Mbona huoni unbalance ya maendeleo kati ya mikoa ya kusini na kaskazini?
Wachagga wameiba wakaweka maendeleo kwao mkoa wa Kilimanjaro angalia miundo mbinu ya Mtwara,Lindi,Ruvuma,Rukwa,Tabora,Kigoma je hao wachagga ambao wapo kwenye system za uongozi wameitendea nini mikoa hiyo?Zaidi ya kupora mabilioni na kuinemeesha mikoa ya kaskazini kwenu huko.
Ili nchi hii iendelee inabidi wachagga wakae kando kwenye system kwani kila idara ukienda wameenea.
Mbona huoni unbalance ya maendeleo kati ya mikoa ya kusini na kaskazini?
Wachagga wameiba wakaweka maendeleo kwao mkoa wa Kilimanjaro angalia miundo mbinu ya Mtwara,Lindi,Ruvuma,Rukwa,Tabora,Kigoma je hao wachagga ambao wapo kwenye system za uongozi wameitendea nini mikoa hiyo?Zaidi ya kupora mabilioni na kuinemeesha mikoa ya kaskazini kwenu huko.
Ili nchi hii iendelee inabidi wachagga wakae kando kwenye system kwani kila idara ukienda wameenea.
wasukuma si wakabila na hawajipendelei kama wachagga.
.. Juzi mramba alipokuwa anatoa mchango wake bungeni, alizema ili tanzania tuweze kuendelea tunatakiwa tuwe na miundombinu ya barabara ambayo itaunganisha vijiji, kata, wilaya, mikoa na mwisho nchi nzima. hutu akitolea mfano kwa madoido kwamba, jimboni kwake wamefanikiwa hilo, kwani wanabarabara nzuri. zaidi ya hapo alionyesha hata sehemu ya kupata fedha kujengea barabara hizo. huku akisahau kwamba, alipokuwa akijenga barabara za kwake, huku akiwa waziri katika nchi hii, akiacha sehemu nyingine. je huu sio ubaguzi ambao anaouzungumzia mwanakjj? hatuwezi kuzungumzi hili, kwani bila usawa hakuna haki.
.. Juzi mramba alipokuwa anatoa mchango wake bungeni, alizema ili tanzania tuweze kuendelea tunatakiwa tuwe na miundombinu ya barabara ambayo itaunganisha vijiji, kata, wilaya, mikoa na mwisho nchi nzima. hutu akitolea mfano kwa madoido kwamba, jimboni kwake wamefanikiwa hilo, kwani wanabarabara nzuri. zaidi ya hapo alionyesha hata sehemu ya kupata fedha kujengea barabara hizo. huku akisahau kwamba, alipokuwa akijenga barabara za kwake, huku akiwa waziri katika nchi hii, akiacha sehemu nyingine. je huu sio ubaguzi ambao anaouzungumzia mwanakjj? hatuwezi kuzungumzi hili, kwani bila usawa hakuna haki.
Tonga.. unachokiona hapa na mawazo ambayo yanatolewa dhidi ya Wachagga yapo na kuna watu wanaamini kabisa wanachosema. Nina uhakika siyo tu umeshtushwa na baadhi ya maneno lakini pia umehuzunishwa kuwepo kwa maneno hayo.
Haya mambo tumekuwa tukiyakwepa kuyazungumzia au kuyacknowledge kuwa yapo. Mada hii siyo tu imeendelea kunithibitishia kuwa kuna watu wana chuki kali kweli na isiyo na msingi dhidi ya Wachagga lakini pia imenifanya nielewe kwa namna fulani sentiments zinazoweza kuwa zimechangia hisia hizo.
Kama jamii ni lazima tupinge kwa nguvu zetu zote wale wanaoeneza sumu ya ukabila, udini, urangi kwa ajili ya kupata manufaa ya kisiasa au ya kinamna yoyote ile. Wakati huo huo tusije kufanya mambo yetu bila kuangalia jinsi gani mambo hayo yanaweza kutafsirika vibaya.
