Je, Viongozi wa Idara ambao ni Wachagga waachie ngazi!??

Je, Viongozi wa Idara ambao ni Wachagga waachie ngazi!??

Status
Not open for further replies.
Kubwajinga,

..tatizo lako wewe umeelekeza macho na masikio Kilimanjaro, ukisikiliza nini kinaendelea huko halafu unaishia kutibuka akili.

..inaelekea kwasababu unafikiri Kilimanjaro "imeendelea" sana basi serikali should spend no penny there, na ifunge shughuli zake ihamie kule kwenye potential na population kubwa zaidi.

..katika taarifa aliyoleta Mwanakijiji kuna barabara nyingi tu za Kusini, na Kusini magharibi, ambazo zinajengwa na serikali hivi tunavyozungumza. barabara za kusini na kusini magharibi make the majority of the road improvement program that Tz gov' is implementing now.

..lakini pamoja na hayo yote wewe umengangania Kilimanjaro X 3. unadai barabara ya Tarakea,Rombo, inaelekea kwenye mpaka wenye magendo. sasa hivi tutakuwa na mpaka rasmi kwa hiyo tuna nafasi ya kupambana na magendo kisayansi. Kenya is among our top 4 trading partners, do not underestimate that.

..barabara ya jimboni kwa Mramba ilikuwa ni ya vumbi miaka yote tangu uhuru. design na upembuzi yakinifu ulifanyika mwaka 1998. ilimualiwa toka kwamba 98 kwamba imepasi vigezo vya kiuchumi kuwa barabara ya lami. mwaka 1998 Rombo ilikuwa chini ya Wapinzani.



Kubwajinga said:
Kwa hiyo kama ulitaka Msukuma ambaye kwao hakuna aliyewahi kwenda shule au kuona shule ashindane na mmachame wa pale maili 20, ambaye kijiji kizima kinajua tayari umuhimu wa shule for the past 50+ yrs, then hufikirii kwa misingi ya kujenga nchi bali kwa misingi ya mimi kwanza wengine watajijua wenyewe.

Kubwajinga,

..again, unayaangalia maendeleo katika hali ya kushindana na kupokonyana. maendeleo hayaishi, ni juhudi binafsi na collective tu zinatakiwa wakati mwingine.

..kutokana na quota-system, kwa mtizamo wako unafikiri ni watoto wangapi ambao ilikuwa wafaulu kwenda sekondari lakini wakaponzwa kwasababu tu wamezaliwa Kilimanjaro?

..badala ya quota-system nadhani serikali ingejieleka kwanza ktk kuinua kiwango cha elimu ktk mikoa ya pembezoni. siyo kuwarubuni wananchi kwa pass-mark ndogo halafu miaka 20 baadaye tunajikuta tuko palepale. kwenye suala kama elimu kuna wakati quality ina umuhimu kuliko quantity.

..serikali pia inaweza kutoa incentives zaidi kwa waalimu, madaktari,na mabwana shamba,... watakaoamua kwenda kufanya kazi huko. kuna tatizo la wataalamu kuyakimbia maeneo yaliyoachwa nyuma kwa sababu mbalimbali.

..
 
Naamini kuwa sasa mjadala huu hapa utakuwa umefikia kikomo baada ya kuweza kuonesha pasipo shaka kuwa chuki dhidi ya Wachagga haina msingi wowote na ya kuwa kosa la mtu mmoja au kitendo cha mtu mmoja hakiwezi na hakipaswi kamwe kuwa mzigo wa kabila zima. Tumeweza pia kuonesha kuwa kila Mtanzania anastahili nafasi sawa ya kufanikiwa na kamwe kusiwepo kizuizi chochote chenye asili ya upendeleo.

Tumeweza kuonesha pia kuwa Tanzania ni ya Wachagga kama vile ni ya wasukuma, na hazina za nchi hii ni zetu na wana wetu sawasawa. Tumeweza pia kuonesha kuwa chuki ya kikabila ambayo inatuuma baadhi yetu ni lazima ikemewe na siyo kuvumiliwa au kufichwa ardhini. Na kwa wazi kabisa tumeza kuona ni nani anasukumwa na chuki hii hata kama hana data au ushahidi kuthibitisha madai yake.

Ni jukumu letu kama mtu mmoja mmoja na kama TAifa kuendelea kuupiga vita ubaguzi wa aina yoyote popote utakapoonekana lakini pia kuwa tayari kuja kuwatetea wale ambao wanabaguliwa au wanachukiwa pasipo sababu yoyote ile.
 
kwanini mjadala ufungwe? acha demokrasia ifanye kazi yake. Wangwe alivyokupa hoja za uchagga mbona ulikaa kimya.
 
mimi kwa maoni ya wengi hapa na mwelekeo wa haya majadiliano, naona wazaramo wanapendelewa, hasa waisho daresalamu.
 
