Je, Uzinduzi Royal Tour ungekuwa na maana kama Rais Samia angetua kwa Dreamliner & ATC kuzindua Direct Flights from DAR-JFK-DAR/JRO-JFK-JRO?

Je, Uzinduzi Royal Tour ungekuwa na maana kama Rais Samia angetua kwa Dreamliner & ATC kuzindua Direct Flights from DAR-JFK-DAR/JRO-JFK-JRO?

Tuna Dreamliner na Airbus 2 zote ni jet engine, bombardier ya jet unakuja. kati ndege zetu 15, 5 ndio za pangaboi, 10 ni jet engine.
P

Mkuu, Mayalla, it’s more complicated than that! Air route authority is valuable; haitolewi kirahisi rahisi, kwasababu ina direct impact on the market shares of the major players. Remember, home countries of the major players in the aviation industry have bilateral treaties that essentially serve to protect the interests of the major players involved. Kwa ATCL kupewa hiyo air route authority itabidi iruke viunzi vingi.
 
Wanabodi,

Naendelea na zile makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa, makala ya Leo ikiwa ni makala ya swali la hypothetical question (swali la kufikirika), Kwa njia ya "thinking aloud", yaani unawaza kwa sauti.

Swali ni hili "Jee uzinduzi wa filamu ya Royal Tour, unaofanyikia nchini Marekani, upi ungekuwa na maslahi zaidi Kwa taifa kama Rais Samia angetua nchini Marekani kwa dege Letu la Dreamliner, huku ATC ikizindua Direct Flights from DAR-JFK-DAR/JRO-JFK-JRO? au kwenda Kwa ndege za watu, kuzindua kushangaa na kurejea, then what?.

Japo mimi sio mtaalam usafiri wa anga, lakini kusafiri nchi mbalimbali na katika misafa mbalimbali kumenipa exposure ya kutosha kuwaza kwa sauti.

Rais Samia na ujumbe wake, wako nchini Marekani, ambapo pamoja na mambo mengine, Rais Samia atafanya uzinduzi wa filamu yake ya Royal Tour.

Kwanza nitoe pongezi Kwa Sterling wa movie hiyo, mtu kuwa sterling wa movie yoyote kiukweli sii mchezo na kwa jinsi nilivyo ziona zile pati gazeti, "treilers", angekuwa ni Nyerere, asingeweza, Mwinyi, asingeweza, Mkapa ndio kabisa, na JPM asinge kubali hata huruhusu, mtu mwingine ambaye angeweza kuwa starling wa movie kama hii ni JK, tena angepatia zaidi kwa sababu ni "hechibii" kumkaribia Steven Kanumba, Will Smith, Denzel Washington or Sidney Pointer.

Uzinduzi wa Royal Tour kufanyikia Marekani, ni mahali sahihi Kwa sababu huko ndio a catchment areas za watalii wenye fedha.

Kwa mawazo yangu, kwa vile lengo , pamoja na mambo mengine, ni ku promote utalii, hakuna kitu kinacho ongoza Kwa kupromote utalii kama usafiri wa ndege wa direct flights.

Na hakuna kitu kinaitangaza nchi kimataifa kama kupeperusha bendera ya nchi moja kwenye nchi nyingine, hakuna kitu kinaipeperusha vizuri bendera ya nchi kimataifa kama the national flag carriers, yaani ndege za mashirika yakitaifa kutua viwanja vya nchi nyingine.

Hii ni mara ya pili rais Samia kwenda Marekani, mara zote anakwenda Kwa ndege za mashirika ya ndege za mashirika ya kibiashara ya nchi nyingine.

Rais Samia hasafiri safari za mbali za ndege zetu ili kukwepa gharama. Kuliamsha Dreamliner letu kutua Marekani ni gharama kubwa. Lakini kama ni kweli tumedhamiria Kwa dhati kuutangaza utalii wetu kimataifa, hatuwezi kukwepa gharama.

Tanzania na Marekani, tuna mkataba wa anga huria, hatuhitaji kuomba landing rights kwenye viwanja vyovyote vya Marekani, tunachohitaji ni kutoa tuu taarifa ili tutengewe a parking slot.

Dreamliner yetu ya Boeing 787 - 8 inabeba abiria 248 na Airbus ambapo abiria ni 240 na 8 crew. Tuki reserves nafasi 40 kwa rais na ujumbe wake, halafu tukabeba abiria 200, kila abiria alipe nauli ya US $ 5,000 kumsindikiza Mama Kuzindua Royal Tour, hao wasanii tuu wa Bongo Movies na Bongo Fleva wangeweza kuijaza. Ukijumlisha na wafanyabiashara, kampuni yangu ingepewa tender ya uhamasishaji hiyo trip, ningewapa abiria 500!.

