Je wanyama na mimea wana roho (do animal and plants have soul)

Je wanyama na mimea wana roho (do animal and plants have soul)

SONGOKA

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
1,841
Reaction score
1,843
Wanadamu tunaamini katika maisha baada ya kifo, ingawa maisha haya yanapishana kutokana na dini mbalimbali, lakini kwa ujumla common ground ni kuwa tutaishi baada ya kufa. Msingi wa maisha baada yakifo ni imani kuwa mbali na viungo vyoote tulivyonavyo, pia tuna ROHO.

Na ni
msingi wa uwepo wa roho (soul) ndo unaojenga nadharia ya maisha baada ya kifo katika dunia mpya.
Kumekuwa na dhana na mtizamo tofauti katika wanyama na mimea linapokuja swala la roho. Wanazuoni wanaamini kuwa mimea na wanyama hawana roho na sifa hii ya mwanadamu ni kati ya sifa kuu zinazomtofautisha binadamu na wanyama au mimea.

Swali la kujiuliza ni Je,kama msingi wa imani ya uwepo wa roho kwa wanadamu unajengwa na imani ya maisha baada ya kifo. Na kwa kuwa maisha baada ya kifo ni dhana ya kidini kwa wafuasi wa Mungu mmoja.

Na ni roho ndo inaaminika kuwa huendeleza maisha kwa kwenda mbinguni
Je vitabu vya dinivinasemaje kuhusu uwepo wa wanyama na mimea katika dunia ya roho/ mbingu (ntazungumzia biblia, mwenye taarifa nakuran ntaomba achangie mtizamo huo) Isaya 65:25 "mbwa mwitu namwanakondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani kama ngo'ombe, na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka.

Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote" asema Bwana.
Nabii isaya anathibitishakuwa mbinguni kutakuwa na wanyama na anatoa mfano wa mbwa mwitu, kondoo, ng'ombe,simba, na nyoka. Ufunuo 19:14 pia Yesu anaonekana akirudi na jeshi lake la mbinguni huku akiwa juu ya FARASI mweupe.

Lakini pia Ufunuo 22:1-3 inaonyesha kuwa mbinguni patakuwa na miti. Je hii ni uthibitisho kuwa wanyama na mimea pia wana roho kamawanadamu, na kila wanyama na mimea wanapopoteza maisha roho zao huishi na pia huenda mbinguni kama wanadamu ili kungojea ile siku kuu ya Dunia mpya ya waliochaguliwa na Mungu pekee.

Karibuni.


CC Ishmael, Eiyer, Punjab Singh, Mkuu wa chuo
 
Kwanza namna viumbe vingine tofauti na Binadamu viliumbwa kwa Mungu kutamka tu,yaani neno ndilo lililoumba [Yesu],lakini binadamu aliumbwa au kwa lugha nyingine Mungu mkamilifu [nafsi zote tatu] zilihusika kwenye uumbaji wa mwanadamu na hata alivyoumbwa imeelezwa,kwa maana hiyo basi viumbe vingine vina uhai lakini havina roho

Nasema hivyo kwasababu Mungu ni roho na wakati anamuumba binadamu alisema kabisa "tumuumbe mtu kwa mfano wetu [roho]" lakini wakati anamuumba binadamu hakusema hivyo,kwa maana hiyo kama hakumuumba mbuzi au ng'ombe kwa mfano wake na Mungu ni roho basi hao wengine hawana ule mfanano wa Mungu ambao ni roho

Nikija kwenye hoja yako ya uwepo wa viumbe wengine baada ya maisha haya ni kwamba kwanza haijaelezwa kuwa vitafufuliwa hivi ambavyo leo vinakufa bali imeelezwa vitakuwepo kama hivi,sasa kwa maana hii ni kwamba inawezekana vitaumbwa vingine tofauti na hivi na tutaishi navyo milele bila kuharibika!
 
Kwanza namna viumbe vingine tofauti na Binadamu viliumbwa kwa Mungu kutamka tu,yaani neno ndilo lililoumba [Yesu],lakini binadamu aliumbwa au kwa lugha nyingine Mungu mkamilifu [nafsi zote tatu] zilihusika kwenye uumbaji wa mwanadamu na hata alivyoumbwa imeelezwa,kwa maana hiyo basi viumbe vingine vina uhai lakini havina roho

Nasema hivyo kwasababu Mungu ni roho na wakati anamuumba binadamu alisema kabisa "tumuumbe mtu kwa mfano wetu [roho]" lakini wakati anamuumba binadamu hakusema hivyo,kwa maana hiyo kama hakumuumba mbuzi au ng'ombe kwa mfano wake na Mungu ni roho basi hao wengine hawana ule mfanano wa Mungu ambao ni roho

Nikija kwenye hoja yako ya uwepo wa viumbe wengine baada ya maisha haya ni kwamba kwanza haijaelezwa kuwa vitafufuliwa hivi ambavyo leo vinakufa bali imeelezwa vitakuwepo kama hivi,sasa kwa maana hii ni kwamba inawezekana vitaumbwa vingine tofauti na hivi na tutaishi navyo milele bila kuharibika!

mkuu kumbuka uumbaji ni jambo ambalo halitajirudia.
 