Natangaza kuwachukia Wachaga..nina sababu na ni watu wenye Chuki na wabinafsi...Yes i said na nitaandika kuhusu hili
 
Natangaza kuwachukia Wachaga..nina sababu na ni watu wenye Chuki na wabinafsi...Yes i said na nitaandika kuhusu hili

Angalau wewe umesema wazi chuki yako, hivyo tutakaposoma ulichoandika tutajua kinaongozwa na kitu gani. Kuliko watu wenye kuficha chuki yao.
 
Kama huwajui umejuaje sasa kama wanazificha? Kama unajua wanazificha basi utakuwa unawajua kwa vile unajua kuwa wanazificha.....

najua wanazificha japo sijui ni nani anazificha! sasa hadi wanaposema ndipo najua walikuwa wanazificha.
 
Natangaza kuwachukia Wachaga..nina sababu na ni watu wenye Chuki na wabinafsi...Yes i said na nitaandika kuhusu hili

Who cares??? life moves on. I quote Charles Colton " We hate some people because we don't know them,and we will not know them because we hate them.
So goodluck in your hating but remember hatred bounces!
 
Mgao wa walimu usitishwe Dar, Kilimanjaro- Wabunge

2008-07-16 09:45:01
Na Mashaka Mgeta, Dodoma


Serikali imeshauriwa kusitisha mgawo wa walimu kwa mikoa ya Dar es Salaam na Kilimanjaro, badala yake waelekezwe katika mikoa mingine inayokabiliwa na upungufu wa wataalamu hao.

Hayo yalisemwa na baadhi ya wabunge wakati wakichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi bungeni, mjini hapa jana.

Mbunge wa Kibiti (CCM), Bw. Abdul Marombwa, alisema takwimu zinaonyesha kuwepo idadi ya walimu yenye uwiano wa mwalimu mmoja kwa wananfunzi 38 katika mikoa hiyo, hali ambayo ni tofauti na mikoa mingine yenye uwiano wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi zaidi ya 100.

Alisema kama kuna maeneo yenye walimu wachache jijini Dar es Salaam na mkoani Kilimanjaro, inatokana na upungufu katika mgawanyo wa walimu waliopo.

Naye Mbunge wa Mbozi Magharibi, Dk. Lukas Siyame, alisema jimbo hilo ni miongoni mwa maeneo ya pembezoni yanayokabiliwa na uhaba wa walimu, ambapo kuna wastani wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 200.

Mbunge wa Shinyanga Mjini (CCM), Bw. Charles Mlingwa, alishauri Serikali kuwekeza katika uboreshaji wa miundombinu na kupanua wigo wa elimu ya juu nchini.

Aidha, Bw. Mlingwa, alisema mfumo wa elimu unapaswa kuruhusu pawepo mabadiliko yatakayofuta mitahani ya kidato cha pili.

Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohammed, alipendekeza kuwepo mabadiliko katika Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu, ili kutoa fursa kwa watoto hasa wanaotoka kwenye familia maskini, kupata elimu.

Bw. Hamad, ambaye pia ni Kiongozi wa upinzani bungeni, alisema mfumo uliopo sasa, unaomtaka mwanafunzi kutanguliza asilimia 20 ya malipo yanayohitajika, unawanyima watoto wengi kupata elimu hiyo, hivyo kukinzana na ibara ya 11 ya Katiba.

Kwa mujibu wa maelezo ya Bw. Hamad bungeni, ibara hiyo inazungumzia haki ya raia kupata elimu.
Pia, Bw. Hamad, alisema vigezo vinavyotumika kupitia mtandao wa kompyuta katika kupata uhalisi wa hali ya kiuchumi katika familia wanapotoka wanafunzi hao, vinaweza visitoke majawabu yanayokidhi ukweli kuhusina na suala hilo.

Hivyo, alipendekeza mfumo huo upitiwe upya kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

Bw. Hamad, alisema ili kuhamasisha ushiriki wa wanafunzi wengi katika masomo ya sayansi, kuna haja ya kuweka mazingira bora, kama vile kuongeza fedha kwa ajili ya mafunzo ya vitendo.

Mbunge wa Ubungo (CCM), Bw. Charles Keenja, alipongeza serikali kwa kufanikisha ujenzi wa shule za sekondari katika ngazi za kata, na kupinga hoja za watu wanaozikejeli.

Hata hivyo, Bw. Keenja, alisema ujenzi wa shule hizo jijini Dar es Salaam, unafanyika kwenye maeneo yaliyo nje ya makazi ya watu, na hivyo kusababisha tatizo la usafiri kwa walimu na wanafunzi.

Alisema kutokana na hali hiyo, kuna haja ya kuwekeza katika ujenzi wa mabweni na nyumba za walimu.

