Je, wajua? - Special Thread

Je, wajua? - Special Thread

ju wajua uzito wa tembo unalingana au umepishana kidogo sana na uzito wa mnyama nyangumi?? wajua hilo??


mkuu umezogoa nyungumi mkubwa kabisa anafikia tan 95 na ulimi wake hufikia uzito wa tan tisa na tembo mkubwa kabisa hufikia tan sita umemdhalilisha sana nyangumi kumlinganisha na tembo
 
Je wajua baadhi ya je wajua za kwenye star tv ni za uongo
 
Je wajua ni Tanzania pekee viongozi wa serikali wanaiba pesa za wananchi za Escrow Sh billioni 300 na wananchi
wananyamaza tu kama mambumbumbu?
 
je wajua Tanzania ndio nchi ambayo kuna vyeo vingi ambavyo vingine havina umuhimu,mfano Mkuu wa wilaya
 
Je wajua?
1. Mamba hatafuni anakata vipande na kumeza.
2. Macho ya mamba hayana mifuniko (eyelids)
3. Meno ya mamba hayagusani kwenye surface akifunga mdomo, binadamu ya juu na chini yanagusana (oclussion)
4.Tembo anaweza kunusa harufu ya maji kutoka umbali wa zaidi ya km 3.
5. Papa (shark) anaweza kupata harufu ya TONE MOJA LA DAMU ndanid ya maji akiwa umbali wa mita 400! (Usioge baharini ukiwa na kidonda kibichi)
6.Papa akiwa kwenye maji hawezi kusimama huku akielea. Ni lazima awe ana move ili aelee. Density yake ni kubwa kuliko ya maji na hana swim bladder

Ni kweli mamba anameza mawe ili kusaidia kusaga nyama anayokula?
 
Je wajua mwanza ndio mkoa wenye kiasi kikubwa cha maji kuliko mkoa wowote hapa tz na singida ndio mkoa mkame kabisa

hii si kweli, Kigoma ndio unaoongoza, kama ungesema eneo sawa, but volume no.Kina cha lake Tanganyika kinakusanya maji mengi sana.
Halafu unaposema ukame unatakiwa kudeine zaidi - usio na maji, usio na mvua, usio na misitu, n.k.
 
Je wajua Tanzania ndio nchi pekee duniani yenye maamri jeshi wawili na raisi wa jamhuri ya muungano hana sauti au mamlaka zanzibar?
 
je wajua madini ya Tanzanite yanapatika Tanzania pekee duniani

ila upande wa mauzo india ndio inaongoza kwa kuuza hayo madini duniani
 
Back
Top Bottom