Hivyo uzinduzi huo wa Royal Tour Nchini Marekani, would've made more sense kama Rais Samia angetua kwa Dreamliner na ATC kuzindua Direct Flights from JRO -JFK -JRO.

Hakuna kitu kizuri kama Rais Samia angetua JFK Kwa Dreamliner na kupokelewa uwanjani hapo na Watanzania waishio Marekani kisha kuja nae hadi hotel aliyofikia.

Nikisema Watanzania ni wavivu kuchangamkia fursa, nitakuwa ninawaonea?. Kama ndege tunazo, abiria tunao, na soko lipo, hivi tuliinua hii midege ya nini?. Kweli ATC wanaona raha hii midege ya long distance haul, ikiruka domestic routes huku ikibeba vile vindoo vya samaki Sato kutokea Mwanza kuja Far na kwenda KIA pekee?. Tukisema pomoja na mambo mengine yote, lakini shirika letu la ndege kuendelea kupata hasara mwaka hadi mwaka kunachangiwa na menejinent kukosa wataalamu wa strategic thinking and planning kwenye airline business?.

Nawatakia uzinduzi mwema wa Royal Tour hiyo tarehe 18 na Pasaka Njema

Wasalaam.

Paskali
Kaka pasco naomba kazi kwenye kampuni yako, kijana wako nina professional ya PR.
 
Kuingiza ndege USA direct kutoka Tanzania sio rahisi kama unavyodhani. Kenya walikua na hiyo ruhusa sijajua kwa sasa wanaendeleaje.
Kuna michakato mingi sana ya kiusalama before kupewa hicho kibali.

Nitashangaa sana kama hata hili haulifahamu.
Ni kweli kuwa na direct route to the US kuna mambo mengi ya kuhitimu hasa kiusalama. Lakini penye nia pana njia. Kenya wao waliweza, lakini wakapumzika wakati wa Corona. Na sasa wameanza tena na wanaendelea vizuri. Wao KQ pia wanarusha Dreamliner yao direct. Jumamosi May 7 nitakuwa mmoja wa abiria kwenye KQ kutoka Nairobi mpaka JFK
 
Ni kweli kuwa na direct route to the US kuna mambo mengi ya kuhitimu hasa kiusalama. Lakini penye nia pana njia. Kenya wao waliweza, lakini wakapumzika wakati wa Corona. Na sasa wameanza tena na wanaendelea vizuri. Wao KQ pia wanarusha Dreamliner yao direct. Jumamosi May 7 nitakuwa mmoja wa abiria kwenye KQ kutoka Nairobi mpaka JFK
Nakuomba siku hiyo ikitangazwa tangazo la Ku board, nakuomba simama pembeni ya boarding gate, then wahesabu abiria walio board from Dar, wewe uwe the last to board, ukifika ndani, wahesabu abiria business wao wana board from lounge na VIP, wajumlishe na wale wa economy, then get the total, ili tuwaeleze hawa vichaa wetu wa ATCL, what a wasted opportunity they are missing!. Wakenya wanatubebea watalii wetu, wanatusombea kazi zetu, kule Rombo wanatubebea wake zetu, sasa hata kwenda Marekani, wanatubebea abiria wetu!, kwenye soko la AGOA wanatuingizia bidhaa zetu, hata kwenye kuutangaza utalii wa mlima Kilimanjaro, wanatutangazia mlima wetu kuwa uko kwao, ila unapandwa upande wa Tanzania!. Watanzania tutaendelea kulala mpaka lini?.
P
 
Nakuomba siku hiyo ikitangazwa tangazo la Ku board, nakuomba simama pembeni ya boarding gate, then wahesabu abiria walio board from Dar, wewe uwe the last to board, ukifika ndani, wahesabu abiria business wao wana board from lounge na VIP, wajumlishe na wale wa economy, then get the total, ili tuwaeleze hawa vichaa wetu wa ATCL, what a wasted opportunity they are missing!. Wakenya wanatubebea watalii wetu, wanatusombea kazi zetu, kule Rombo wanatubebea wake zetu, sasa hata kwenda Marekani, wanatubebea abiria wetu!, kwenye soko la AGOA wanatuingizia bidhaa zetu, hata kwenye kuutangaza utalii wa mlima Kilimanjaro, wanatutangazia mlima wetu kuwa uko kwao, ila unapandwa upande wa Tanzania!. Watanzania tutaendelea kulala mpaka lini?.
P
P unasema kweli nilishangaa maajabu EK 726 inaondoka full. Na fikiria wale jamaa wanakomaa na DAR tu bhaasi. TZ watu wanasafir aisee...Bado Turkish, Oman, Fly Dubai, Egypt Air, KLM, Swiss Air, Rwandair, KQ, Air Zimbabwe, Uganda Airlines, Malawian Airlines,Ethiopian airlines etc
 