Mbunge wa Mkwajuni (CCM), Bw. Mzee Ngwali Zubeir, alisema mfumo wa mitaala ya ufundishaji kati ya Zanzibar na Tanzania Bara una matatizo yanayohitaji kushughulikiwa, ili kupata suluhu.

Bw. Zubeir, alitoa mfano kuwa wanafunzi wa shule za msingi visiwani Zanzibar, wanatumia mitaala inayoandaliwa visiwani humo, lakini wakijiunga sekondari, wanatumie inayotumika katika Muungano na kufanya mitihani ya Baraza la Mitihani.

Alisema tofauti hiyo inaweza kuondolewa kwa kuweka utaratibu unawezesha wanafunzi wa pande mbili za Muungano, kutumia mitaala inayofanana tangu elimu ya awali.

Aidha, Bw. Zubeir, alisema takwimu zilizopo, zinaonyesha wanafunzi wa Zanzibar kufanya vibaya katika mitihani ya kidato cha nne na sita, ikilinganishwa na wale wa Tanzania Bara.

Pia, alizungumzia umuhimu wa kuwajali na kuwathamini walimu, kwa kuwajengea mazingira bora ya kazi na kuwaepusha na vitendo visivyokidhi ridhaa yao, kama kuwakata michango bila kuwashirikisha.

Mbunge wa Viti Maalum (CUF), Bi. Merce Mussa Emmael, alipendekeza kutolewa adhabu kwa wanafunzi wanaopata mimba, kama inavyofanyika kwa wanafunzi wa kiume wanaowapa mimba wanafunzi wa kike.

Alisema hali hiyo itawezesha wanafunzi wa kike kuwa makini katika kufanya mahusiano yasiyofaa na wanafunzi wa kiume.

Wakati huo huo, baadhi ya wabunge wameilalamikia serikali kwa kushindwa kuboresha elimu na mazingira ya kazi kwa walimu nchini.

Mbunge wa Wete (CUF), Bw. Mwadini Jecha, alisema ubora wa elimu si suala linalothibitishwa kwa maneno ama kuwepo kwa vitu kama madawati na madarasa, bali kuwepo walimu bora na mazingira mazuri ya utendaji kazi.

Bw. Jecha, alisema ubora wa elimu hautakuwa na manufaa ama kufanikiwa ikiwa walimu hawatathaminiwa.

Naye Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Bi. Bernadeta Mushashu, alisema baada ya kutekeleza mpango wa kuandikisha idadi kubwa ya wanafunzi katika shule za umma, jitihaza inayotakiwa sasa ni kuboresha elimu inayotolewa nchini.

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalum (CUF), Bi. Mkiwa Kimwanga, alisema uboreshaji wa elimu unapaswa kufanyika kwa kuwahusisha walimu, maeneo ya ufundishaji na mazingira ya kazi.

Awali, akiwasilisha hoja za upinzani, Waziri Kivuli wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bi. Suzan Lyimo, alisema uboreshaji wa elimu ni sehemu ya vigezo vinavyochangia ukuaji wa uchumi.

Bi. Susan alisema mfumo wa elimu hivi sasa unatoa fursa za kuwepo dhana ya ubaguzi kutokana na walio wachache kupata elimu bora wakati masikini walio wengi wanapata elimu ya kati ama kuikosa kabisa, hivyo kubaki katika mazingira ya umasikini.

Mbunge wa Kibondo (CCM), Bw. Felix Kijiko, alisema kuna haja kwa serikali kushughulikia kwa undani matatizo yanayowakabili walimu na sekta ya elimu nchini.

Alisema katika kufanikisha hilo, serikali inapaswa kufanya kazi kwa karibu na Chama Cha Walimu (CWT) chenye mtandao wake nchi nzima, ili kubaini matatizo yanayowakabili walimu.
 
Sipendi... umeuliza kitu muhimu. Yoyote anayefikiria kuwaondoa wachagga katika kufanikiwa atakuwa na kazi kubwa sana. Badala ya watu kukaa chini na kuona wivu dhidi ya Wachagga hatuna budi kujiuliza kwanini wao wamefanikiwa na ni nini wengine tunaweza kufanya kufanikiwa.

Wachagga siyo chanzo cha matatizo ya Tanzania. Chuki dhidi yao inaonesha zaidi jinsi gani wengine tunavyojiona duni.

Mwanakijiji, naomba unisaidie kujibu hili swali...! Je tukishawaondoa wachaga kwenye maradaka/uongozi tuweke kabila gani? Wamasai? Wagogo? Wanyaturu? Wakurya? Wabondei? Wahazabe? Wafipa? Wahehe? Wahaya? Wanyakyusa? Wapare? Wakara? Wangoni?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom