#COVID19 Je, Viongozi na Watendaji Serikalini wameyapuuza mapendekezo ya Kamati ya kutathmini Covid-19?

#COVID19 Je, Viongozi na Watendaji Serikalini wameyapuuza mapendekezo ya Kamati ya kutathmini Covid-19?

Hiyo Kamati ya Corona kwa mtazamo wangu ingependeza iundwe wakati ule wa mwendazake wakati Corona ilikuwa inamaliza watu haswa, hasa baada ya kuibuka kile kirusi toka SA.

Pale ndio ingefaa hiyo kamati ije na hayo mapendekezo ya kuvaa barakoa na mengine kwasababu kweli wananchi walikuwa kwenye allert na huo ugonjwa kutokana na taarifa za vifo zilivyokuwa zinatoka kila dakika, mara profesa fulani kaondoka, mara daktari fulani.

Sasa hivi tension kuhusu Corona imeshuka sana, hata kama ugonjwa bado upo, lakini kwa ujumla sio kwa kiwango kile cha mwanzo, hivyo kuhimiza watu wavae barakoa wakuelewe lazima pawepo na taarifa nyingine za kuthibitisha ugonjwa bado upo na unaua, lakini kusema tu ugonjwa upo wakati mtaani pamepoa inakuwa ngumu kueleweka.

Ndio maana hata huko serikalini unaona wanaovaa barakoa ni wale wa ikulu tu, tena hawavai muda wote, tukio fulani kavaa tukio linalofuata hajavaa; mawaziri, manaibu wao, makatibu wakuu na wengine wote hadi kule bungeni hakuna tena anaevaa barakoa kwa sasa, hiyo kamati ni kama inepoteza pesa tu.
Mtaani hakujawahi kuwa na taharuki ya corona ni pamepoa hivi hivi muda wote na ndio maana hakuna tofauti yeyote mtaani kati ya kipindi hicho unachosema watu walikuwa wanakufa sana na sasa hivi.
 
Malinzi ya Legacy ya Mwendazake yapo kazini Lindoni

Covid ilikuja Purposely kutuondolea yule agent wa Lucifer

Sasa kulikuwa na umuhimu gani wa kuunda kamati ya corona wakati malengo ya corona yalikuwa yamekamilika!
 
Watu wanaujua ukweli, sema mama alipotoka Kenya alipewa matango poli na Kenyatta na rais kivuli Jakaya.

Huo ni uvaaji barakoa kuridhisha watu fulani, mama mwenyewe anajua ila unafiki wake unamsumbua.

The most wanted alipokufa, na Tanzia zikaisha bongo, ndo ujue rogue elements walivyoweza kumfrastrate Magu mpka akafa. Kwa akili za kawaida tu, kigogo2014 hapati tena siri za ikulu, hii inatupa uhakika kuwa ile timu tajwa imeshakompromise na mama tayari, maana mzee anatawala saizi, na interests zake wanazipata, then kwanini waendelee kumsumbua?

RIP MAGU, TUMEKUMIC HATARI
Pole baba 😭😭😭😭
 
Aliyekufa na corona ni Maalim seif, mbona mnalazimisha hili suala la Magufuli kufa na corona? Maalim seif alijitangaza kabisa kuwa anaumwa corona na hakupona hadi kifo kinamkuta ila huyo Magufuli sijui hata kinachowafanya mseme kafa na corona ni kipi?
Kufa kwa Kikazi kunapelekea watu kuamini watakavyo. Serekali haisemi ukweli, hivyo watu wanajiongeza.
 
Takriban wiki ya tatu tokea Kamati maalumu ya tathmini ya ugonjwa wa Corona (COVID-19) nchini kukamilisha kazi yake na kukabidhi ripoti kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Tume hiyo ilikuja na mapendekezo zaidi ya 19 ambapo mpaka sasa ukiondoa pendekezo ya kuagiza chanjo ya Corona ambalo serikali imeishalifanya, hakuna pendekezo lingine ambalo limeishafanyiwa kazi kikamilifu.

Hata pendekezo la kuvaa barakoa na kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka au vitakasa mikono halifuatwi achilia mbali kutoa takwimu za maambukizi ya ugonjwa wa Corona kwa wananchi na uhamasishaji wa chanjo kwa wananchi.

Ukichunguza hata uvaaji wa barakoa umebakia Ikulu peke yake na pindi viongozi wanapotoka Ikulu, wanazitupa barakoa kwenye geti za Ikulu! Hakuna cha social distancing hata Ikulu

Ukienda kwenye ofisi zingine za serikali, hakuna cha barakoa au maji ya kunawa/vitaka mikono.

Ukichunguza vizuri hata Rais Samia havai vizuri barakoa bali anafunika mdomo tu huku pua yake ikiwa nje ya barakoa! Ni kama anajilazimisha kuvaa barakoa ili aonekane amevaa lakini kiuhalisia hajavaa.