ATCL kwa sasa haina uwezo huo wa kupata slots ya direct flight to NY ama DC wacha mbwembwe ng’wanone
Hili ndio tatizo kubwa la sisi Watanzania, we don't believe in ourselves, always negative and negativity!. Ndege tunazo, fedha tunazo, mkataba wa anga huria tunao, tatizo lilikuwa moja tuu, kupata abiria wa kuishibisha hiyo direct flights to New York, Royal Tour inakwenda kufungua!, what else do we need?.
P
 
Hili ndio tatizo kubwa la sisi Watanzania, we don't believe in ourselves, always negative and negativity!. Ndege tunazo, fedha tunazo, mkataba wa anga huria tunao, tatizo lilikuwa moja tuu, kupata abiria wa kuishibisha hiyo direct flights to New York, Royal Tour inakwenda kufungua!, what else do we need?.
P
Hapo KQ ananuna maana ATC ikisimama ni maumivu kwake. Ona Route ya Mumbai inavyoleta Neema
 
Mkuu BRN ikianzishwa ni vyema uwepo/upewe nafasi.una mawazo mengi sana na wakupe uhuru wa kumleta yeyote ili ufanye kazi vyema.
 
Hiyo cha mtoto. Ipo ile ya Australia to US, masaa 21 non-stop.

Zamani hizo nilipanda ndege PANAM kutoka Dar Mpaka Dakar. Pale Dakar tukaconnect to New York. Kufika New York nikaambiwa safari yangu bado[ ilikuwa mara yangu ya kwanza kwenda U.S] masaa nane tena kutoka New York Mpaka Seattle!!

Sijasafiri safari ndefu namna hiyo tena!!!
 
Zamani hizo nilipanda ndege PANAM kutoka Dar Mpaka Dakar. Pale Dakar tukaconnect to New York. Kufika New York nikaambiwa safari yangu bado[ ilikuwa mara yangu ya kwanza kwenda U.S] masaa nane tena kutoka New York Mpaka Seattle!!

Sijasafiri safari ndefu namna hiyo tena!!!
Hongera sana Mkuu. Naamin kwa kusafir angalau mawazo yako si Kama ya kina Hawa vijana ambao hawajawahi kuvuka border
 
Ikawa hajazindulia Serengeti wala ngorongoro isipokuwa picha za Serengeti ..vivyo hivyo Dreamliner zetu hao wazungu wazione tu kwa picha kuwa tunazo na wakiwa na utashi zitawafuata tu
 
Hili ndio tatizo kubwa la sisi Watanzania, we don't believe in ourselves, always negative and negativity!. Ndege tunazo, fedha tunazo, mkataba wa anga huria tunao, tatizo lilikuwa moja tuu, kupata abiria wa kuishibisha hiyo direct flights to New York, Royal Tour inakwenda kufungua!, what else do we need?.
P
Mkuu bado ujajibu swali ..umesema mama alipaswa kuzindua na route na abiria ungempa kama ungepewa tenda ..Je una consistency ya kutoa hao abiria 500 kwa uzinduzi tu au kila siku ya route?Sidhani kama hao ATCL hawajaona hio fursa ukute wamechambua gharama za kuihudumia ndege kwenye hiyo route na abiria ambao wanaweza kuwapata wameona ni hasara …Tudadavulie
 
Zamani hizo nilipanda ndege PANAM kutoka Dar Mpaka Dakar. Pale Dakar tukaconnect to New York. Kufika New York nikaambiwa safari yangu bado[ ilikuwa mara yangu ya kwanza kwenda U.S] masaa nane tena kutoka New York Mpaka Seattle!!

Sijasafiri safari ndefu namna hiyo tena!!!
Mimi napenda safari za ku connect, ndege yangu ya sasa ni Quatar, wakati wa booking inaonyesha huna haraka hivyo connection ni more than 6 hours, ukifika Doha unakuwa shifted kwenye a 5 star hotel near airport na umelipwa full board. Unasafiri Kwa raha tuu.
Nikiamua kupanda KQ ni ili ku save money.
P
 
Back
Top Bottom