Je, Waislamu tunaitendea haki Qur'an?

Je, Waislamu tunaitendea haki Qur'an?

U
Kuhusu tafsir ya Qur'an haiwezi kubadilisha au kupotosha maana halisi ya Qur'an kwasababu nakala halisi IPO na itaendelea kuwepo mpaka mwisho wa dunia hii, na hapa ndipo waislamu walipofanikiwa katika kuhifadhi Qur'an ibakie vile vile Kama ilivyo.

Kuhusu Mjomba wako kutumia Qur'an kuroga watu hapo napata ukakasi kidogo kwasababu Mwenyezi Mungu amesema Qur'an ni ponyo na Tiba pia ,sasa iweje iwe INA madhara Kwa watu.

Watu wengi wakiona maandishi ya kiarabu au yanayofanana na kiarabu wanadhani ni Qur'an kitu ambacho si kweli


Kujua elimu ya Dini ni kitu kimoja na kuifuata ni kitu kingine,kwahiyo kuna watu Wana elimu nzuri ya Dini lakini Kwa ukaidi Tu wanaamua kwenda kinyume na mafundisho ya dini,hiyo ni hasara Yao na watawajibika Kwa Hilo,mfano mzuri Mjomba wako kama ulivyosema anajua kabisa anachofanya sio kizuri lakini anafanya Tu na mwisho wake anaujua kuwa utakuwaje.

Lakini Kwa ukubwa wake watu wengine wanafanya maovu Kwa kukosa elimu sahihi ya Dini,hawajui mafundisho ya dini zao,na hawa wakipata elimu sahihi ya Dini hubadilika na kuwa watu wema kabisa.

Mengi kuhusu urahisi WA tafsir ya Qur'an amezungumza tayar ndugu yangu adriz
Sisi tuliozaliwa pwani tunalijua hili kwasababu swali linabaki kwanini huku pwani kila mganga lazima umkute ana msahafu kwenye kilinge chake? Na hata anapokupa dawa lazima asome kwanza,na kwanini waganga watumie kiarabu tu na sio kisambaa au kisukuma?
 
Sisi tuliozaliwa pwani tunalijua hili kwasababu swali linabaki kwanini huku pwani kila mganga lazima umkute ana msahafu kwenye kilinge chake? Na hata anapokupa dawa lazima asome kwanza,na kwanini waganga watumie kiarabu tu na sio kisambaa au kisukuma?
Jibu ni rahisi Sana katika quran kuna Tiba na. Ponyo, sasa vipo visomo vinasomwa kupitia Aya za Qur'an,ambavyo unaweza kumtibu mtu aliyepatwa na majini mapepo,pamoja na kutibu maradhi mengine.

Lakini bahati mbaya Sana hao hao maustadh wanachanya Tiba ya kisheria ambayo sio haram na kuchanganya na haramu ikiwemo kupiga ramli.

Kwahiyo ni kweli huenda Wana Misahafu lakini haimaanishi kuwa Qur'an inatumika katika ushirikina laa! Ila hao Wahusika wanachanganya na ushirikina .
 
Koran mapepo yanajua ni kitabu Chao na sehemu Yao ya kuabudia ni msikitini
 
Jibu ni rahisi Sana katika quran kuna Tiba na. Ponyo, sasa vipo visomo vinasomwa kupitia Aya za Qur'an,ambavyo unaweza kumtibu mtu aliyepatwa na majini mapepo,pamoja na kutibu maradhi mengine.

Lakini bahati mbaya Sana hao hao maustadh wanachanya Tiba ya kisheria ambayo sio haram na kuchanganya na haramu ikiwemo kupiga ramli.

Kwahiyo ni kweli huenda Wana Misahafu lakini haimaanishi kuwa Qur'an inatumika katika ushirikina laa! Ila hao Wahusika wanachanganya na ushirikina .
Acha
Jibu ni rahisi Sana katika quran kuna Tiba na. Ponyo, sasa vipo visomo vinasomwa kupitia Aya za Qur'an,ambavyo unaweza kumtibu mtu aliyepatwa na majini mapepo,pamoja na kutibu maradhi mengine.

Lakini bahati mbaya Sana hao hao maustadh wanachanya Tiba ya kisheria ambayo sio haram na kuchanganya na haramu ikiwemo kupiga ramli.

Kwahiyo ni kweli huenda Wana Misahafu lakini haimaanishi kuwa Qur'an inatumika katika ushirikina laa! Ila hao Wahusika wanachanganya na ushirikina .
Maelezo yako yanajichanganya yenyewe, nimekueleza hayo kwakuwa mimi kwetu kwa upande wa mama ni mikindani kwahiyo ninachokusimulia ni kitu ninachokijua tangu nipo dogo hadi leo,huku pwani kwetu ndio mambo yakawaida tu watu wanaenda kwa masheikh wanapiga visomo vyao vya kichawi na watu wanadhurika wale waliokusudiwa,nakupa mfano kuna kijiji kimoja wanaita mnima huku mtwara vijijini sheikh fulani alipiga visomo mnazi ukakauka mchana kweupe
 
Sasa huo mkuu ni uchawi na umekiri mwenyewe,je Qur'an inaingia wapi hapo?
 