Mtu mwenye fikra pana atajiuliza, kulikuwa na sababu gani kwa serikali kutumia pesa kama posho kwa kamati ya watu zaidi ya 10 ambayo serikali hiyo hiyo inapuuza mapendekezo yake?

Kama hoja ilikuwa ni kuagiza chanjo ya Corona, haikuhitaji mpaka kuunda kamati ya watu zaidi ya 10 ambayo imekuja na vitabu vikubwa kama misahafu vinne vyenye mapendekezo ambayo ni pendekezo moja tu mpaka sasa ndilo limefanyiwa kazi. Ni kama ulikuwa ni usanii fulani ambao matokeo yake yalikuwa yanajulikana bali kilichokuwa kinatafutwa ni uhalalisho wa kuagiza chanjo ya corona na kukopa pesa za kukabiliana na ''janga la Corona''.

Kuagiza chanjo hakukuhitaji tume ya watu zaidi ya 10 bali kilichohitajika kwanza ni elimu ya corona kwa watanzania.

Ni ukweli kuwa mapendekezo ya Kamati ya Corona yamepokelewa kwa hisia hasi na watanzania wengi.

Kwa sasa tunakuwa na serikali ambayo inatoa ishara zisizoeleweka kwa wananchi kwa sababu viongozi hawana ujumbe/mwelekeo mmoja kwa wananchi kuhusu suala la Corona.

Serikali wanatakiwa watuambia kama Corona ipo na tujiandae kwa chanjo au watuambia corona haipo na chanjo iwe kwa wasafiri wa nje ya nchi.

Serikali kukaa kimya hakuwezi kuondoa ''tatizo'' ambalo kiuhalisia wameliasisi wao wenyewe baada ya kuunda Kamati ya Corona.
Unashabikia kitu ambacho hakipo na unajua fika kuwa kamati ya corona ilitupiga fix la mwaka!!
 
Takriban wiki ya tatu tokea Kamati maalumu ya tathmini ya ugonjwa wa Corona (COVID-19) nchini kukamilisha kazi yake na kukabidhi ripoti kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Tume hiyo ilikuja na mapendekezo zaidi ya 19 ambapo mpaka sasa ukiondoa pendekezo ya kuagiza chanjo ya Corona ambalo serikali imeishalifanya, hakuna pendekezo lingine ambalo limeishafanyiwa kazi kikamilifu.

Hata pendekezo la kuvaa barakoa na kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka au vitakasa mikono halifuatwi achilia mbali kutoa takwimu za maambukizi ya ugonjwa wa Corona kwa wananchi na uhamasishaji wa chanjo kwa wananchi.

Ukichunguza hata uvaaji wa barakoa umebakia Ikulu peke yake na pindi viongozi wanapotoka Ikulu, wanazitupa barakoa kwenye geti za Ikulu! Hakuna cha social distancing hata Ikulu

Ukienda kwenye ofisi zingine za serikali, hakuna cha barakoa au maji ya kunawa/vitaka mikono.

Ukichunguza vizuri hata Rais Samia havai vizuri barakoa bali anafunika mdomo tu huku pua yake ikiwa nje ya barakoa! Ni kama anajilazimisha kuvaa barakoa ili aonekane amevaa lakini kiuhalisia hajavaa.

Mtu mwenye fikra pana atajiuliza, kulikuwa na sababu gani kwa serikali kutumia pesa kama posho kwa kamati ya watu zaidi ya 10 ambayo serikali hiyo hiyo inapuuza mapendekezo yake?

Kama hoja ilikuwa ni kuagiza chanjo ya Corona, haikuhitaji mpaka kuunda kamati ya watu zaidi ya 10 ambayo imekuja na vitabu vikubwa kama misahafu vinne vyenye mapendekezo ambayo ni pendekezo moja tu mpaka sasa ndilo limefanyiwa kazi. Ni kama ulikuwa ni usanii fulani ambao matokeo yake yalikuwa yanajulikana bali kilichokuwa kinatafutwa ni uhalalisho wa kuagiza chanjo ya corona na kukopa pesa za kukabiliana na ''janga la Corona''.

Kuagiza chanjo hakukuhitaji tume ya watu zaidi ya 10 bali kilichohitajika kwanza ni elimu ya corona kwa watanzania.

Ni ukweli kuwa mapendekezo ya Kamati ya Corona yamepokelewa kwa hisia hasi na watanzania wengi.

Kwa sasa tunakuwa na serikali ambayo inatoa ishara zisizoeleweka kwa wananchi kwa sababu viongozi hawana ujumbe/mwelekeo mmoja kwa wananchi kuhusu suala la Corona.

Serikali wanatakiwa watuambia kama Corona ipo na tujiandae kwa chanjo au watuambia corona haipo na chanjo iwe kwa wasafiri wa nje ya nchi.

