Fernando Wolle
JF-Expert Member
- Aug 19, 2022
- 387
- 770
Kwa mtazamo wa wenye akili timamu kichwani.Ukweli Kwa mtazamo wa nani??
Waliulizwa swali hao wengi ni wangapi?, kumbe humo humo kwenye baraza kuna matajiri wakubwa wenye kuguswa maslahi yao.Sauti ya wengi ni sauti ya mungu kwakuwa na tec ni jopo la watu wengi hivyo ni sauti ya mungu
Pia kumbuka kuwa mamlaka yoyote ya kidunia hubarikiwa na Mungu pia. Ukimuona rais anaapa kashika kitabu cha dini jua kuwa anabeba mzigo mzito lakini kazi yake ina kibali kwa Mungu.Soma Kitabu Cha Wafalme wa Kwanza Sura ya 18 na 19 kuhusu Nabii Elia na Mfalme Ahabu. Kama huamini Utakatifu wa Biblia basi soma tu kama Story ya Kawaida utaelewa Nafasi ya Watumishi wa Mungu kwamba ni maiki ya Mungu kuzungumza na Taifa lake.
Unabii wa maaskofu unaheshimiwa na sisi wakatoliki lakini unahojika pia. Kama miongoni mwao wanayo maslahi makubwa ya utafutaji mali na wanajificha kwenye sera za uzawa maana yake serikali inayotazama mbali inayo haki ya kuendelea na mipango yake.Ahsante Bro! huyu ni mkatoliki magumashi tu!
Yohanne Mbatizaji alimkemea Herode kwa kumwoa herodia mke wa nduguye--
Matokeo yake fitna ikawepo na yohane mbatizaji akakatwa kichwa.
Wengi waliteswa na kuuawa kwa kuwa wakweli akina Daniel, Jeremia, Paulo na Sira, Na yule nabii aliyemwonya yule tajiri aliyekuja kunyakua shamba la Naboth (shamba la Urithi) nk.
Shadrack abednego na Meshack waliotupwa kwenye tanuru la moto walipokataa kuabudu lisanamu la mfalme!
Maaskofu wetu ukiona wamefikia kutoa barua ya kichungaji jua wako tayari kwa lolote.
Askofu wa Karagwe Rweyongeza kawaambia waumini wake wazi wazi nyie mchague vizuri viongozi wenu. Siye tumezoea kufa/kuuawa kwa sababu ya kweli ndiyo maana mavazi yetu ni mekundu.
Ule waraka ni barua ya kichungaji kama nyingine zilizotolewa, Alipigwa nazo mkapa, Kikwete, Magufuli na sasa huyu.
Askofu ana vyeo 3: Mchungaji, Mfalme na Nabii.
Barua ya kichungaji ni Unabii- Tunatakiwa kuufuata!!
Kuhoji ni kuuliza jambo na kutaka litolewe ufafanuzi, watanzania wana haki ya kumhoji Rais hata kama ni in direct lkn ujumbe ufike na hujavunja sheria!! Nadhan ungeiweka sawa context yako kua ... Wanaccm hawapasw kumhoji mwenyekiti wao na sio wananchi!!
Kama wameguswa maslahi yao ni vibaya kulalamika kwanWaliulizwa swali hao wengi ni wangapi?, kumbe humo humo kwenye baraza kuna matajiri wakubwa wenye kuguswa maslahi yao.
Paskali pitia hii comment huenda ubongo wako ukafungukaPasco
kuchanganya dini na siasa ni dhana potofu. Rais na Wabunge wanaapa kwa kushika Biblia na Quran Tukufu.
Bunge linaanza kwa sala ya kutambua uwepo wa Mungu ambalo ni jambo la dini.
Mgeni rasmi wa Baraza la Eid siyo sheikh mkuu ni Rais wa Nchi
Mgeni rasmi wa maadhamisho ya miaka kama yale ya miaka 60 KKkT siyo Askofu mkuu ni Rais
Mvua isoponyesha tunakwenda uwanja wa Taifa viongozi wa dini, siyo RC au DC kuombea Nchi
Tunapozozana kwa Katiba au vyama vya siasa tunakwenda uwanja wa Taifa kuombea amani
Anayeongoza sala na maombi ni viongozi wa dini, siyo Waziri Mkuu au Mkuu wa Mkoa
Orodha inaendelea....
Viongozi wa dini wanaotenda hayo hapo juu wakizungumzia mambo yanayohusiana na hayo hapo juu inakuwa kuchanganya dini na siasa. Yaani kuchanganya siasa na dini ni sawa, lakini dini na siasa si sawa.!!
Kwa wale wanaosoma, mifumo ya utawala wa Dunia imejengwa katika Template ya mifumo ya Tawala za dini.
Yaani dini ndiyo imetengeneza 'structures' za siasa za Dunia ya leo, kwahiyo dini ni siasa kwanza.
Pili, kuna tatizo kubwa sana kwa Watanzania na limjitokeza wakati huu wa tatizo la Bandari
Kuna ' messenger ' halafu ' Message' . Watu wanamshambulia messenger badala ya message
Bila kujali Waraka ni wa kidini, una nguvu gani au la, soma 'contents' kisha uzijibu kwa kukukubaliana nazo au kutokubaliana nazo kwa kuangalia 'MKATABA' kama reference.
Bila kujali upande mtu anaouchukua, muhimu ni kujibu iwe 'for or against'.
Watanzania hatujui debate au kujenga hoja, tunaongea tu bila ufahamu wa mada.
