Je, wapinzani ni wakombozi?

Je, wapinzani ni wakombozi?

We Masatu

Acha kunizulia mambo ati. Tanzania Njema amesema CCM inajisafisha kwa kuondokana na rushwa; mimi nisema katu asilani CCM ni ile ile yenye kukumbatia rushwa. Waanzie wapi kujisafisha ili hali wameingia kwa rushwa? Waanze wapi kujisafisha chamani wakati serikalini wanajichafua kwa rushwa? Waanze wapi kujisafisha chamani wakati chaguzi za chama mwaka huu toka chini zilikuwa na rushwa? Lakini wasema upinzani ujisafishe; lini upinzani umejichafua kwa rushwa kama CCM ili ujisafishe?

Msinitie vidole vya macho Asha mie. Nataka tu mnieleze nielewe, na mnanijua humu-nikielezwa nikaelewa huwa nakubali kuelewa.

Hivi Masatu nawewe CCM? Nishawishi basi nami nijiunge. CCM ya Kikwete ina lipi jipya?

Asha

Bibie,

Labda hapa tukubaliane kutokubaliana, mtazamo wangu kuhusu posting ya TN ni kama nilivyoeleza hapo juu, kimsingi nakubaliana na alichosema TN, hata hivyo hayo ni maoni yangu kama mtu binafsi.

Kwa upande mwingine naheshimu mawazo yako ingawa sikubaliana nayo.

Suala kama mimi ni CCM au la nadhani hilo langu binafsi na halitakusaidia kama utajua, kwa msingi huo huo swali la ushawishi wangu kwako kujiunga na CCM nitakuwa nimelijibu pia
 
Hivi vyama vya upinzani kujisafisha lazima mpaka wasubiri CCM wajisafishe?

Hayo mambo mawili inatakiwa yaende sambamba. CCM ni chafu na wanakula na kupokea rushwa. Upinzani pia kuna uchafu, wanaongoza vyama kama kampuni zao za mifukoni. Wanatafuna ruzuku badala ya kuzitumia kuendeleza wananchi nk.
 
hivi mchochezi ni mwizi au ni yule raia mwema anaye mwambia mwenzie, kuwa unaibia. mimi naona mwizi ndio mchochezi, so manumba kamata wezi.
hii ni sawa sawa na wale wezi wa kwenye daladala, anamwibia abiria mwezio, wewe unaona unamtonya jamaa kwamba unaibia, then wezi wana kurudi wewe.
 
Hivi vyama vya upinzani kujisafisha lazima mpaka wasubiri CCM wajisafishe?

Hayo mambo mawili inatakiwa yaende sambamba. CCM ni chafu na wanakula na kupokea rushwa. Upinzani pia kuna uchafu, wanaongoza vyama kama kampuni zao za mifukoni. Wanatafuna ruzuku badala ya kuzitumia kuendeleza wananchi nk.

We Mtanzania

CCM wamekiri wenyewe kuwa watu wao wanato rushwa na sasa wanaanza kujisafisha.

Tupe hoja zinazothibitisha kwamba wapinzani wanaendesha vyama kama kampuni zao na kwamba wanatafuna ruzuku badala ya kutumia kuwaendeleza wananchi(sheria ya vyama vya siasa haisemi kwamba ruzuku ni kwa ajili ya kuwagawia wananchi, inasema ruzuku ni kwa ajili ya kuendesha vyama tu).

Na katika kutoa hoja zako uchambua chama kwa chama badala ya kusema tu upinzani kwa ujumla kaka.

Vyama vya upinzani vinavyopokea ruzuku ni hivi hapa na navipanga kwa kadiri ya uwingi wa ruzuku wanazopokea.

1. CUF

2. CHADEMA

3. UDP

4. TLP

5. PPT Maendeleo(kwa kuwa na diwani mmoja).

Sasa jenga hoja yako kwa chama kimoja baada ya kingine. Kile kitakachoonekana kuwa hakina rushwa ama ubadhirifu wa ruzuku hicho ndicho tukiamini na kukipa uongozi badala ya CCM kwa kuwa Masatu amekwepa kunithibitishia ni kwa vipi CCM anayoitetea haina RUSHWA.

