Je, Wajua Benki Kuu ya Afrika Kusini inamilikiwa na watu binafsi? Ni miongoni mwa benki 8 zenye umiliki wa aina hiyo Duniani

Je, Wajua Benki Kuu ya Afrika Kusini inamilikiwa na watu binafsi? Ni miongoni mwa benki 8 zenye umiliki wa aina hiyo Duniani

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Kawaida Benki Kuu Duniani huwa zinamilikiwa na Serikali za nchi husika zikiratibu sera mbalimbali za kifedha ikiwemo kudhibiti kiwango cha fedha kinachoingia kwenye mzunguko na kuzisimamia benki binafsi zilizopo kwenye nchi husika. Benki kuu huwa zina nafasi ya kipekee kuimarisha uchumi wa nchi.

Benki kuu ya Afrika Kusini ilianzishwa mwaka 1921 na kuwa benki kuu ya nne kuanzishwa nje ya bara Ulaya na ni benki yenye umri mkubwa zaidi barani Afrika. Benki hiyo inazo hisa milioni 2 huku kila mwanahisa hawezi kuzidisha umiliki wa hisa 10,000 na kwasasa benki hiyo ina wanahisa 696.

Nchi nyingine zenye benki za aina hiyo ni Ubelgiji, Ugiriki, Italia, Japan, Switzerland, Uturuki na Marekani.

Mwaka 2017 chama tawala cha ANC kiliazimia kutaifisha benki hiyo, azimio ambalo utekelezaji wake umekwama hadi sasa.

Rais wa sasa wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa akiwa kwenye kongamano la sera siku tatu zilizopita amethibisha kuendelea kwa azimio hilo huku wajumbe wakitaka utekelezaji wa kasi ikizingatia gharama kwa hazina ya Taifa hilo ambayo tayari imetumika.
 
Uchumi wa South Africa unamilikiwa na Wayahudi, kwahiyo possibly wenyewe watakuwa ni hao Jews.
 
Bank zooote Duniani ni Mali ya Rothchild family wana asili ya uyahudi uchwara!.....wa kujipachika ilihali wayahudi original wapo lkn hawajitambui kabisaa.....kwa sababu mbalimbali ambazo sitazitaja hapa sababu si lengo la mleta uzi.
 
Bank zooote Duniani ni Mali ya Rothchild family wana asili ya uyahudi uchwara!.....wa kujipachika ilihali wayahudi original wapo lkn hawajitambui kabisaa.....kwa sababu mbalimbali ambazo sitazitaja hapa sababu si lengo la mleta uzi.
Myahudi halisi utakuwa wewe
 
Myahudi halisi utakuwa wewe
Naaam!!! ubarikiwe. Uko wapi sasa hivi! Make umenifurahisha sana!..... Unaweza kuja hapa nilipo upate moja baridi??.....dogo Kiti moto inapanda kwani? ......Basi njooo. Usogope popo bawa wee njoo tu ivo ivo!!........
 
Back
Top Bottom