Je, wajua? - Special Thread

Je wajua kwamba paka huweza kukuua endapo atapigana na wewe mkiwa ndani huku milango imefungwa?
 
Je wajua fisi anapocheka ujue ameshikwa na uoga au kuna kitu anaogopa
 
Je wajua asilimia 60 ya mwili wa binadamu ni maji
 
1.Kuna
baadhi ya mafuta ya kupaka na
vipodozi vinaweza kuvutia siafu
endapo ukatumia mwilini.Na kama
ikatokea umepumzika kwenye
eneo lenye vichuguu na ukapitiwa
na usingizi fofo,siafu wanaweza
kukujeruhi au kukuua

2.Siafu
huua zaidi ya watu 30 kwa mwaka
duniani

3.Sheria zote za mpira wa
miguu duniani ziliundwa mnamo
Okt.1863 katika Lodge ya
Freemason's Tavern mjini
London,Uingereza 4.Hapo
kabla,mji(mkoa) wa Dar-es-
Salaam,Tanzania ulikuwa unaitwa
Mzizima

5.Wasukuma ndiyo kabila
linaloongoza kwa idadi kubwa
zaidi Tanzania wakati Wamasai
ndiyo kabila pekee linalovaa
kitamaduni

6.Neno Dodoma kwa
Kigogo humaanisha "Imezama"
wakati neno Nyamwezi
humaanisha "Waona Mwezi"

7.Noti ya sh.5000 ya Tanzania,enzi
za utawalawa wa B.W.Mkapa,iliku
wa na picha ya mnyama kifaru

8.Marekani na Canada ndiyo
mataifa pekee duniani yaitao
mpira wa miguu "Soccer"
 
Usingizi na kula mdio kitu pekee ambacho watu wote duniani wanakifanya
 
Je wajua mafuta ya nazi ni dawa ya mafizi!

Kwa wale wenye matatizo ya kutokwa damu mafizini unachotakiwa kufanya - chukua mafuta ya nazi jiweke kwenye kidole/vidole kisha anza kuyapakaza kwenye mafizi kwa kupitisha kidole/vidole kama unavyofanya unapokuwa unaswaki
 
Je wajua Tanzania tunasifika sana kwa uuaji wa Tembo!

Na imesadikika tembo japo 30 wanauliwa kwa siku au naweza sema ndani ya siku moja
 
Je wajua siku ya jumatatu ndio siku inayochukiwa zaidi katika wiki?
 
Huyu mlimbwende acha tu, sijui niendelee, jamani huyu mlimbwende, mjue naumia mie, kama vipi naendelea.

Je wajua yule mlimbwende muigizaji filamu wa kuitwa Halle Berry hakuoga kwa kipindi cha miezi miwili mfululizo wakati wakiwa wanatengeneza filamu yao jina JUNGLE FEVER
 


Kila Alhamisi na Ijumaa, shughuli katika mji wa Kisumu, magharibi mwa Kenya, huvurugika kwa sababu mamia ya waendesha pikipiki huzuia barabara kutokana na kukodiwa kuomboleza msiba kwa malipo.

Kelele za sauti zao, ukubwa wa misafara ya pikipiki vinatumiwa kama kigezo cha umaarufu na heshima kwa marehemu.

Lakini sasa haya yote huenda yakawa mambo ya kale, baada ya serikali ya kaunti ya Kisumu kuharamisha mtindo huu wa uombolezaji.

Chanzo: BBC Swahili

 
Habari wana JF! Katika pita pita yangu nimekutana na mambo yafuatayo hapa chini nikaona ni vizuri tujuzane, kama kuna anayeweza kutuongezea, pia siyo mbaya: Je wajua;

1.Tar 4/4, 6/6, 8/8, 10/10 &12/12 zinaangukia siku moja kwa mwaka wowote?

2.Fisi hujifungua kupitia kisimi?

3.Mstari wa Equator hupitia nchi 13 ambazo ni: Ecuador,Colombia, Brazil, Sao Tome & Principe, Gabon, Republic of the Congo,Democratic Republic of the Congo, Uganda, Kenya, Somalia, Maldives, Indonesia na Kiribati.

4.Chuo kikuu cha Al – Azhar kilichoko Cairo nchini Misri ndicho chuo kikuu cha zamani zaidi duniani, kilianzishwa mwaka 969 AD.

5.Pesa ya noti haikutengenezwa kwa karatasi bali kwa pamba?

6.Ulimi wa Kinyonga ni mrefu kuliko mwili wake?

7.Binadamu hutengeneza wastani wa nusu lita ya ushuzi kwa siku?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…