Masatu we wangu, naomba unijibu-ni kweli CCM imebadilika na sasa imeweka pembeni rushwa.

Aie wewe nijibu basi, usichukie. Hoja hujibiwa kwa hoja.

Asha
 
Mimi najiuliza sana na labda kupata majibu kwamba sasa RA atakuwa kesha kamilisha mpango wake wa kumbana Zitto. Maana kwa CCM hii ni vita kwao kutaka Wadanganyika wasijue lolote . CCM na Polisi watafanya kosa kubwa sana kumkamata Zitto leo kwa hoja tete kama hii. Au kama polisi wameamua kuingia kwenye siasa fine .
 
Sasa jenga hoja yako kwa chama kimoja baada ya kingine. Kile kitakachoonekana kuwa hakina rushwa ama ubadhirifu wa ruzuku hicho ndicho tukiamini na kukipa uongozi badala ya CCM kwa kuwa Masatu amekwepa kunithibitishia ni kwa vipi CCM anayoitetea haina RUSHWA.

Masatu we wangu, naomba unijibu-ni kweli CCM imebadilika na sasa imeweka pembeni rushwa.

Aie wewe nijibu basi, usichukie. Hoja hujibiwa kwa hoja.

Asha

Bibie,


Sina sababu ya kuchukia afterall hii baraza ya kubadilishana mawazo.
Hakuna mahala niliposema kuwa CCM imeacha rushwa, ukifuatilia kwa makini mjadala toka mwanzo kama ulivyoanzishwa na TN nilichosema ni kuwa kuna some changes (japo kidogo) ktk suala zima la vita dhidi ya rushwa ndani ya CCM.

Yawezekana ikawa ni danganya toto (kama alivyosema mchangiaji mmoja)hata hivyo hoja yangu ilikuwa ni wapinzani waichukulie hali ya hii kama ni changamoto na kujipanga vizuri.
 
Bibie,


Sina sababu ya kuchukia afterall hii baraza ya kubadilishana mawazo.
Hakuna mahala niliposema kuwa CCM imeacha rushwa, ukifuatilia kwa makini mjadala toka mwanzo kama ulivyoanzishwa na TN nilichosema ni kuwa kuna some changes (japo kidogo) ktk suala zima la vita dhidi ya rushwa ndani ya CCM.

Yawezekana ikawa ni danganya toto (kama alivyosema mchangiaji mmoja)hata hivyo hoja yangu ilikuwa ni wapinzani waichukulie hali ya hii kama ni changamoto na kujipanga vizuri.


Wooh, ndio maana nakupenda Masatu

Hizo 'some changes' ni zipi?

Kama inawezekana ni danganya toto kama ulivyosema kwa hiyo wapinzani nao wajipange kufanya danganya toto?

Kwa nini wapinzani wasijipange kusema kwamba CCM inafanya danganya toto?

Nashukuru kwamba huna hasira.

Asha
 
Nadhani TanzaniaNjema ameleta changamoto nzuri sana kwa vyama vya upinzani. Kama nitakuwa nimemuelewa vizuri anachotaka kusema hapa ni kuwa kuna some changes ndani CCM ( Japo ndogo sana) katika suala zima la vita dhidi ya rushwa, kwa mtazamo wake kama wapinzani hawatajipanga vizuri ( na wao kusafisha nyumba zao) CCM itawapiga bao.

La msingi hapa ni kuifanyia kazi changamoto hii, badala ya kuanza kulaumu CCM kuwa ni danganya toto, dharau kama hizi zaweza kuwa na athari kubwa kwa ustawi wa upinzani.

Masatu

Bado niko nawe mpenzi

Hapa tulikuwa tunajadili kuhusu rushwa ndani ya CCM; umesema hapo juu kuwa wapinzani nao wanapaswa kusafisha nyumba zao. Ni uchafu upi wa rushwa upo kwa kila chama cha upinzani?