Ndio maana kwa upande wangu linapokuja suala la Chadema kwa mfano, tatizo ninaloliona lilitokea katika suala la wagombea wa viti maalumu ni suala la utaratibu na mchakato wa jinsi gani hao wanapatikana. Jambo hilo nasikia hata wao wanafahamu ndio maana baada ya mabadiliko ya Katiba yao ya 2006 waliamua kubadili jinsi wanavyofanya uteuzi wa wabunge wa viti maalumu.
Hili pia linatokea katika nafasi mbalimbali za uongozi au utumishi ambapo ninachokiona kama tatizo kubwa si ukabila bali undugunization uliokithiri kutokana na utaratibu mbaya wa kupata ajira na madaraka nchini. Ni kwa sababu hiyo utaona mngoni aliyepata nafasi atahakikisha watoto wake na wenyewe wanaingia kwenye eneo hilo, au akawapa habari za ndani zenye faida watu wa "kwao" na wakapata unfair advantage ya mambo fulani. Hili linatokea kwa karibu makabila yote.
Tatizo kubwa wakati mwingine ni suala la taratibu zilizowazi, huru, na fair kwa mtu yeyote. Endapo, inatangazwa nafasi, kwa uwazi, na huru na nafasi hiyo ikatokewa kugombewa na na watu kadhaa basi lazima tujifunze kukubali matokeo yake hata kama hatupendi yawe hivyo.
Tusikubali kuongozwa na hisia kinyume (negative emotions) kwa sababu hatuoni tunachotaka kuona. Tusilazimishwe kuona kitu ambacho hakipo kama alivyofanya Wangwe hivi karibuni.
Lakini ukweli utaendelea kubakia Watanzania siyo binadamu tofauti na wengine kiasi kwamba hawana mawazo ya kibaguzi ati tu kwa vile ni wa Tanzania. Mawazo haya yapo, yanachochewa na wakati mwingine yanatukuzwa. Ni jukumu la kila mtanzania kuhakikisha siyo tu anapinga mawazo ya kuchochea ukabila, lakini pia kupinga dalili zozote za ukabila zinapojitokeza hata kama zinahusu kabila lake au watu wa jamii yake.
Ni tutakapofanya hivyo ndipo tutakuwa kweli tunajenga Taifa la watu "walio huru, sawa, na wenye kufurahia haki zote za msingi sawasawa katika Taifa lao".
nilikuwa na imani kubwa sana kwako mkuu M.M.MA MODEST PROPOSAL
Na. M. M. Mwanakijiji
Kuna vumbi la chuki, fitina, wivu, kisasi, na hisia za kibaguzi dhidi ya jamii ya Wachagga nchini. Kuna kila dalili kuwa jamii ya Wachagga nchini siyo tu inaanza kutengwa lakini uwepo wake katika nafasi mbalimbali za uongozi inazua hoja ya ukabila kwa haraka zaidi yawezekana kuliko kabila jingine lolote nchini. Katika Tanzania yetu, wachagga wameanza kunyoshewa kidole siyo kwa siri tena bali kwa wazi kabisa tena na watu ambao wakati mwingine hawapati hata kigugumizi.
Ubaguzi huo msingi wake mkubwa ni idadi ya wachagga katika nafasi mbalimbali za uongozi na hasa kuhusiana na elimu yao. Kuanzia mara tu baada ya uhuru jamii ya wachagga mojawapo ya jamii ambayo watu wake wengi wamesoma sana na kufanikiwa kielimu na kiuchumi imekuwa ikinyoshewa kidole cha kupendelewa.
Mtu yeyote ambaye anaweza akafanya uchambuzi yakinifu hatoshangaa kukuta wataalamu wa kichagga katika nafasi mbalimbali za uongozi au taaluma nchini. Kwenye vyuo vikuu, kwenye idara za serikali na hata kwenye taasisi binafsi kumejaa watu wenye asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hususan watu wa jamii ya Kichagga.
