Black Sniper
JF-Expert Member
- Dec 10, 2013
- 32,406
- 55,148
Tena wanashangilia kwa kuambiwa tembeeni vifua mbele huku hajala tangu asubuhiWatanzania walikuwa wakiambiwa sie si maskini hawakuwa wanaamini.
Ila kiukweli umaskini upo vijijini kuanzia barabara mbovu, ukosefu wa umeme, na hali duni ya maisha.
Mkuu Asante kwa hiloMkuu, mimi niliishi pale UK na kwa kweli mfumo wao wa biashara haujali mtu atoka wapi ili mradi ana pesa ya kuwekeza na atatoa ajira kiasi gani na atalipa kodi.
Pili, mtu ambae ataendesha na kusimamia hiyo biashara si mtu wa kawaida ni vichwa khasa.
Kwa mfano yapo yale maduka madogomadogo yaitwa "Discount Chains" mojawapo ni Poundland.
Poundland huuza kila kitu kwa pauni moja tu! lakini ina maduka nchi nzima na mwaka 2016 ilinunuliwa na kampuni ingine yaitwa Pepco Group. Hawa Pepco Group waitwa kitaalam Institutional Investors yaani ni wawezekezaji ambao wamejikita katika biashara hizo za maduka ya bei ndogo.
Hawa Pepco nao ni kampuni tanzu tu kwamba nao iko chini ya kampuni kubwa ya kimataifa iitwayo Steinhoff International ambayo ni ya Afrika Kusini. CEO wa zamani wa Asda ndie asimamia Pepco Group na hii kampuni imeajiri watu 30,000.
Poundland UK ana maduka yapatayo 500 na hawa Pepco Group pia wana kampuni ingine iitwayo Dealz ipo Ireland.
Kwenye hizi biashara ni lazima utumie kampuni zenye mitaji mikubwa au Equity Firms ambazo zote hupata fedha kutoka kwa mazee Rothschild.
Walichofanya wenzetu wahindi na waarabu au wachina ni kujipenyeza hadi ndani yaani "centre of operations" ya hizi shughuli za fedha na ndani kabisa ya viambaza vyao hawa maglobalists.
Sie waafrika yatubidi kwanza tufanye mapinduzi makubwa ya kiakili na kijamii ijitambue kisha tujiweke sawa na tuone twaanzia wapi.
Mafanikio yao yasiyowahusu watu wangu hayanihusu wala kunihangaisha. Wana TATA ndiyo. Kwani hao waajiriwa elfu nane ni wamakonde wenzetu au magabacholi. Hawa jamaa wana roho mbaya na ni wabaguzi. Kuwatetea ni sawa na kutetea ukimwi kuwa ni bingwa wa kuuaMkuu Asante kwa hilo
Hapa Wilko pia wamekwisha na kufunga maduka yao ila B&M wamenunua maduka 51 na rivals wengine wamepitia yaliyobaki
Kweli wahindi, wachina, na hata waarabu wamepenya kwenye biashara kubwa kwa sababu wakisoma huku hawakariri kama waafrika anaerudi nyumbani na makaratasi
Hii ndio tofauti zetu
Hebu angalia jirani wanalia na kusema mwaka 2050 Kenya itakuwa ya wasomali kwa sababu wame dominate biashara zote na wanaporomosha majengo kila leo huku wakizaana sana
Baadhi wanajielewa mkuu ila Wahindi hata watukanwe wako mbali sana
Kampuni ya TATA ipo hapa ๐ฌ๐ง na imeajiri wafanyakazi Elfu 8
Kwa kweli mimi binadamu hanipi shida kwa ubaguzi wake kwani nimeishi middle east miaka ya nyuma na huko wahindi wanadharaulika sana na hata kuzabwa makofi na kazi zao ni za ndani na kufagia barabaraniMafanikio yao yasiyowahusu watu wangu hayanihusu wala kunihangaisha. Wana TATA ndiyo. Kwani hao waajiriwa elfu nane ni wamakonde wenzetu au magabacholi. Hawa jamaa wana roho mbaya na ni wabaguzi. Kuwatetea ni sawa na kutetea ukimwi kuwa ni bingwa wa kuua
Tatizo kubwa ni watu wenye asili ya Afrika nao kuwa na uwezo wa kuwa na makampuni makubwa au biashara kubwa khasa yale yanogusa maisha ya watu kama supermarkets.Mafanikio yao yasiyowahusu watu wangu hayanihusu wala kunihangaisha. Wana TATA ndiyo. Kwani hao waajiriwa elfu nane ni wamakonde wenzetu au magabacholi. Hawa jamaa wana roho mbaya na ni wabaguzi. Kuwatetea ni sawa na kutetea ukimwi kuwa ni bingwa wa kuua
Nakubaliana nawe. Wakati mifumo yetu tuliyorithi toka kwa wakoloni iliwajengea wao na wageni mazingira mazuri kwa kutunyima sisi fursa, mifumo ya nchi za Ulaya iko wazi kuwa ni kwa faida ya watu wake kwanza.Tatizo kubwa ni watu wenye asili ya Afrika nao kuwa na uwezo wa kuwa na makampuni makubwa au biashara kubwa khasa yale yanogusa maisha ya watu kama supermarkets.