Vyote story na nadharia tu hamna mwenye uhakika wowote au na kitu chochote kama ambavyo hujui ulijikuta vipi duniani na lini utakufa hivyo hivyo.ni lazima tukubali akili zetu ni limited
 
Bin adam atakapo kuwa peponi ataishi kwa mfumo wa roho kama viumbe vilivyopo huko, kama Ng'ombe, Tai na Mitende ya Duniani haina Roho basi nategemea kuna/kutakuwa na viumbe kwa mfumo huo eidha kwa kutumia roho za Malaika au Bin adam.
 
Kwa ushahidi upi mkuu?

kwa mujibu wa uumbaji wa biblia, baada ya Mungu kuumba vitu vyote aliviona ni PERFECT, na akakamilisha uumbaji wake na kupumzika. Perfect kwa hapa ni kwamba vinakidhi nadharia zote yaani nadharia ya kiroho/kimbingu na kimaumbile na Pia Kidunia.

kwa hiyo out of perfection there cant be another creation.
 
kwa mujibu wa uumbaji wa biblia, baada ya Mungu kuumba vitu vyote aliviona ni PERFECT, na akakamilisha uumbaji wake na kupumzika. Perfect kwa hapa ni kwamba vinakidhi nadharia zote yaani nadharia ya kiroho/kimbingu na kimaumbile na Pia Kidunia.

kwa hiyo out of perfection there cant be another creation.

Lakini hakukanusha kuja kufanya uumbaji mwingine sio?
 
Kwanza namna viumbe vingine tofauti na Binadamu viliumbwa kwa Mungu kutamka tu,yaani neno ndilo lililoumba [Yesu],lakini binadamu aliumbwa au kwa lugha nyingine Mungu mkamilifu [nafsi zote tatu] zilihusika kwenye uumbaji wa mwanadamu na hata alivyoumbwa imeelezwa,kwa maana hiyo basi viumbe vingine vina uhai lakini havina roho

Nasema hivyo kwasababu Mungu ni roho na [size=+2]wakati anamuumba binadamu alisema[/size] kabisa "tumuumbe mtu kwa mfano wetu [roho]" [size=+2]lakini wakati anamuumba binadamu hakusema hivyo[/size],kwa maana hiyo kama hakumuumba mbuzi au ng'ombe kwa mfano wake na Mungu ni roho basi hao wengine hawana ule mfanano wa Mungu ambao ni roho

Nikija kwenye hoja yako ya uwepo wa viumbe wengine baada ya maisha haya ni kwamba kwanza haijaelezwa kuwa vitafufuliwa hivi ambavyo leo vinakufa bali imeelezwa vitakuwepo kama hivi,sasa kwa maana hii ni kwamba inawezekana vitaumbwa vingine tofauti na hivi na tutaishi navyo milele bila kuharibika!

Mkuu Eiyer, hapo kwenye rangi sijakupata vizuri. Una maana gani?
 
Last edited by a moderator:
Kwanza namna viumbe vingine tofauti na Binadamu viliumbwa kwa Mungu kutamka tu,yaani neno ndilo lililoumba [Yesu],lakini binadamu aliumbwa au kwa lugha nyingine Mungu mkamilifu [nafsi zote tatu] zilihusika kwenye uumbaji wa mwanadamu na hata alivyoumbwa imeelezwa,kwa maana hiyo basi viumbe vingine vina uhai lakini havina roho

Nasema hivyo kwasababu Mungu ni roho na wakati anamuumba binadamu alisema kabisa "tumuumbe mtu kwa mfano wetu [roho]" lakini wakati anamuumba binadamu hakusema hivyo,kwa maana hiyo kama hakumuumba mbuzi au ng'ombe kwa mfano wake na Mungu ni roho basi hao wengine hawana ule mfanano wa Mungu ambao ni roho

Nikija kwenye hoja yako ya uwepo wa viumbe wengine baada ya maisha haya ni kwamba kwanza haijaelezwa kuwa vitafufuliwa hivi ambavyo leo vinakufa bali imeelezwa vitakuwepo kama hivi,sasa kwa maana hii ni kwamba inawezekana vitaumbwa vingine tofauti na hivi na tutaishi navyo milele bila kuharibika!