Endapo itatangazwa nafasi yoyote ya kitaalamu usishangazwe ukiona kuwa waombaji wengi wana majina ya "Kichagga".
Ni kwa sababu hiyo basi kuna kila dalili kuwa kutokana na wingi wao katika nafasi muhimu na vyeo mbalimbali (hata ndani ya Jeshi la Polisi) Wachagga siyo tu ni wengi lakini wanaonekana kufanikiwa zaidi. Hili ni tishio kwa baadhi ya watu. Ni tishio kwa watu ambao hawako tayari kuangalia jitihada za watu katika kufanikiwa kwao na matokeo yake kushutumu ukabila kila idadi ya Wachagga kwenye kitengo fulani inazidi mmoja.
Ushauri wangu ni kuwa, kwa vile Wachagga wameshasoma sana na kuendelea katika biashara karibu mikoa mingi nchini. Na kwa vile wanaendelea kufanikiwa pia katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini, basi itakuwa vizuri kama watajitolea kuachilia nafasi hizo ili kuwapa nafasi watu wa makabila mengine.
Kwa vile ni wao wanaonekana kulalamikiwa kutokana na mambo ya kifisadi aidha kwa moja kwa moja au kwa kuashiria basi ni vizuri wawape watu wengine nafasi hizo hata kama watu hao hawajasoma sana. Hii yote itakuwa ni katika kudumisha mshikamano, umoja na udugu wa Taifa letu.
Endapo Wachagga wataachilia nafasi mbalimbali kama UCEO, Ukurugenzi, Ukuu wa Idara n.k watasababisha watu wawapende na kuwakubali kuwa ni wazalendo wa kweli. Sitoshangaa kuwa ndugu zetu wa Jamii ya Kichagga wakikaa pembeni, basi ufisadi utakoma serikalini, idara zitaongozwa na watu wazuri, na mara moja na daima Tanzania itaanza kukua katika uongozi.
Kwa kupendekeza nashauri wabunge wote ambao ni Wachagga au wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro kuachia ngazi mara moja ili watu wa makabila mengine wapewe nafasi hizo. Siyo wao tu bali pia wabunge ambao wameoa au kuolewa uchagani vile vile wafuate nyazo hizo.
Wakishamaliza hao, wakuu wote wa idara za serikali ambao wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hasa wa jamii ya kichagga (wamarangu, wamachame, wa Rombo, na wa Kibosho) na wao waamue kuachilia nafasi hizo kwa ndugu zao Wamakua, Wamwera, Wa Ndali, Wadigo n.k Katika hili Wapare hawahusishwi.
Tukishamaliza wakuu hao wa idara za serikali ningependekeza madaktari wote wenye kumiliki hospitali binafsi ambao ni wachagga au wameoa/kuolewa uchagani na wenyewe waamue kuingia ubia na watu wa makabila mengine kama wangengereko, wambuu, na wanjiro ili hayo makabila madogo na wenyewe wapate nafasi ya kujifunza fani hizi muhimu.
Zaidi ya yote, majaji na mahakimu wote ambao wana asili ya Uchaggani na wenyewe waamue kujitoa katika nafasi hizo kwani wingi wao pia unaonekana sana na hivyo kuwa kikwako kwa watu wa makabila mengine kufanikiwa zaidi katika nyanja ya sheria. Kwanza kabisa wale majaji wa Kichagga wa mahakama ya Rufaa na Mahakama Kuu wawe wa kwanza kuweka manyanga chini.
Katika kufanya hivyo jamii ya Watanzania ambao inaona ukabila wa wachagga katika sehemu nyingi itaridhika kwani kwa mara ya kwanza tutakuwa tumeshughulikia chanzo cha matatizo yetu mengi.