Serikali kukaa kimya hakuwezi kuondoa ''tatizo'' ambalo kiuhalisia wameliasisi wao wenyewe baada ya kuunda Kamati ya Corona.
Unashabikia kitu ambacho hakipo na unajua fika kuwa kamati ya corona ilitupiga fix la mwaka!!9
 
Takriban wiki ya tatu tokea Kamati maalumu ya tathmini ya ugonjwa wa Corona (COVID-19) nchini kukamilisha kazi yake na kukabidhi ripoti kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Tume hiyo ilikuja na mapendekezo zaidi ya 19 ambapo mpaka sasa ukiondoa pendekezo ya kuagiza chanjo ya Corona ambalo serikali imeishalifanya, hakuna pendekezo lingine ambalo limeishafanyiwa kazi kikamilifu.

Hata pendekezo la kuvaa barakoa na kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka au vitakasa mikono halifuatwi achilia mbali kutoa takwimu za maambukizi ya ugonjwa wa Corona kwa wananchi na uhamasishaji wa chanjo kwa wananchi.

Ukichunguza hata uvaaji wa barakoa umebakia Ikulu peke yake na pindi viongozi wanapotoka Ikulu, wanazitupa barakoa kwenye geti za Ikulu! Hakuna cha social distancing hata Ikulu

Ukienda kwenye ofisi zingine za serikali, hakuna cha barakoa au maji ya kunawa/vitaka mikono.

Ukichunguza vizuri hata Rais Samia havai vizuri barakoa bali anafunika mdomo tu huku pua yake ikiwa nje ya barakoa! Ni kama anajilazimisha kuvaa barakoa ili aonekane amevaa lakini kiuhalisia hajavaa.

Mtu mwenye fikra pana atajiuliza, kulikuwa na sababu gani kwa serikali kutumia pesa kama posho kwa kamati ya watu zaidi ya 10 ambayo serikali hiyo hiyo inapuuza mapendekezo yake?

Kama hoja ilikuwa ni kuagiza chanjo ya Corona, haikuhitaji mpaka kuunda kamati ya watu zaidi ya 10 ambayo imekuja na vitabu vikubwa kama misahafu vinne vyenye mapendekezo ambayo ni pendekezo moja tu mpaka sasa ndilo limefanyiwa kazi. Ni kama ulikuwa ni usanii fulani ambao matokeo yake yalikuwa yanajulikana bali kilichokuwa kinatafutwa ni uhalalisho wa kuagiza chanjo ya corona na kukopa pesa za kukabiliana na ''janga la Corona''.

Kuagiza chanjo hakukuhitaji tume ya watu zaidi ya 10 bali kilichohitajika kwanza ni elimu ya corona kwa watanzania.

Ni ukweli kuwa mapendekezo ya Kamati ya Corona yamepokelewa kwa hisia hasi na watanzania wengi.

Kwa sasa tunakuwa na serikali ambayo inatoa ishara zisizoeleweka kwa wananchi kwa sababu viongozi hawana ujumbe/mwelekeo mmoja kwa wananchi kuhusu suala la Corona.

Serikali wanatakiwa watuambia kama Corona ipo na tujiandae kwa chanjo au watuambia corona haipo na chanjo iwe kwa wasafiri wa nje ya nchi.

Serikali kukaa kimya hakuwezi kuondoa ''tatizo'' ambalo kiuhalisia wameliasisi wao wenyewe baada ya kuunda Kamati ya Corona.
Hahaha, unategemea nani atoke mbele atubadilisha,walikosea tangu mwanzo, na hii chanjo haitafua dafu.
Wazir wa afya alituaminisha kuishi kwa nyunyu mashine ya kupiga nyungu ikafungwa, yeye alipiga nyungu live akiwa na bebi yake,hatukuaminishwa kuvaa Barakoa, hatukuambiwa wagonjwa waliokufa kwa covid-19. Utakuwa unafik wakija kutuambia.
 
Watu wanaujua ukweli, sema mama alipotoka Kenya alipewa matango poli na Kenyatta na rais kivuli Jakaya.

Huo ni uvaaji barakoa kuridhisha watu fulani, mama mwenyewe anajua ila unafiki wake unamsumbua.

The most wanted alipokufa, na Tanzia zikaisha bongo, ndo ujue rogue elements walivyoweza kumfrastrate Magu mpka akafa. Kwa akili za kawaida tu, kigogo2014 hapati tena siri za ikulu, hii inatupa uhakika kuwa ile timu tajwa imeshakompromise na mama tayari, maana mzee anatawala saizi, na interests zake wanazipata, then kwanini waendelee kumsumbua?