How dd you know that god is a soul ?.Tabia na namna mnavyomwelezea mungu wenu ni dhahili kabisa kwamba sio roho bali ni personal god idea mnayoijengea picha na kuipa sifa kedekede.Em fikilia roho unayoisema inaposses sifa kama hiz,
Mkono wa kuume,Uso,Image n.k

Pili,neno"" tumuumbe mtu kwa mfano wetu"" haikumaanisha roho kama ulivyoandika.Kwa maana hata katika maana rahisi na halisi hakuna mfano wa roho.Yaani image iwe soul hiyo haipo.

Halafu unaposema mbuz na ng'ombe au wanyama kwa ujumla hawatafufuka umejuaje na imeandikwa wapi?.Ndio maana nasema hisia zenu zinamuumba mungu ambaye kiuhalisia hayupo.Yaan umeamua tu mwenyewe kusema kwamba wanyama hawata fufuka kwa sababu hawakuumbwa kwa mfano wa mungu wenu.Basi ungetuambia wanyama wameumbwa kea mfano upi?.

kijana Thick twice !karibu kayika umwengu huru!
 
Mkuu Eiyer, hapo kwenye rangi sijakupata vizuri. Una maana gani?

Nilichokuwa namaa nisha ni kwamba,wakati Mungu anaumba wanyama na vingine alikuwa anasema "na awe sungura" na baada ya kusema hivyo sungura alikuwa anatokea,kwa maana nyingine aliehusika na uumbaji wa vingine vyote ni Yesu tu [neno] na Mungu baba wala Roho mtaklatifu hakuhusika

Kwa binadamu tukio lilikuwa tofauti kwani hakusema "na awe mtu" bali alisema "na tufan ye mtu kwa mfano wetu" na baada ya hayo binadamu hakutokea bado bali Mungu alii ngioa kazini na kumuumba binadamu,hapa tunaona Mungu akiumba kwa maana alihusika Mungu kwa maana ya utatu wake wote na ndio utofauti unapokuja kati ya kuumbwa kwa binadamu na vingine!
 
Kivipi????

uumbaji wa kwanza ulikuwa perfect kwa misingi kuwa unakidhi mahitaji ya dunia ya sasa na itakayokuja. so ukisema kutakuwa na uumbaji mwingine then utamaanisha ule wa kwanza haukukidhi mahitaji ya mbingu. so haukuwa PERFECT
 
How dd you know that god is a soul ?
Kwasababu alisema hivyo ..
.Tabia na namna mnavyomwelezea mungu wenu ni dhahili kabisa kwamba sio roho bali ni personal god idea mnayoijengea picha na kuipa sifa kedekede.Em fikilia roho unayoisema inaposses sifa kama hiz,
Mkono wa kuume,Uso,Image n.k
Mungu anauwezo wote na hakuna kinachomshinda,kama unamuwekea vizingiti kuwa hawezi kuwa hivi au vule huyo ni mungu wako wewe na sio ninaemjua mimi
Pili,neno"" tumuumbe mtu kwa mfano wetu"" haikumaanisha roho kama ulivyoandika.Kwa maana hata katika maana rahisi na halisi hakuna mfano wa roho.Yaani image iwe soul hiyo haipo.
Unaizungumzia picha kama ile ambayo unaweza kupiga kutoka kwenye camera ya simu yako?
Halafu unaposema mbuz na ng'ombe au wanyama kwa ujumla hawatafufuka umejuaje na imeandikwa wapi?.Ndio maana nasema hisia zenu zinamuumba mungu ambaye kiuhalisia hayupo.Yaan umeamua tu mwenyewe kusema kwamba wanyama hawata fufuka kwa sababu hawakuumbwa kwa mfano wa mungu wenu.Basi ungetuambia wanyama wameumbwa kea mfano upi?
.
Nilichokisema hapo mwanzo kinafanya hili swali lako liwe na hovyo kwasababu kama hawana roho [mfanano wa Mungu] nini kinakufanya udhani kuna ufufuo baadae kwaajili ya hivyo?

Halafu hivi unajua hata ufufuo upo kwaajili ya nini?
kijana Thick twice !karibu kayika umwengu huru!
Nimekujibu kwasababu moja tu nayo ni kwamba kuna watu wanaweza kusoma hii post yako na kujiuliza maswali kuhusu jibu langu,ukija na maswali yako ya bla bla ya kuthibitisha bla bla sitakujibu kwasababu hii sio mada kwaajili ya hayo

Mtoa mada anataka kujua kama viumbe vingine vina roho au laa!
 
uumbaji wa kwanza ulikuwa perfect kwa misingi kuwa unakidhi mahitaji ya dunia ya sasa na itakayokuja. so ukisema kutakuwa na uumbaji mwingine then utamaanisha ule wa kwanza haukukidhi mahitaji ya mbingu. so haukuwa PERFECT

Kwani parfect maana yake nini?
 
Bear in mind, biblically! hayo majina ni adamu ndio aliwapa.
 
Kila kinachokufa kina roho,
Tofauti ya binadamu na viumbe wengine ni maumbile na akili
 
Back
Top Bottom