U
Kuhusu tafsir ya Qur'an haiwezi kubadilisha au kupotosha maana halisi ya Qur'an kwasababu nakala halisi IPO na itaendelea kuwepo mpaka mwisho wa dunia hii, na hapa ndipo waislamu walipofanikiwa katika kuhifadhi Qur'an ibakie vile vile Kama ilivyo.
Kuhusu Mjomba wako kutumia Qur'an kuroga watu hapo napata ukakasi kidogo kwasababu Mwenyezi Mungu amesema Qur'an ni ponyo na Tiba pia ,sasa iweje iwe INA madhara Kwa watu.
Watu wengi wakiona maandishi ya kiarabu au yanayofanana na kiarabu wanadhani ni Qur'an kitu ambacho si kweli
Kujua elimu ya Dini ni kitu kimoja na kuifuata ni kitu kingine,kwahiyo kuna watu Wana elimu nzuri ya Dini lakini Kwa ukaidi Tu wanaamua kwenda kinyume na mafundisho ya dini,hiyo ni hasara Yao na watawajibika Kwa Hilo,mfano mzuri Mjomba wako kama ulivyosema anajua kabisa anachofanya sio kizuri lakini anafanya Tu na mwisho wake anaujua kuwa utakuwaje.
Lakini Kwa ukubwa wake watu wengine wanafanya maovu Kwa kukosa elimu sahihi ya Dini,hawajui mafundisho ya dini zao,na hawa wakipata elimu sahihi ya Dini hubadilika na kuwa watu wema kabisa.
Mengi kuhusu urahisi WA tafsir ya Qur'an amezungumza tayar ndugu yangu
adriz