Je, wakati umefika kwa nchi yetu kutunga sheria inayoruhusu utoaji salama wa Mimba?

Je, wakati umefika kwa nchi yetu kutunga sheria inayoruhusu utoaji salama wa Mimba?

new forest

Member
Joined
Mar 28, 2024
Posts
35
Reaction score
97
Nimelazimika kuleta Uzi huu, kutokana na kuona ongezeko kubwa la watoto wa mitaani, yatima, watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, machokoraa, "panya road" na kadhalika.

Ukichungiza matatizo yote hayo, mwanzo wake ni kutokana na mimba zisizotarajiwa.

Kwa vyovyote vile mtoto akiletwa duniani Kwa wakati sahihi, Kwa malengo sahihi, na watu sahihi, hawezi hata siku moja akaishia kuwa chokoraa, mtoto wa mitaani au panya road.

Nafikiri ni wakati umefika kwa jamii yetu kuondoa dhana potofu kuwa Kila tendo la UTOAJI MIMBA ni haramu. Kuna nyakati binti/mwanamke anaweza akapata mimba katika mazingira yasiyotarajiwa au kwa bahati mbaya mfano kubakwa, au binti ni mwanafunzi au umri bado mdogo nk.

Kuna mazingira mengi yanaweza yakatokea, na "option ya kutoa mimba ikawa sahihi zaidi Ili kuepusha matatizo yanayoweza kuzuilika siku za usoni.

Nafikiri ni wakati Kwa jamii yetu kuondoa kasumba ya kuamini Kila tendo la kutoa mimba ni haramu. Na kusema kutoa mimba unakuwa umeua kiumbe hai sio sahihi kwani kiumbe hai kinaanza kuhesabika siku unayo zaliwa.

Wakati umefika Kwa nchi yetu kitunga Sheria kuhalalisha utoaji mimba salama (safe abortion) kama baadhi ya nchi zinavofanya Ili kuepusha jamii na matatizo lukuki yanayosbabishwa na mimba zisizotarajiwa ambazo baadaye zinasababisha watoto wasiotarajiwa, na baadaye tunakuwa na jamii isiyotarajiwa.

Naomba kuwasilisha, wakuu. Matusi, mapovu ruhksa kabisaa. Karibuni.
 
Hao machokoraa elewa kuwa wapo waliozaliwa na wazazi wawili na hawana uyatima. Hizo tabia mbovu ni matokeo ya malezi mabaya kwa watoto. Hakuna sheria ya utoaji mimba salama ila mimba zinatolewa sana tu na hakuna anayekamatwa
Malezi mabovu katika familia ni chanzo Cha mimba zisizotarajiwa , uchokoraa, wadudu, panya roads etc. Hizi sheria hazina maana km kwenye familia hatuwezi badilika
 
Malezi mabovu katika familia ni chanzo Cha mimba zisizotarajiwa , uchokoraa, wadudu, panya roads etc. Hizi sheria hazina maana km kwenye familia hatuwezi badilika
vipi kuhusu single mother, huko si ndiko matokeo ya malezi mabaya ya watoto kulelewa bila baba? Hata kama mama ana uchumi mzuri lakini watoto wake watakuwa na upungufu wa malezi ya baba na kujikuta wana tabia za hovyo
 
vipi kuhusu single mother, huko si ndiko matokeo ya malezi mabaya ya watoto kulelewa bila baba? Hata kama mama ana uchumi mzuri lakini watoto wake watakuwa na upungufu wa malezi ya baba na kujikuta wana tabia za hovyo
Sidhani kama tabia za mtoto zinaendana na hilo... Mimi ni mmoja wapo wa niliyelelewa na mzazi 1 na tupo 6 mpaka sasa katika utu uzima wangu hakuna ambaye alimsumbua mzazi.
Busara na hekima na kumfundisha mtoto mapema kuwa na hofu juu ya Mungu inatosha.
 
Back
Top Bottom