RIP MAGU, TUMEKUMIC HATARI
Si aliteua karibu watu wa kwao na ndiyo walikuwa wanamlinda
 
Hahaha, unategemea nani atoke mbele atubadilisha,walikosea tangu mwanzo, na hii chanjo haitafua dafu.
Wazir wa afya alituaminisha kuishi kwa nyunyu mashine ya kupiga nyungu ikafungwa, yeye alipiga nyungu live akiwa na bebi yake,hatukuaminishwa kuvaa Barakoa, hatukuambiwa wagonjwa waliokufa kwa covid-19. Utakuwa unafik wakija kutuambia.
Gwajina hafai kuwa waziri hata kwa dak moja
 
Huu mtazamo mnaotaka kuuleta kuonesha kwamba Corona ilikuwepo kama mpango fulani wa kufanya Magufuli aonekane anakosea kwa ule msimamo wake naupinga sana.

Corona inakuja kwa phase, ilikuja phase ya kwanza ikaua watu mwenyewe akaenda kujificha Chato, amekaa kule karibia miezi miwili haonekani mjini, then ikapoa akaibuka.

Ilipokuja phase ya pili (variant from SA) hii ndio ikaua wengi zaidi wakiwemo wasaidizi wake kina Kijazi na yeye mwenyewe (hata kama alikufa kwa moyo, lakini Corona inaua zaidi wenye magonjwa makubwa), na wale masista na mapadri wa Kanisa Katoliki waliokufa kwa wingi mpaka Kanisa likaamua kuwaambia waumini wake wajikinge.

Wakati huo Magufuli yuko busy kuaminisha watu Tanzania hakuna Corona baadae mwenyewe kuona hali inazidi kuwa mbaya akasema ipo kidogo, sasa nyie mnaoibuka leo na kusema Corona ilitumiwa kama njia ya kufanya Magufuli aonekane hafai hamjielewi, mnaficha ukweli either makusudi, au kwa kutokujua.
Mawazo lazima kuwepo na mkinzano wa kimawazo, Mimi nadhani kila mmoja Yuko Sawa Kwa kuwa kila mtu Hana uhakika wa alichosimamia!!

Yote yanaweza kuwa Sawa, Kwa kuwa pia anayewaza hivyo kinyume na mawazo yako mkuu, anazo sababu za Kwa nini ameamua kusimamia hapo, lakini pia kwako vilevile,

Ni nini cha kufanya mshindi awe mmoja pekee Kati ya mawazo haya tofautitofauti miongoni mwa Watanzania, ni labda kuliacha hivyohivyo ili kila mtu aamini anavyoweza, ama kufanyike uchunguzi huru, Kwamba Kwa nini huyu na Yule wanatofautiana juu ya tukio Hilo??
 
Kufa kwa Kikazi kunapelekea watu kuamini watakavyo. Serekali haisemi ukweli, hivyo watu wanajiongeza.
Watu kuamini watakavyo huwezi kuzuia ila mtu akileta humu hizo imani zake inabidi atoe sababu za msingi, sijawahi kuona mtu akitoa sababu ya msingi kwanini afikirie kuwa Magufuli kafa kwa corona?
 
Kwenye suala corona ni kweli, serikali haieleweki!
Duuu, hapa kazi ipo. Waumini wa watu na Sio mfumo.
Watu kuamini watakavyo huwezi kuzuia ila mtu akileta humu hizo imani zake inabidi atoe sababu za msingi, sijawahi kuona mtu akitoa sababu ya msingi kwanini afikirie kuwa Magufuli kafa kwa corona?

Sababu za msingi zipo, ila zinapishana na unachoamini.
 
Watu kuamini watakavyo huwezi kuzuia ila mtu akileta humu hizo imani zake inabidi atoe sababu za msingi, sijawahi kuona mtu akitoa sababu ya msingi kwanini afikirie kuwa Magufuli kafa kwa corona?
Mkuu, Mimi bado naziamini hoja zote zinazo ongoza humu kuhusu hayati JPM, naziamini Kwa sababu kila mtu anahoja nzito na inahitaji majibu ya kina,

Wale wenye Mashaka na namna alivyotuaga, wako na sababu zao na hoja zao sio tu mtu uwaropokee na kuwakaripia wakati ukiwajibu, lakini pia Kwa hao wengine wanaoamini kinyume na wenye msimamo wa mashaka juu ya kutuaga kwake JPM, Wana hoja vilevile na huwezi tu kukaa unawatukana Kwa sababu ya intereste za hao wenye msimamo mwingine

Na ili kuondoa hii misimami miwili tofauti, ni ama ibaki hivi hivi Kwa kuwa hawezi kuwepo mshindi juu ya hilo, na endapo kunahitajika apatikane mshindi wa hoja mbili kinzani hizi, basi uchunguzi ni wa lazima, tena uwe ni uchunguzi huru kutoka huko Kwa wasioweza kuhongwa
 
Back
Top Bottom