Asha
 
Masatu

Bado niko nawe mpenzi

Hapa tulikuwa tunajadili kuhusu rushwa ndani ya CCM; umesema hapo juu kuwa wapinzani nao wanapaswa kusafisha nyumba zao. Ni uchafu upi wa rushwa upo kwa kila chama cha upinzani?

Asha

Bibie,

Nisingependa kugeuza ukumbi huu kuwa ni court chamber kwa cross examination.

Suala la some changes unless unaishi sayari nyingine na huna habari na yanayoendelea hivi sasa kwenye vyombo vya habari nk.

Kusafisha nyumba za upinzani kunabeba mambo mengi zaidi ya rushwa, masuala ubadhirifu ktk vyama (huko Chadema kulikuwa na kitimtim mara baada ya uchaguzi) undugunization, kauli za vitisho na za kuhatarisha amani ( Mbowe) nk.

Kwa ujumla hoja yangu hapa ni kuwa wapinzani wajipange vizuri ku counter hii move ya CCM

Kama msimamo wako ni kuwa vyama vya upinzani (kwa ujumla wake) ni clean na havina hayo niliyoyasema then bravo sis...
 
Labda itatusaidia kama tutaweza kuonesha hayo ambayo wapinzani wanatakiwa nao wajisafishe. Kwa mfano, kwa CCM tumesema wazi kuwa kuna rushwa kwa sababu wamekatamatana wao wenyewe wakipeana rushwa kupitia hiyo PCCB yao. Sasa unaposema wapinzania wajisafishe, kwa nini pia usiwe specific kwa kusema kwa hili na lile kama ambavyo tumekuwa tukifanya kwa CCM?

Haya nimeona pia Mtanzania amesema, pamoja na mambo mengine, kuwa wapinzani "wanatafuna ruzuku badala ya kuendeleza wananchi", sasa this is a serious allegation. je, ni kweli kwamba wapinzani wanatafuna ruzuku, hapa nafikiri anamaanisha kuiba au kutumia hiyo ruzuku kwa manufaa binafsi badala ya kuendeleza hivyo vyama vyao, je ana ushahidi wowote na hili? Au msajili wa vyama ametoa report inayoonesha kuwa viongozi wa upinzani wameiba hela za ruzuku? Halafu unaposema "badala ya kuendeleza wananchi", je, tumejibidisha kujua hasa kazi ya hii pesa ya ruzuku kwa vyama vya siasa ni nini?

Otherwise, naogopa kwamba tutakuwa tunatoa blanket allegations ambazo lengo linaonekana sio kusaidia sana katika kupambana na ufisadi nchini mwetu bali kuhalalisha kwamba vyama vingine navyo ni vichafu kama CCM, wakati, in the absence of credible evidence, sio kweli!
 
jamani ebu nipeni tofauti ya UCHOCHEZI na KUHAMASISHA wananchi KUTETEA rasilimali zao,hawa kina manumba wametumwa na nani?

naona ni yale yale ya kina Nyerere na wakoloni,yaani hizi harakati za kina mbowe zinaleta woga na wasiwasi kwa ccm kama enzi zile za kudai uhuru na ccm sasa wanajiandaa kutumia silaha "YAO" ambayo wanacnhi WOTE huwa tunailipia kodi;POLISI

Wasi wasi wangu ni kwamba CCM wanataka jifunga goli la pili kwa kutumia polisi! Subirini tuone

Sidhani kama kuna mtanzania ambaye bado aniona hiyo amani na utulivu wakati kunywa chai mpaka alazwe muhimbili apewe ushauri wa daktari, make bei kilo moja sh. 1500?? kwahiyo chai siku hizi anasa!
 