Hizi biashara nyingi zina miaka zaidi ya 100 yaani wayahudi wazishika hizi biashara kwa mfano maduka ya Aldi, Lidl, Tesco ni wayahudi. Sainsburys ni wazungu, Wilko na Morrisons ni wazungu. Mabiashara mengine kama zile Malls ni familia zamiliki lakini ni biashara ambazo zilianza tangu kabla ya vita ya kwanza ya dunia.
Miaka nilokaa pale UK na Ulaya nilijifunza sana kabla ya kuamua kurudi bongoland kujaribu vibiashara vyangu vidogovidogo. Sasa hivi nimejishika uzuri maana kwa Tanzania watu hukukwambia ni lazima uonane na wenye mji ili uweze kuruhusiwa kuwa na biashara ya maana! Yaani ni lost "of nonsense" lakini ni lazima uifuate hiyo maana usipofanya hivyo utavunjiwa biashara yako.
Hivyo ukiangalia sana utaona kuwa huu ni mfumo ambao ulijikita tangu enzi ya mababu zao na waliweza kusimama kwa kukubalika. Waziri mkuu wa sasa wa UK Rishi Sunak baba yake alikuwa na duka la dawa Sunak Pharmacy miaka ya 60, hivyo Rishi Sunak asingeweza kuwa maskini leo.
Leo hii waziri wa biashara wa UK ni mwafrika kwani Kemi kwa asili atokea Nigeria na akizungumza khasa kiyoruba.
Sasa waafrika wana nafasi yoyote ya kusimama leo kwenye mabisahara haya? Jibu ni hapana kwani mifumo ilowekwa kwa zaidi ya miaka 100 ilopita ni migumu na iliwekwa kwa ajili ya watu fulani ambao nao husaidiana hadi leo.
TATA hatengenezi magari tu pia ana kampuni tanzu ambazo zingine ni kutoka India kama kampuni ya Tata Consultancy Services ambayo hutoa ushauri elekezi kwenye masuala ya Artificial Intelligence kwa wateja kadhaa barani Ulaya na mabara mengine na waingiza fedha kwelikweli.
TATA haohao washughulika na vyuma yaani wana kampuni tanzu ya TATA Steel ambayo ni kampuni tanzu ta TATA inoshughilika na kutafuta vyuma na kutengeneza vyuma hivyohivyo. Kwahiyo TATA si magari tu wana vikampuni vingi tanzu ambavyo vyaifanya TATA kuwa kampuni kubwa sana duniani.
Ila kwa Afrika khasa Tanzania yawezekana kabisa kubadili "mindset" kwa ajili ya kujenga maisha ya vizazi vijavyo kwa serikali kuandaa mazingira bora kwa wazawa na watanzania wengine kufanya biashara kubwa kwa kuwepo miundominu imara, umeme wa uhakika na kodi rafiki kwa wanoanza biashara hizo.
Bila hivyo Waafrika hatutoboi tukiwa ndani ya nchi zetu na hata tukitoka kwenda huko nje ya mipaka yetu kwa sababu sisi wenyewe tunazibiana na kurogana na kibaya zaidi kuchumiana na kuchomeana dhambi.
๐๐โNimekuwa nikija Tanzania kwa miaka 30 iliyopita, nakuja kila mwaka,
Contradiction..โKwa hiyo matunda yote haya ni kutokana na filamu ya Royal tour, ndio tunaona msanii huyu amekuja Tanzania.
Ni utapeli na ubaguzi mtupu. Kwa miaka 30 aliyokuja Tanzania anasema " "nimekuja Tanzania kwa miaka 30 sikuitangaza.... sasa nitaitangaza." Hapa ndipo unaweza kuona unafiki na utapeli wa maponjoro.๐๐
Contradiction..
Msanii anasema amekuwa akija Tz kila mwaka kwa miaka 30 sasa..
Huyo mkurugenzi anasema msanii amekuja kutokana na Royo Tua ya sa100, duh!
Waongo hawa!