Je, utumiaji wa kiyoyozi(AC) unaongeza matumizi ya mafuta kwenye gari?


Hahahahaha😀😀😀😀
 
RRONDO;
umewahi kukaa kwenye foleni??? Kama upo Highway sawa, pandisha vioo, weka AC. Hapo sawa sawia kabisa, lakini kwenye foleni, mafuta ya lita 2 uweke AC?

Ni kweli kabisa langu cylinder 6 ukikaa kwenye foleni ya Mbagala mjini basi viwese vyote vinakwisha hapo.

Hivi sasa AC ina matatizo sifungui basi nina afueni kubwa ya mafuta.
 
Ni kweli kabisa langu cylinder 6 ukikaa kwenye foleni ya Mbagala mjini basi viwese vyote vinakwisha hapo.

Hivi sasa AC ina matatizo sifungui basi nina afueni kubwa ya mafuta.

ukikaa kwenye foleni as long as engine iko on inakula mafuta.....hapa unajipa moyo tu
 

Kwa hypothesis yako Mabasi yote wangekuwa wanatumia AC ili kubana mafuta.
Ila kama unaenda safari ndefu kwa uzoefu wangu ukiwasha AC mafuta hutumika sana kuliko kufungua vioo hata hiyo dragforce unayosemea ukiwa katika spidi kubwa hutaweza kufungua vioo hadi mwisho
 
Last edited by a moderator:

1.wenye mabasi hawana elimu hata ya kuendesha yale magari so elimu huu ni way too much for them
2.you are completely wrong. ukisafiri na ukienda 80kph na vioo wazi unatumia 20% more fuel kuliko ukiwasha ac na ufunge vioo.

http://auto.howstuffworks.com/fuel-efficiency/hybrid-technology/driving-with-windows-down1.htm
 
ukikaa kwenye foleni as long as engine iko on inakula mafuta.....hapa unajipa moyo tu

Siyo kujipa moyo lakini hiyo ni uhakika maana wakati AC ilipokuwa inanguruma ilikuwa inakula kama lita 50 diesel kwa wiki, lakini sasa bila AC zinabaki na kuendelea mpaka wiki ya pili.

Na dereva ni mimi tu kwa hivyo kufanya monitoring ni rahisi.
 
Ni kweli kabisa langu cylinder 6 ukikaa kwenye foleni ya Mbagala mjini basi viwese vyote vinakwisha hapo.

Hivi sasa AC ina matatizo sifungui basi nina afueni kubwa ya mafuta.

Tena foleni ya kimara unapata mimba isiyo na MZAZI

ujafika oilcom unasikia kama mtu Analisukuma kumbe mafuta yamekata
 
mimi kigari changu hata sijuagi vioo vinafunguliwaje nijuzeni wadau.full kipupwe.

kwani unajuaga bei ya ltr 1 ya mafuta..ukiacha vile vibill vya ofisini lte 50 kwamwezi unapeleka oilcom
 

Mkuu asante kwa taarifa yako japo na mimi nilishaisoma miaka 4 iliopita kwenye link hiyo hiyo uliotupa. Humu kuna watu wabishi wanaamini walichozoea na stori za mitaani kua AC inakula sana mafuta.
Japo wameshauri kwenye hiyo makala kua kama unaendesha kwenye jam kubwa gari inapokwenda kwa mwendo mdogo sana ni bora ukashusha vioo na kuzima AC kama unataka kusevu mafuta .
 
 

imebidi niweke hio link kwasababu kuna wenzetu bado wanaamini AC inatumia mafuta sana kuliko wakishusha vioo na kuendesha.
 
Siyo kujipa moyo lakini hiyo ni uhakika maana wakati AC ilipokuwa inanguruma ilikuwa inakula kama lita 50 diesel kwa wiki, lakini sasa bila AC zinabaki na kuendelea mpaka wiki ya pili.

Na dereva ni mimi tu kwa hivyo kufanya monitoring ni rahisi.

kiukweli gari ikiwa imesimama au inatembea taratibu kwenye foleni,AC itatumia extra fuel kwa sababu ukiwasha AC rpm inakuwa 800-1000 na ikiwa idle rpm inakuwa 500-600,na sio muda wote,inapanda na kushuka kwahio ni kiasi kidogo sana kinaongezeka.

lakini ukiwa unaendesha freely ukifungua vioo unatumia mafuta mengi kuliko ukiwasha AC na kufunga vioo kwa sababu ya 'DRAG' tena ukiwa highway at 80kph unatumia 20% more!!.....kwahio kama uko kwenye foleni mbaya zima gari kabisa,zima ac fungua vioo kwasababu hata ukizima ac gari inaunguruma itatumia mafuta bila kusogea.
 
hiyo theory yako ni kweli but haiku take into consideration scenario za magari ya africa kama mafuta ya tanzania tunayotumia ambyo yamechakachuliwa na fake plugs za gari.mfano i own a vw golf gti,ilivokuja trip computer readings ilikua inasoma 1 litre kwa 13km ila after a while baada ya mafuta ya kibongo kutumika now inasona 1 litre kwa 10kms na nkizima ac inapanda mpaka 1:11kms...hata turbo boost husoma 1.0 psi which is inadequate.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…