Unajua nilisha sema kwamba Mtanzania ana yale ajenda. Nakuheshimu sana rafiki yangu Mtanzania lakini kuanza kubadilsha mwelekeo wa mada ili kuidhoofisha ndiyo mbinu zenu za ki CCM.Mlishasema Chadema ni mali ya mtu lakini watu wakauliza mlete ushahidi kama kweli si Chama cha Kitaifa hadi leo mko kimya . Baada ya kuona mmefanikiwa kuwayumbisha watu kwamba CUF ni wadini mnahamia sasa Chadema mara ruzuku kwenye vyama mara Chama kampuni nk. Leo CCM kuanzia JK , Mkewe , mwanae na mpwa ama mjomba wake wako kwenye uongozi mkubwa ndani ya CCM , watu wakauliza mkasema wana haki kikatiba , tukisema JK sasa kafanya CCM kuwa kampuni mtasemaje ?
 
Ninajua baadhi ya watu toka Usalama na Police HQ na Immigration ni wanachama hapa . Sasa nawashauri wajaribu kuwapa ushauri wakubwa wao juu ya maneno ya amani na utulivu .Wote tuna elewa maana ya maneno haya na faida na hasara zake lakini why watu sasa wanaanza kuongea mambo openly ? Ni bora hata Mbowe anasema lakini kuna ambao hawasemi wanajipanga tu sasa kweli hakuna haja ya kupeana haki sawa kwa wote ?
 
Ninajua baadhi ya watu toka Usalama na Police HQ na Immigration ni wanachama hapa . Sasa nawashauri wajaribu kuwapa ushauri wakubwa wao juu ya maneno ya amani na utulivu .Wote tuna elewa maana ya maneno haya na faida na hasara zake lakini why watu sasa wanaanza kuongea mambo openly ? Ni bora hata Mbowe anasema lakini kuna ambao hawasemi wanajipanga tu sasa kweli hakuna haja ya kupeana haki sawa kwa wote ?

ni kweli kabisa,raia wengi hawataki kuongea kwa sababu either wamebanwa sana ila wanasubiri mtu mmoja tu AJITOLEE kuwaongoza,na nadhani huu ndio wasiwasi wa serikali (CCM?)mpaka wameamua kutumia mbinu mmbovu kabisa iliyopitwa na wakati,ETI polisi wachunguze maneno ya UCHOCHEZI.kama manumba anaipenda sana nchi hii kwa nini wasijitolee kuchunguza ufisadi na ubadhirifu wa kutisha huko BoT,Kiwira,etc?fine,kama wameingia siasa watuambie itikadi yao ni ipi...naomba kuwasilisha hoja...
 
Lunyungu,

Hilo ndilo tatizo lenu la kuwa na mawazo kama akina Bush "You are either with us or with the terrorists" Tukiwasema CCM mnashangalilia, tukiongelea CHADEMA au upinzani mnaanza kutupachika majina na kutuvisha uanachama.

Siku nitakayoamua kuwa mwanachama wa chama cha siasa nitasema wazi na sina cha kuficha.
 
WANA JF
Ningeomba mnisaidie, nini maana ya "uchohcezi" kwa tafsiri inayotumiwa hapa. Maana hilo neno linatumika vaguely, what actually entails "uchochezi"?. Ukiwashawishi watu waahce ujinga ni uchochezi? Ukivaa kimini ni uchochezi? maana hasa ya hili neno ni nini? Ukiwaambia watanzania peace and harmony without prosperity is madness, ni uchochezi? Au ndio maneno yaliyopo kwenye katiba yenye lengo la kuwashughulikia watu?
 
Wacha tuone tafsiri inaendaje toka kwa hao walio nao jirani .
 
Labda itatusaidia kama tutaweza kuonesha hayo ambayo wapinzani wanatakiwa nao wajisafishe. Kwa mfano, kwa CCM tumesema wazi kuwa kuna rushwa kwa sababu wamekatamatana wao wenyewe wakipeana rushwa kupitia hiyo PCCB yao. Sasa unaposema wapinzania wajisafishe, kwa nini pia usiwe specific kwa kusema kwa hili na lile kama ambavyo tumekuwa tukifanya kwa CCM?