Sasa huo mkuu ni uchawi na umekiri mwenyewe,je Qur'an inaingia wapi hapo?
Nimewahi kumpeleka mtu kwa sheikh fulani pale pande alikuwa na kesi moja mbaya sana vilipigwa visomo na kafara kibao pale tangu saa 3 usiku mpaka saa 10 alfajiri na jamaa alichomoka kwenye hiyo kesi
 
Sasa huo mkuu ni uchawi na umekiri mwenyewe,je Qur'an inaingia wapi hapo?
Mapepo ambayo kitabu Chao na dini yao wamesema ni uislam, ndio yanayotumiwa na ao mashekh tena wanayaita kwa kutumia koran
 
Siku moja nimesafiri na sheikh abbas hadi Dubei kichwani nafikiri mwenzangu kiarabu ndo lugha yake maashallah hatutapata ugumu kupata huduma.

Aliniangusha mbaya!
Zile za kukarori kuran kumbe hua ni changa la macho
 
Kuna msitari mwembaba sana wa Kutofautisha Ushirikina na uislamu.

Yani ni mwembamba mno
 
Nimewahi kumpeleka mtu kwa sheikh fulani pale pande alikuwa na kesi moja mbaya sana vilipigwa visomo na kafara kibao pale tangu saa 3 usiku mpaka saa 10 alfajiri na jamaa alichomoka kwenye hiyo kesi
Kwahiyo unataka kusema nini sasa mkuu
 
Ma shaa allah
JazakAllah Khair Akhy. Thread nzuri sana. Hakika tukishikamana na quran hakuna jambo litakua gumu kwetu na changamoto tuzipatazo ndan ya quran kuna faraja. Ya allah tujalie tuwe ni wenye mapenz na yale yaliyomo ktk kitabu chako
 
Mimi kwa mtazamo wangu haya mambo ya kutafsiri tafsiri ndio yatatokea yale ya kwenye biblia utatafsiri kwa lugha ambayo haijitoshelezi kwa maneno je kipi kitatokea? Quran iachwe tu kwa lugha yake ya asili,halafu mwanadamu ni mbishi tu kwa asili kumbuka kisa cha wana wa israeli ambao walikuwa wanauona utukufu na nguvu za Mungu live kabisa kwa macho yao ila kwamakusudi kabisa walikuwa wanampinga Mungu sembuse sisi ?

Tafsiri ya Quran ni fani katika fani ya elimu ya Quran, hivyo pamoja na kwamba Quran ipo kwa lugha ya kiarabu ila bado inahitaji kutafsitiwa.

Na Quran inatafsiriwa kwa Quran yenyewe, sunna(hadith za mtume), kauli za maswahaba, lugha ya kiarabu.....

Hivyo tafsiri ya Quran haishii tu kwenye yale maneno ya kiarabu, bali ni mafuhumu yaliyo kusudiwa ambayo ndio elimu yenyewe. Na ndio maana Quran inatakiwa itafsiriwe na wenye elimu hiyo( Wanachuoni).

Hivyo kuitafsiri Quran kwenda lugha zingine za kiajemi, ni jambo linalo takikana ili ifahamike, almuhimu kuhifadhi ule ufahamu na maaana iliyokusudiwa.

Na katika jamii yakiislamu, sawasawa ya kiarabu au sio ya kiarabu wapo wasiokuwa na elimu(a'ammiy) hivyo ni lazima watu hawa watafsiriwe na kufahamishwa na wenye elimu.

Na Allah ni mjuzi zaidi.
 
Ma shaa allah
JazakAllah Khair Akhy. Thread nzuri sana. Hakika tukishikamana na quran hakuna jambo litakua gumu kwetu na changamoto tuzipatazo ndan ya quran kuna faraja. Ya allah tujalie tuwe ni wenye mapenz na yale yaliyomo ktk kitabu chako
Amin thuma Amin ukhty
 
Tafsiri ya Quran ni fani katika fani ya elimu ya Quran, hivyo pamoja na kwamba Quran ipo kwa lugha ya kiarabu ila bado inahitaji kutafsitiwa.

Na Quran inatafsiriwa kwa Quran yenyewe, sunna(hadith za mtume), kauli za maswahaba, lugha ya kiarabu.....

Hivyo tafsiri ya Quran haishii tu kwenye yale maneno ya kiarabu, bali ni mafuhumu yaliyo kusudiwa ambayo ndio elimu yenyewe. Na ndio maana Quran inatakiwa itafsiriwe na wenye elimu hiyo( Wanachuoni).

Hivyo kuitafsiri Quran kwenda lugha zingine za kiajemi, ni jambo linalo takikana ili ifahamike, almuhimu kuhifadhi ule ufahamu na maaana iliyokusudiwa.

Na katika jamii yakiislamu, sawasawa ya kiarabu au sio ya kiarabu wapo wasiokuwa na elimu(a'ammiy) hivyo ni lazima watu hawa watafsiriwe na kufahamishwa na wenye elimu.

Na Allah ni mjuzi zaidi.
Shukrani Sana Al akhy Kwa mchango wako wenye kilo nyingi za kutosha
 
Back
Top Bottom