Je, Wanaume wanaogopa ku-date na Wanawake waliowazidi kipato?

Je, Wanaume wanaogopa ku-date na Wanawake waliowazidi kipato?

Bila kupoteza muda niende kwenye mada.

Nimekutana na matukio mawili yaliyonifikirisha na kunifanya nikaribie kwenu ili nipate mawazo yenu

Binafsi nimewahi kudate huko nyuma baada ya kumaliza masomo ya chuo siwezi kusema yalikua serious kwasababu bado nilikua sijapata kazi na kufikia malengo yangu mbali mbali niliyojiwekea. Nimefanya kazi sehemu kadhaa nikapata nafasi ya kwenda nje kujiendeleza kielimu. Baada ya kurudi Mungu hamtupi mja wake nimepata kazi nzuri nikafanikiwa kuanza ujenzi na sipo sehemu mbaya nikijaliwa mwisho wa mwaka nahamia kwangu.

Niwe tu mkweli mimi ni mchakarikaji haswa , sio wale wadada wanaopata vitu kwa kwa kutegemea wanaume hapa nilipo ni bidii yangu na support ya wazazi. Sasa katika maisha ya kazi nilibahatika kukutana na kaka ambaye katika kuzoeana tulianzisha mahusiano ambayo kwa namna moja yalikua serious ( ama ndivyo nilivyoyatafsiri) tulikua huru na wazi na baadhi ya nduguze walinifahamu.

Huyu kaka baadae katika ukaribu wetu alijua kwamba nimejenga na nina kabiashara kangu kaongeza kipato japo sikua najivuna lakini alianza kuonyesha inferiority na ikawa chanzo cha ugomvi. Nikisafiri kikazi alikua muda wote anapiga video call na voic call nikajua mahaba kumbe alikua na wivu na vitu kama hivyo mwishowe tulishindwana maana ikitokea kupishana anasema unaringa sababu una gari, umejenga etc kwa hiyo nikagundua hajiamini na anawivu hata usiopaswa ( kuna wakati alisema niache kazi kwasababu nasafiri sana) kitu ambacho kilipelekea mimi kukosa furaha na hatimae nikaumaliza mwendo.

Juzi tu nimekaa na rafiki yangu wa karibu ambae ni single mom wa baby girl mmoja mume alifariki mapema mno ila ni mpambanaji haswa na kwao wanamsupport sana kwa hiyo mambo yake si haba ana kazi nzuri, ana kwake , usafiri na mwanae anaishi nae vizuri sasa katika kufuta upweke akakutana na mkaka wakaanza mahusiano.

Miezi michache mbele mkaka akamwambia dada najiskia vibaya kuwa na mwanamke alienizidi anajiona ha-fit kwa huyu dada ( yani sio wa level zake) na anaona kama dada atamuacha afate wa size yake. Ninavyomfahamu rafiki yangu yuko humble sana na ana aibu yani sio mdada wa mjini .

Ameumia kuachika kisa tu mwanaume anahisi hawaendani vipato ( Mwanaume ni mwajiriwa private) , ni wiki inakata mwanaume kakata mawasiliano.

Ina maana siku hizi wanaume wanaogopa kukuta mwanamke ana kila kitu? Wanaona watadharaulika ama wanaona watachitiwa? Karibuni tujadili kwa lugha ya staha na heshima.

Ikiwezekana ushauri utolewe nini kifanyike kwa dada anaejikuta katika situation ii na vijana wafanyaje ili wasihisi hawana nafasi kwa wadada waliowazidi status.
Mimi ni mmoja wa wasiogopa status ya mwanamke wa aina yoyote ila tu niwe na income ambayo ntaacha kodi ya meza na pango la nyumba, siku hizi waoga wengi, angalizo mwanaume alishe familia na alipe kodi ya nyumba yeye, kama anapesa basi awe na moyo wa kunipa kiasi cha pesa kikae kwenye account yangu pasipo masharti wala mikataba sijui nini wala nini. Mwaume lisha na lipa kodi hapo siogopi kiumbe ila unilishe na ulipe kodi halafu pocket inasumbua ntakula mzigo ntasepa tu kilazima
 
Wanawake mlio na vipato hamtaki kujishusha mnataka mpambane na wanaume ndo maana yote yanatokea hayo unatakiwa mwanamke ujishushe sasa hlo kwenu gumu.
 
