Serikali yote ya Awamu ya Sita imejikusanya Arusha kutumbua tu na si vinginevyo
 
Kwamba siasa ni mtaji wa kujitajirisha
 
Umehitimisha tofauti kubwa kati ya Magufuli na MaRais wengine kuwa alijari zaidi maisha ya watawaliwa wasio nacho km kuboresha miundo mbinu na huduma za jamii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…