Je, vyombo vya usalama vinatumika vibaya (njama) kumharibia kisiasa mama ?

Je, vyombo vya usalama vinatumika vibaya (njama) kumharibia kisiasa mama ?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Kuna vitu vinafikirisha na kuzaa maswali yaliyokosa majibu kwa haya yanayoendelea hapa nchini kwa sasa yakihusisha kupotea ovyo kwa watu, kamata kamata ya wapinzani, wanaharakati na waandishi wa habari.

Taifa linalazimishwa kwa nguvu kubwa mnoo kuingizwa kwenye taharuki isiyo ya lazima. Vyombo mbalimbali vya habari duniani vinaripoti matukio haya huku vikijenga taswira mbaya ya ubovu wa utawala wa mama katika kusimamia haki za binadamu, demokrasia na utawala bora.

Heka heka hizi zinaendeshwa na nani, kwa malengo gani ikiwa ziko kinyume na mtazamo wa mama?

Kauli za kukinzana baina ya wanausalama wao kwa wao na baina ya watawala kuhusu haya yanayoendelea nchini zinazidisha hofu na mashaka kuwa huenda ni matukio ya njama za kimakusudi kumchafulia mama kisiasa.

Hakuna jambo linaloweza kutendeka kwa bahati mbaya ikiwa linafanywa na mfumo rasmi tena kwa mtindo wa kujirudia rudia.

Huenda yatakayofuata yatakuwa mabaya zaidi ikiwa hatua za kimakusudi kuzuia kuendelea kwa mambo haya hazitachukuliwa sasa. Hakuna aliye salama.

PIA SOMA
- Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akamatwa uwanja wa Ndege Songwe

- Lissu, Mnyika na Sugu wakamatwa na Polisi usiku huu. Baadhi ya Waandishi wa habari pia wakamatwa

- Kuelekea 2025 - Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Nchimbi aiagiza Serikali kuwaachia Viongozi wa CHADEMA
 
IMG_2729.jpeg
 
Akina ChoiceVariable na wennzake wa CCM wanampa mama kongole kwa kuwanyoosha chadema. Kwa mtu mwenye akili timamu hii mambo imekaa vibaya sana kwa mama
Kimsingi kama Chadema wanataka kuleta vurugu washughulikiwe ila kama ni porojo zao za Kisiasa waachwe tuu kama awali.

This time wamepata headlines sana Kwa hii crackdown lakini ilikuwa ni lazima Kwa Kauli za kina Mwaipaya wa Bavicha
 
Habari ya kukamatwa na kuswekwa ndani kwa viongozi wote wa wa juu wa Chadema zimevuma sana leo kwenye vyombo vikubwa vyote vya habari duniani na ndiyo lengo la waliosuka mpango huu mahsusi wa ku tarnish jina na image ya Rais Samia na serikali yake.
 
Mama asimamie nyumba yake achukue kiboko acharaze watt wanaowapiga wenzie bila sababu ..
Mamlaka aliyonayo ni kubwa sanaa
 
Kuna vitu vinafikirisha na kuzaa maswali yaliyokosa majibu kwa haya yanayoendelea hapa nchini kwa sasa yakihusisha kupotea ovyo kwa watu, kamata kamata ya wapinzani, wanaharakati na waandishi wa habari.

Taifa linalazimishwa kwa nguvu kubwa mnoo kuingizwa kwenye taharuki isiyo ya lazima. Vyombo mbalimbali vya habari duniani vinaripoti matukio haya huku vikijenga taswira mbaya ya ubovu wa utawala wa mama katika kusimamia haki za binadamu, demokrasia na utawala bora.

Heka heka hizi zinaendeshwa na nani, kwa malengo gani ikiwa ziko kinyume na mtazamo wa mama?

Kauli za kukinzana baina ya wanausalama wao kwa wao na baina ya watawala kuhusu haya yanayoendelea nchini zinazidisha hofu na mashaka kuwa huenda ni matukio ya njama za kimakusudi kumchafulia mama kisiasa.

Hakuna jambo linaloweza kutendeka kwa bahati mbaya ikiwa linafanywa na mfumo rasmi tena kwa mtindo wa kujirudia rudia.

Huenda yatakayofuata yatakuwa mabaya zaidi ikiwa hatua za kimakusudi kuzuia kuendelea kwa mambo haya hazitachukuliwa sasa. Hakuna aliye salama.

PIA SOMA
- Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akamatwa uwanja wa Ndege Songwe

- Lissu, Mnyika na Sugu wakamatwa na Polisi usiku huu. Baadhi ya Waandishi wa habari pia wakamatwa

- Kuelekea 2025 - Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Nchimbi aiagiza Serikali kuwaachia Viongozi wa CHADEMA
stop that nonsense, unyama huu unafanyika kwa ruhusa yake, with her consent!
 
Back
Top Bottom