Majibu someni hapa

 
Maneno ya wanawake wenye vipato huwa yanaumiza sana. Anakwambia wewe huna jeuri ya kunitunza mimi, mimi naweza kukuweka ndani na kukuhudumia, labda amekupigia simu umechelewa kurudi home anakwambia kwenda huko hata usiporudi mimi sijali. siku umetoka safarini bila ya kuleta kitu home badala ya kupokelewa unaambiwa si bora ungebaki hukohuko.Kuishi nao inahitaji uvumilivu sana ndo maana tuliambiwa tuishi na kwa umakini

Sent from my SM-A500H using JamiiForums mobile app
 
Asilimia kubwa ya wanawake waliowazidi kipato wanaume zao hujiona kuwa wao ndio babaz wa familia hivyo mambo ya heshima sijui kuhudumiwa sijui kuwa chini ya mwanaume utayasikia kwa makungwi tu.
 
HEKIMA
Bado naangaza macho kuona wanawake wenye uchumi uliosimama Kama ndoa zao zinadumu ??
 
wasababu hii mada ni story ya kweli ninachukua muda hasa kusoma na kutafakari mtazamo wa mwanaume juu ya kudate na mwanamke aliemzidi kipato.

Nimejivua uhusika nikasimama pembeni kuangalia Wanawake ambao mnawataka nyie kaka zetu sifa mlizoweka hajasoma sana au asiwe na kipato kukuzidi meaning wewe ndio umtunze na kuangalia mahitaji mengine.

Hili ni jambo jema kabisa hata mimi ningependa wa hivyo ila je mmewaza huyu unae taka awe goli kipa ndie mama wa watoto wako ? Ndio partner wako na ndio mtunza siri wako na mshauri wako?

Mnajua wanawake wa hivi siku mkifa hua wananyanyasika sana kwa kunyang'anywa mali, je nani atatunza wanao ikiwa mama yao hakua na kipato cha kutosheleza?

Siku ukiugua ni yeye atakaehangaika kukuhudumia wakati ndugu zako na marafiki zako hawakujali. Tena siku utakayo ugua ukamaliza fedha zote hadi kuuza baadhi ya mali ili ujitibie mwanamke huyu ndio atatakiwa ahakikishe bado unapata huduma ipasavyo na aangalie hapo ndani mnaishije?!

Nyinyi ni mashahidi namna familia inavyoteseka siku yule breadwiner akiugua au kufariki. Vipi kama angekua na kazi ambayo ingeweza kusupport mahitaji na matunzo ya hapo ndani?

Ninaifahamu familia ambayo mume aliugua haswaaa ikafika sehemu ambayo alihitaji kwenda India....hakua na bima wala kazini kwake hawakua na utaratibu wa kutibwa nje ya nchi ila baba huyu kilichomsaidia ni Bima nzuri ya kazini kwa mke kwake alipokua anafanya kazi ndio iliwezesha matibabu. Mwingine ni baba alikumbwa na hizi tumbua jipu za mwendazake pila alieshikilia mhimili na kuficha aibu ya familia ni mama. Watoto wanasoma, wanakula na maisha yanaendelea.

Tukiangalia nchi zingine baba haoni shida kua stayhome dad, yani anabaki nyumbani anatunza watoto mama ndio aende kazi ( Japo hii kiukweli hata mimi inanipa ukakasi hahahaha)

All in all sioni sababu ya mwanaume kuogopa kua mwanamke akimzidi kipato atamdharau au atapata wa level zake kikubwa mwanaume ajue namna ya kumtiisha mke wake lazima mwanaume accomand respect .

Mwanamke aliefundwa na mwenye akili atamzidi kipato mumewe lakini nyumbani atabaki kua mke na mama wa familia na kufanya yanayompasa kufanya.
 
Back
Top Bottom