#COVID19 Je, Viongozi na Watendaji Serikalini wameyapuuza mapendekezo ya Kamati ya kutathmini Covid-19?

#COVID19 Je, Viongozi na Watendaji Serikalini wameyapuuza mapendekezo ya Kamati ya kutathmini Covid-19?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2012
Posts
13,171
Reaction score
23,996
Takriban wiki ya tatu tokea Kamati maalumu ya tathmini ya ugonjwa wa Corona (COVID-19) nchini kukamilisha kazi yake na kukabidhi ripoti kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Tume hiyo ilikuja na mapendekezo zaidi ya 19 ambapo mpaka sasa ukiondoa pendekezo ya kuagiza chanjo ya Corona ambalo serikali imeishalifanya, hakuna pendekezo lingine ambalo limeishafanyiwa kazi kikamilifu.

Hata pendekezo la kuvaa barakoa na kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka au vitakasa mikono halifuatwi achilia mbali kutoa takwimu za maambukizi ya ugonjwa wa Corona kwa wananchi na uhamasishaji wa chanjo kwa wananchi.

Ukichunguza hata uvaaji wa barakoa umebakia Ikulu peke yake na pindi viongozi wanapotoka Ikulu, wanazitupa barakoa kwenye geti za Ikulu! Hakuna cha social distancing hata Ikulu

Ukienda kwenye ofisi zingine za serikali, hakuna cha barakoa au maji ya kunawa/vitaka mikono.

Ukichunguza vizuri hata Rais Samia havai vizuri barakoa bali anafunika mdomo tu huku pua yake ikiwa nje ya barakoa! Ni kama anajilazimisha kuvaa barakoa ili aonekane amevaa lakini kiuhalisia hajavaa.

Mtu mwenye fikra pana atajiuliza, kulikuwa na sababu gani kwa serikali kutumia pesa kama posho kwa kamati ya watu zaidi ya 10 ambayo serikali hiyo hiyo inapuuza mapendekezo yake?

Kama hoja ilikuwa ni kuagiza chanjo ya Corona, haikuhitaji mpaka kuunda kamati ya watu zaidi ya 10 ambayo imekuja na vitabu vikubwa kama misahafu vinne vyenye mapendekezo ambayo ni pendekezo moja tu mpaka sasa ndilo limefanyiwa kazi. Ni kama ulikuwa ni usanii fulani ambao matokeo yake yalikuwa yanajulikana bali kilichokuwa kinatafutwa ni uhalalisho wa kuagiza chanjo ya corona na kukopa pesa za kukabiliana na ''janga la Corona''.

Kuagiza chanjo hakukuhitaji tume ya watu zaidi ya 10 bali kilichohitajika kwanza ni elimu ya corona kwa watanzania.

Ni ukweli kuwa mapendekezo ya Kamati ya Corona yamepokelewa kwa hisia hasi na watanzania wengi.

Kwa sasa tunakuwa na serikali ambayo inatoa ishara zisizoeleweka kwa wananchi kwa sababu viongozi hawana ujumbe/mwelekeo mmoja kwa wananchi kuhusu suala la Corona.

Serikali wanatakiwa watuambia kama Corona ipo na tujiandae kwa chanjo au watuambia corona haipo na chanjo iwe kwa wasafiri wa nje ya nchi.

Serikali kukaa kimya hakuwezi kuondoa ''tatizo'' ambalo kiuhalisia wameliasisi wao wenyewe baada ya kuunda Kamati ya Corona.
 
Hiyo Kamati ya Corona kwa mtazamo wangu ingependeza iundwe wakati ule wa mwendazake wakati Corona ilikuwa inamaliza watu haswa, hasa baada ya kuibuka kile kirusi toka SA.

Pale ndio ingefaa hiyo kamati ije na hayo mapendekezo ya kuvaa barakoa na mengine kwasababu kweli wananchi walikuwa kwenye allert na huo ugonjwa kutokana na taarifa za vifo zilivyokuwa zinatoka kila dakika, mara profesa fulani kaondoka, mara daktari fulani.

Sasa hivi tension kuhusu Corona imeshuka sana, hata kama ugonjwa bado upo, lakini kwa ujumla sio kwa kiwango kile cha mwanzo, hivyo kuhimiza watu wavae barakoa wakuelewe lazima pawepo na taarifa nyingine za kuthibitisha ugonjwa bado upo na unaua, lakini kusema tu ugonjwa upo wakati mtaani pamepoa inakuwa ngumu kueleweka.

Ndio maana hata huko serikalini unaona wanaovaa barakoa ni wale wa ikulu tu, tena hawavai muda wote, tukio fulani kavaa tukio linalofuata hajavaa; mawaziri, manaibu wao, makatibu wakuu na wengine wote hadi kule bungeni hakuna tena anaevaa barakoa kwa sasa, hiyo kamati ni kama inepoteza pesa tu.
 
Watu wanaujua ukweli, sema mama alipotoka Kenya alipewa matango poli na Kenyatta na rais kivuli Jakaya.

Huo ni uvaaji barakoa kuridhisha watu fulani, mama mwenyewe anajua ila unafiki wake unamsumbua.