Haya nimeona pia Mtanzania amesema, pamoja na mambo mengine, kuwa wapinzani "wanatafuna ruzuku badala ya kuendeleza wananchi", sasa this is a serious allegation. je, ni kweli kwamba wapinzani wanatafuna ruzuku, hapa nafikiri anamaanisha kuiba au kutumia hiyo ruzuku kwa manufaa binafsi badala ya kuendeleza hivyo vyama vyao, je ana ushahidi wowote na hili? Au msajili wa vyama ametoa report inayoonesha kuwa viongozi wa upinzani wameiba hela za ruzuku? Halafu unaposema "badala ya kuendeleza wananchi", je, tumejibidisha kujua hasa kazi ya hii pesa ya ruzuku kwa vyama vya siasa ni nini?

Otherwise, naogopa kwamba tutakuwa tunatoa blanket allegations ambazo lengo linaonekana sio kusaidia sana katika kupambana na ufisadi nchini mwetu bali kuhalalisha kwamba vyama vingine navyo ni vichafu kama CCM, wakati, in the absence of credible evidence, sio kweli!

Kitila at aleast sasa tunaanza kuongea substance.

Hoja zako ni nzuri sana, kosa kubwa tunalolifanya hapa ni kufikiri upinzani ni Chadema na Chadema ndio upinzani (haijaandikwa popote bali ni observation yangu tu), niliposema wapinzani (kwa ujumla wao) wasafishe nyumba zao kwanza nilikuwa nalenga pamoja na mambo mengine yafuatayo;

1. Demokrasia ndani ya vyama, tumeshuhudia Mrema na Cheyo wanavyoendesha vyama na kufukuza viongozi na wanachama kila wanapopingana kimawazo.

2. Migogoro na uchu wa kugombea madaraka ( same as above)

3. Matumizi mabaya ya Ruzuku ( mfano Mrema kajinunulia nyumba Sinza na katangaza chama kimemuenzi na kumpa)

4. Kauli vitisho zenye kuhatarisha amani na utulivu ( Mbowe, CUF, nk)

5. Kujiimarisha na kuwa na mtandao mzuri wa matawi nchi nzima kwa vyama vyote ( Mfano uchaguzi uliopita kuna majimbo kadhaa wapinzani hawakusimamisha wagombea kwenye ubunge na kwenye Udiwani ndio zaidi)

6.Harufu ya Udini (CUF)

7. NK
 
ni kweli kabisa,raia wengi hawataki kuongea kwa sababu either wamebanwa sana ila wanasubiri mtu mmoja tu AJITOLEE kuwaongoza,na nadhani huu ndio wasiwasi wa serikali (CCM?)mpaka wameamua kutumia mbinu mmbovu kabisa iliyopitwa na wakati,ETI polisi wachunguze maneno ya UCHOCHEZI.kama manumba anaipenda sana nchi hii kwa nini wasijitolee kuchunguza ufisadi na ubadhirifu wa kutisha huko BoT,Kiwira,etc?fine,kama wameingia siasa watuambie itikadi yao ni ipi...naomba kuwasilisha hoja...

Ibambasi, mbona itigadi yao ipo wazi huna haja ya kutafuta tochi.
 
Kitila,
Unataka hata nyie CHADEMA mpaka mkamatwe na PCCB ndio mjue au msafishe mapungufu yenu?

Mengi niliyotaka kuandika naona Masatu kayaandika.

Pia nafikiri kwa CHADEMA kuna malalamiko kuhusu ugawaji wa nafasi za ubunge kwa wanawake.

Kulikuwa na suala la viongozi wengi kutoka Kilimanjaro lakini nafikiri hili mmelishughulikia na sasa kamati kuu yenu inawakilisha karibu nchi nzima. Huko ndiko kujisafisha tunakokusema, sio lazima kusubiri PCCB.
 
Back
Top Bottom