Ikiwa mtu anadhani kuna kitu kizuri au kibaya kinaambatana na MKATABA wa Bandari, jambo la kwanza atueleze kwanini anadhani mkataba ni Mzuri au ni Mbaya halafu ajenge hoja yake anayokusudia , si kutueleza conclusion bila analysis
Huyo ni njaa inamtesa, sijui alikwama wapi kama 1990 tayari alikuwa na degree viwanja pale Ubungo nadhani ilikuwa ni pori unajikatia mpk Manzese darajani maanake sahivi alitakiwa awe na mali nyingi sn sijui ni uzinzi na starehe vilimponza sahivi ndiyo kajibana channel 10 apate namna ya kuishiMungu ni KWELI na neno lake ni ukweli.
Kama waraka una ukweli basi ni neno la Mungu, kama uongo siyo.
Wasijenge hoja kwa kusingizia umma wa watanzania kwamba eti sauti ya Mungu wameisikiliza, wakati ukweli ni kuwa maslahi yao hapo bandarini yanakwenda kupotea mazima.Kama wameguswa maslahi yao ni vibaya kulalamika kwan
Tatizo kibogoyo ni sawa na simba aliyekula nyama ya mtu........................unamshambulia bure mwenzako, hebusoma hii kutoka kwa Kalidinali Pengo
Kadinali Pengo ameyasema hayo wakati akiadhimisha ibada ya Jumapili ya matawi huko Bagamoyo katika tamasha la vijana.
“Katika wiki chache zilizopita watu wamekuja kwangu wakaniuliza unaionaje ile barua ya Maaskofu kuhusu Kwaresma mwaka huu? Ninazungumzia hilo na wala mtu asiende aka-quote kitu kingine ndio maana nataka kusema wazi kabisa:-
“Barua ile ijapokuwa hata jina langu mnaliona limeandikwa pale kwamba na mimi ni mmoja wa waandishi au watamkaji…mimi nimeipokea, baadhi yenu mmeshaipokea.
” Kwahiyo sioni namna gani mimi naweza kuwa mwandishi au mhubiri kwenu wa ile barua ambayo imetungwa labda na maaskofu…naamini na baadhi ya maaskofu lakini mimi mwenyewe hata nilikuwa sijaiona, hata nilikuwa sijaambiwa kuna kitu cha namna hiyo kinakuja.
“Tuelewane vizuri, ninaposema hivi sitaki kusema ile barua ni mbaya. Moja tu ni kwamba barua nzima imechanganya vitu viwili; Mwalimu angekuwepo angepiga kelele Maaskofu msichanganye Dini na Siasa.
“Angepiga kelele sana kuhusu waraka huu katika nyakati zake. Na hilo nawambia sina hofu, muende mkamwambie mtu yeyote nimesema hivi. Ndio wala msione aibu, najua labda hata wengine mmekunja nyuso, kunjeni tu lakini huo ndio msimamo wangu.
“Zipo sehemu katika waraka huo zinazochanganya Dini na Siasa na si kazi ya maaskofu ni kazi yenu wanasiasa mkiwa ni wa CHADEMA, mkiwa ni wa CCM lakini haiwezi kuwa kazi yangu mimi.
“Siwezi kwanza nikaanza kuchambua na ku-criticize Serikali katika mambo yaliyo yake; sikupewa mamlaka hayo. Na kwanini niwe padri mpaka nikubali kuwa Askofu na huku kumbe wito wangu ni siasa?
Sio kujibu kwa ufasaha, hataweza kujibu kabisaWakati mwingine kunyamaza pia ni busara, hata kama una uhuru wa kutoa maoni. Hii njia uliyoichagua, itakushushia heshima yako kwa kiwango cha ajabu.
Na ushahidi mdogo tu ni hayo maswali uliyoulizwa na wajumbe! Sidhani kama baadhi yae unaweza kuyajibu kwa ufasaha.
Mungu hamtumii Kila mtu kufanya maamuzi sahihi. Historia zinaonesha Wafalme wengi na watawala wamewahi kuuingiza umma kwenye matatizo kwa kukaidi sauti za Mitume na Manabii. Hao Watanzania milioni 60 na shee unaosema wewe ni wangapi wamekubali maamuzi ya Serikali kama sio wale tunwalioko serikalini na vibaraka?Pia kumbuka kuwa mamlaka yoyote ya kidunia hubarikiwa na Mungu pia. Ukimuona rais anaapa kashika kitabu cha dini jua kuwa anabeba mzigo mzito lakini kazi yake ina kibali kwa Mungu.
Ukiona serikali imeamua kupuuza huo waraka ujue kwamba ni kwa faida ya watanzania milioni sitini na ushee ambao ndio hao hao wenye sauti ya wengi inayojulikana kwa Mungu.
Pascali ana mtazamo wa siasa..Waraka wa TEC ni neno la Mungu bro. LINAKUWA SEHEMU YA MAPOKEO. RUDIA MAFUNDISHO
Tumehama kwenye dp world tumehamia kwenye amri kumi za Mungu...?😂😂 Mpaka damu itokeNionyeshe bandari kwenye amri kumi za Mungu
Kiapo cha rais ni duniani na mbinguni kumbuka hilo.Hao manabii wetu na wao ni wachafu vile vile na ushahidi ulishawekwa hadharani na mwingine hatuwezi kuuweka humu jukwaani.Mungu hamtumii Kila mtu kufanya maamuzi sahihi. Historia zinaonesha Wafalme wengi na watawala wamewahi kuuingiza umma kwenye matatizo kwa kukaidi sauti za Mitume na Manabii. Hao Watanzania milioni 60 na shee unaosema wewe ni wangapi wamekubali maamuzi ya Serikali kama sio wale tunwalioko serikalini na vibaraka?
Hela iliyokusomesha bora ingenunua ng'ombeSiliza rais ndiye mwenye dhamana -heshimu mamlaka