The most wanted alipokufa, na Tanzia zikaisha bongo, ndo ujue rogue elements walivyoweza kumfrastrate Magu mpka akafa. Kwa akili za kawaida tu, kigogo2014 hapati tena siri za ikulu, hii inatupa uhakika kuwa ile timu tajwa imeshakompromise na mama tayari, maana mzee anatawala saizi, na interests zake wanazipata, then kwanini waendelee kumsumbua?

RIP MAGU, TUMEKUMIC HATARI
 
Watu wanaujua ukweli, sema mama alipotoka Kenya alipewa matango poli na Kenyatta na rais kivuli Jakaya.

Huo ni uvaaji barakoa kuridhisha watu fulani, mama mwenyewe anajua ila unafiki wake unamsumbua.
Watanzania unaweza kuwaita kwa majina yoyote lakini ukweli wa corona wanaujua vizuri! Ukweli ni kuwa ugonjwa huwa haufichwi!

Kwa sasa serikali wako njia panda kuhusu namna ya kuwahamasisha watanzania wengi kama sio wote ili wapate chanjo!
 
Malinzi ya Legacy ya Mwendazake yapo kazini Lindoni.

Covid ilikuja Purposely kutuondolea yule agent wa Lucifer.
 
Unategemea viongozi walewale waliokuwa wanahimiza mambo ya tangawizi,vitunguu swaumu pamoja na malimao ambao ndiyo haohao wapo madarakani sasa hivi waanze kuhimiza mambo ya kuvaa barakoa?

Tunavyosema kuwa Samia ni Rais wa hovyo huwa hatumuonei ila huwa tunamaanisha mambo kama haya.Wale viongozi wa malimao na tangawizi walipaswa kuwekwa pembeni wote but she didn't!
 
Watu wanaujua ukweli, sema mama alipotoka Kenya alipewa matango poli na Kenyatta na raisi kivuli Jakaya.
Huo ni uvaaji barakoa kuridhisha watu fulani, mama mwenyewe anajua ila unafiki wake unamsumbua.
Magu kafa kwa ujinga wake mwenyewe, msisingizie watu.
 
Unategemea viongozi walewale waliokuwa wanahimiza mambo ya tangawizi,vitunguu swaumu pamoja na malimao ambao ndiyo haohao wapo madarakani sasa hivi waanze kuhimiza mambo ya kuvaa barakoa?
Si huwa mnahubiri kwamba sasa akili zimewarudia.
 
Watu wanaujua ukweli, sema mama alipotoka Kenya alipewa matango poli na Kenyatta na raisi kivuli Jakaya.

Huo ni uvaaji barakoa kuridhisha watu fulani, mama mwenyewe anajua ila unafiki wake unamsumbua....
Huu mtazamo mnaotaka kuuleta kuonesha kwamba Corona ilikuwepo kama mpango fulani wa kufanya Magufuli aonekane anakosea kwa ule msimamo wake naupinga sana.

Corona inakuja kwa phase, ilikuja phase ya kwanza ikaua watu mwenyewe akaenda kujificha Chato, amekaa kule karibia miezi miwili haonekani mjini, then ikapoa akaibuka.

Ilipokuja phase ya pili (variant from SA) hii ndio ikaua wengi zaidi wakiwemo wasaidizi wake kina Kijazi na yeye mwenyewe (hata kama alikufa kwa moyo, lakini Corona inaua zaidi wenye magonjwa makubwa), na wale masista na mapadri wa Kanisa Katoliki waliokufa kwa wingi mpaka Kanisa likaamua kuwaambia waumini wake wajikinge.

Wakati huo Magufuli yuko busy kuaminisha watu Tanzania hakuna Corona baadae mwenyewe kuona hali inazidi kuwa mbaya akasema ipo kidogo, sasa nyie mnaoibuka leo na kusema Corona ilitumiwa kama njia ya kufanya Magufuli aonekane hafai hamjielewi, mnaficha ukweli either makusudi, au kwa kutokujua.
 
Hiyo Kamati ya Corona kwa mtazamo wangu ingependeza iundwe wakati ule wa mwendazake wakati Corona ilikuwa inamaliza watu haswa, hasa baada ya kuibuka kile kirusi toka SA
Taratibu Corona inaanza kuzoeleka na tension kuanza kupungua. Ukiangalia nchi mbalimbali zimeanza kupunguza masharti yaliyokuwa yamewekwa kama vile lockdown na hata kupeleka utalii kuanza kuruhusiwa.
 
Takriban wiki ya tatu tokea Kamati maalumu ya tathmini ya ugonjwa wa corona (Covid-19) nchini kukamilisha kazi yake na kukabidhi ripoti kwa Rais Samia Suluhu Hassan...
Kuna rafiki yangu yupo idara nyeti alinitonya mapema kwamba Mama anataka kuleta chanjo ila hataki kufanya tu out of nowhere. Hivyo kamati aliyounda ilikua ni justification Tu. Lengo haswa ni kuleta chanjo.

P.S: Kwa namna ambavyo mapendekezo mengine yanapuuzwa, pengine kuna ukweli.
 
Back
Top Bottom